Wataalamu wa UN: Korea Kaskazini yaiba mamilioni ya dola kupitia udukuzi mitandaoni

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,495
9,275
1644311395097.png

Wataalam wa Umoja wa Mataifa wamesema kwenye ripoti yao kwamba Korea ya Kaskazini inaendelea kuiba mamilioni ya dola kutoka katika taasisi za kifedha na makampuni yanayojihusisha na sarafu za mitandao na ubadilishanaji fedha.

Wataalamu hao waliowanukuu wataalamu wa masuala ya mitandao kwenye ripoti yao, wamesema fedha hizo za wizi zimekuwa muhimu kwa Pyongyang kufadhili miradi yake ya nyuklia na makombora.

Jopo la wataalam la Umoja wa Mataifa limesema kulingana na duru ambazo hazikutajwa serikalini, wadukuzi wa mitandao wa Korea Kaskazini waliiba zaidi ya dola milioni 50 kati ya mwaka 2020 na katikati ya mwaka 2021.

Fedha hizo ziliibwa kutoka mashirika yasiyopungua matatu ya ubadilishanaji fedha yaliyoko Amerika ya kaskazini, Ulaya na Asia, kitendo ambacho huenda kinaakisi njama ya Korea Kaskazini kujumuisha uhalifu wa mitandao kwenye operesheni zake.

Wataalamu hao wamesema kwenye ripoti yao kuhusu uhalifu wa mitandao, kwamba kampuni moja ya usalama wa mitandao ambayo haikutajwa jina iliripoti kwamba mnamo mwaka 2021, wadukuzi wa mitandao wa Korea Kaskazini waliiba jumla ya dola milioni 400 za sarafu za kidijitali.
 
kiduku ana washinda kwa Tech, halafu Kuna mtu yupo manzese huko anasema kiduku Hana lolote
 
Back
Top Bottom