Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 15,997
Nyerere alipata kusema ''mzungu anakupa kipande cha chupa na wewe unampa almasi kisha unakimbia kama zuzu''...pili, wabongo wengu humuamini mtu anayezungumza kiingereza."Carbon dioxide produced during smelting of Copper Concentrate can result into acid rain, which is harmful to plants".
Naunga mkono hoja. Hao walioandika mambo haya watafutwe wafunguliwe kesi ya kuhujumu uchumi.
Lakini kama watu wamehongwa kuruhusu wizi wa mahela yote hayo, basi kuna watu wana hela sana jamani. Au huwa wanahongwa bila kujua thamani ya kile wanachoruhusu, hivyo kushindwa kukadiria kiasi cha mlungula wanachostahili? Maanake unaweza kukuta Waziri aliahidiwa ufadhili wa kumsomesha bintiye ughaibuni, akadondoka signature. Nina mashaka makubwa na uwezo wa watendaji wetu. Pia elimu yetu.