Wataalamu wa ubuntu pitieni hapa

Xiang Hao

Senior Member
Nov 19, 2016
126
97
Habari wanandugu pande zote za ulimwengu naombeni msaada wenu hapa siku tano zilizopita nime install UBUNTU kwenye laptop yangu lakini kutokana na kutokujua ninachokifanya ilipelekea kufuta vitu vyangu vyote.

Ila hilo sikuliwaza sana kwa sababu nilikuwa na vitu kidogo na pia sijatumia gharama kubwa kuzipata hivyo jana nikaamua kupiga windows 10 na Ubuntu sasa balaa likaanzia hapa kwanza ubuntu kuitumia siwezi lakini naipenda maana mara yangu ya kwanza kuitumia ilikuwa ni mwaka 2011 kwa brother wangu from another mother na sijui nilikuwa natumia Ubuntu ngapi lakini kwa sasa natumia ubuntu 13.10.

Tatizo langu kwenye ubuntu nashindwa ku install program na pia kwenye windows 10 imekuwa nikiitumia kwa muda kidogo hata kama ni dakika 5 tu inakuwa nzito mno, Pia upande wa mouse kwenye 10 inakuwa nzito ila hili lilikuwa kuanzia nanunua hii laptop lakini kwenye ubuntu ipo makini kabisa. msaada wenu naomba je nimekosea wapi? upande wa windows 10 na upande wa ubuntu naomba mnijuze jinsi ya kuitumia japo kuistall program mpya.

Natanguliza shukrani.
 
kuistall software kwenye ubuntu nenda kwenye software manager fungua hapo kwenye all packages kisha tafuta program unayoitaka na ufanye installation
 

Attachments

  • ubuntu.png
    ubuntu.png
    77.1 KB · Views: 54
kuistall software kwenye ubuntu nenda kwenye software manager fungua hapo kwenye all packages kisha tafuta program unayoitaka na ufanye installation
je naweza kupakua app bila ku upgrade hii 13.10?
 
Tafuta software inayoweza Wine then itakuruhusu kuinstall programs nyingine kama kawaida. Mfano office nk
 
natumia ubuntu 13.10
Ubuntu 13.10??kwanii unatumia hiyo version?for the record official support ilisitishwa bade ya mizen 6 took kuwa released! Ubuntu ina Long Term Support (LTS) releases ambazo zinakua na official 5 years support,,Kama ni novice,ni vizur kuinstall LTS version mostly likely kuepusha matatizo ambayo kuyatatua (as a novice)ni ngumu na community haitoi official support(help),,its best ku upgrade to v14.04 or most likely v16.04

lakini kila nikijaribu naambiwa net ipo chini wakati kwenye windows 10 napakua vitu bila shida
Odds ni kwamba utakua na tatizo na network configuration zako,,unapta error gani??
 
Ubuntu 13.10??kwanii unatumia hiyo version?for the record official support ilisitishwa bade ya mizen 6 took kuwa released! Ubuntu ina Long Term Support (LTS) releases ambazo zinakua na official 5 years support,,Kama ni novice,ni vizur kuinstall LTS version mostly likely kuepusha matatizo ambayo kuyatatua (as a novice)ni ngumu na community haitoi official support(help),,its best ku upgrade to v14.04 or most likely v16.04


Odds ni kwamba utakua na tatizo na network configuration zako,,unapta error gani??
shukrani sana mkuu leo nimekomaa kodwnload 16.04 sasa nateleza tu kweli ile 13,10 ni jipu
 
shukrani wote ndugu zangu kwa kunisapoti na kunisaidia mungu awalipe na kuwazidishia elimu yenye manufaa
 
Mkuu, nimeona unajaribu kuinstall 16:04, jaribu kuinstall software manage inaitwa "Synaptic Package Manager". Hii unaweza kuinstall kupitia Software Center. Kama hiyo itashindikana, tumia TERMINAL app.

Hapo una type;

sudo apt install synaptic (press enter) acha imalize.

Ikimaliza una fungua hiyo synaptic app ambayo itakuwezesha kuistall app zozote zilizo kuwepo kwenye repository ya ubuntu.

Jaribu kugoogle Ubuntu repository, kujifunza zaidi jinsi ya kuistall app ambazo huzipati kwenye Ubuntu repositories.
 
mkuu hapo kwenye windows 10 specs za laptop yako unaweza kuzitaja?

na ubuntu ina store yake ya software just one click una install na ku remove apps

How to Easily Add and Remove Programs in Ubuntu 14.04
Mkuu mimi nilikuwa natumia window 7 baadaye microsoft walitoa ofa ya kuupgrade kwenda window 10 sasa sijajua wakati naupgrade imeingia na virus maana iko nzito Sana na antvirus nimeupdate ile window defender lakini niki scani inaonyesha hakuna virus inaweza kuwa ni tatizo gani?
 
Mkuu, nimeona unajaribu kuinstall 16:04, jaribu kuinstall software manage inaitwa "Synaptic Package Manager". Hii unaweza kuinstall kupitia Software Center. Kama hiyo itashindikana, tumia TERMINAL app.

Hapo una type;

sudo apt install synaptic (press enter) acha imalize.

Ikimaliza una fungua hiyo synaptic app ambayo itakuwezesha kuistall app zozote zilizo kuwepo kwenye repository ya ubuntu.

Jaribu kugoogle Ubuntu repository, kujifunza zaidi jinsi ya kuistall app ambazo huzipati kwenye Ubuntu repositories.
NATYPE WAPI MKUU sudo apt install synaptic
 
Mkuu mimi nilikuwa natumia window 7 baadaye microsoft walitoa ofa ya kuupgrade kwenda window 10 sasa sijajua wakati naupgrade imeingia na virus maana iko nzito Sana na antvirus nimeupdate ile window defender lakini niki scani inaonyesha hakuna virus inaweza kuwa ni tatizo gani?
1. hakikisha ume update driver zote muhimu
2. ikiwa slow bonyeza ctrl+alt+delete nenda task manager halafu angalia kitu gani kimejaa hadi pc ipo slow
 
Back
Top Bottom