Wataalamu na wajuzi wa Redio naomba msaada wenu

Llio 002

JF-Expert Member
Jul 14, 2015
1,615
2,031
Mambo vipi wana jamvi, nna redio yangu LG xboom mini Hifi ina spika mbili sasa nilikuwa nna wazo la kutafuta spika zingine za JBL ili niunganishie kwenye hii redio nisiwe natumia hizi za Lg jee inawezekana?

Kiuhalisia Redio ipo vizuri inatema sound yakutosha tu naenjo haya mengine nnayoyahitaji ni manjonjo tu.

Mwenye ushauri napokea.

Nb: uwezo wa speker za Lg ni 3 nini sijuwi
 
Usibadilishe wala usiongeze speaker. Kila redio inakuja na speaker zilizopimwa kwaajili yake katika vitu vifuatavyo.
_ nguvu ya speaker na ukinzani (Power and resistance).
_mipaka itakayomudu (Frequency responce).

_Namna speaker zilivyofungwa kulingana na aina ya muziki unaozalishwa na amplifier husika. Hapa kuna mechanism ya speaker kuwa LEFT /RIGHT na pia kuna mechanism ya Response ya signal (+) na signal (-) yaani inaitwa PUSH/PULL . ukiangalia kwa makini utaona katika mapigo ya speaker kwa wakati mmoja, kuna wakati baadhi zinapiga kutoka nje na nyingine zinarudi ndani kutegemeana na aina ya Redio.

Redio kama hizi pia zimewekwa protection ya kutambua kama kuna shoti kwenye moja ya speaker zake endapo kuna speaker itakayokuwa na restistance tofauti na ile iliyotegemewa , sasa ukifunga speaker tofauti pia redio inaweza kuonyesha tabia za ajabu ikiwemo overheating, au kuTrigger shot circuit signal pia inaweza kuyoa muziki usiokuwa bora ingawa unaweza kuwa mziki mkubwa.
 
Nataka nijue watts za spika alizo nunua,siyo redio maana ya redio hawezi kujua kama sio expert wa electronics
 
Back
Top Bottom