Wataalamu watuambie,nini matokeo ya kuvunja katiba?

kibaravumba

JF-Expert Member
Dec 21, 2012
6,635
7,005
Mara nyingi naona baadhi ya watu wakilalamika kuhusiana na suala la kuvunjwa kwa katiba katika maamuzi mbali mbali.Kuvunjwa huku kumekuwa kunafanywa na wale walioapa kuilinda na kuitetea katiba.Sasa nina maswali yafuatayo;

1.Kwa nini watu huapa kwa dini ama imani yao wanapopewa madaraka na kuahidi kuilinda katiba?Nini madhara ya kutotimiza kiapo?

2.Iwapo mtu atavunja katiba makusudi ama kwa kutojua,nini kitatokea?Hiki kitakachotokea mbona watu hawakiogopi kama kweli kipo?

3.Je utaratibu wa kuapa kwa wakristo,hawaoni kuwa ni kinyume na biblia yenyewe mtu anayotumia kuapa kwani imeandikwa "msiape"?

4.Je ni lazima kuwepo kwa katiba ambayo wala haitekelezwi au inapuuzwa?
 
Mtu anapoapa kwa kumuomba Mungu amsaidie lakini akakaidi ni sawa na kujipalia mkaa wa moto kichwani
 
Angalia maisha yao baada yao baada ya muda Wao kuisha. Wanaishi maisha kama ya tu mbili. Wanakua wapole na wanakufa na kutoweka kwenye USO wa Dunia japo kimwili tunakua nao bado
 
Nashukuru ila naona kama matokeo yanayosemwa ni ya kufikirika zaidi.Kuna watu waumini wazuri lakini hawamwamini Mungu,anaweza kuua ama kuagiza kuua na anachokifanya kuepuka maruwe ruwe anaenda kwa sangoma tu.Sasa sababu ya kisomi ni ipi hadi mtu aapishwe na akivunja kiapo nini kinampata?
 
Dini yangu inasema ukiapa tena kwa kumshirikisha Mungu halafu usifanye yale uliyoapia ukifa jehenam inakuhusu.
 
Back
Top Bottom