Kipeperushi
Senior Member
- Aug 17, 2011
- 167
- 33
Hivi karibuni nilibahatika kutembelea wilaya tatu zilizopo katika mkoa wa Mtwara na miongoni mwa mambo mapya kwangu niliyojifunza, hususani katika masuala ya ujenzi, ni matumizi ya matofali yaliyotengenezwa kutokana na mchanganyiko wa cement na udongo wa kichuguu (mfinyanzi). Kinachoangaliwa hapo ni uwezekano wa kupata matofali mengi zaidi kwa mfuko mmoja wa cement pale unapotumia mfinyanzi ikilinganishwa na unapotumia mchanga wa kawaida. Ninachoomba kujuzwa toka kwenu ni usahihi wa mtazamo huu wa uchanganyaji cement na mfinyanzi. Je, unakubalika kisayansi? Na kama inakubalika ratio sahihi ni ipi kwa mfuko mmoja? Natanguliza shukrani zangu kwa mchango wowote wa mawazo toka kwenu.