BekaNurdin
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 2,267
- 2,041
Hatudanganyiki ng'o!Wizara ya Afya kesho watatoa tiketi za bure za mechi ya Simba na Yanga kwa wale watakaokubali kuchanja siku ya kesho.
Kwanza kabisa naipongeza Wizara ya Afya kwa ubunifu huu, ila kuna jambo litaonekana haliko sawa.
Chanjo ya corona ikiendelea kuwekewa zawadi hizi ni kutengeneza zaidi mashaka badala ya kupunguza mashaka.
Wapo wataojiuliza kwa nini iwe hivi?
Wizara ilipaswa iendelee kutoa elimu juu ya watu kupata chanjo. Ila kuweka hizi zawadi kunazidisha maswali.
Wizara haioni kwamba wale waliochanja na ni wapenzi wa soka, hawana uwezo wa kununua tiketi watakuwa wanajilaumu sana?
Yote kwa yote kila la kheri!
View attachment 1951083