KENZY
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 26,213
- 56,849
Si ulishasikia ile kauli ya jino kwa jino..? Sasa nikajaribu kuifata! Kumbe sikujua mwenzangu anameno mimi namapengo!
Aliponiblock nami si tu ya kwamba nikamblock bali nilimubuloku!.. haikuisha hapo aliacha kunitafuta nami si tu nikaacha kumtafuta bali nilimfuta kabisa!.. mambo ya jino kwa jino hayo!
Nae wala hakuisha visanga akafanya kimbwanga nami nikafanya tena huku nikijipa moyo kwani yeye nani?
Sahivi nimeshajua yeye ni nani na Mimi ni nani!.. yeye ni nyonga mkalia ini wangu nami ni komamanga tu!! Hii jino kwa jino sahivi inanitesa! Kumbe nilisahau nilikuwa na mapengo 😭
Mkimuona mwambieni moyo wangu unamfikiria yeye!, yeye ndo kimwana cha jahazi kilichobeba ukopakopa wote unaonisibu!..
Waswahili si kila kitu mtu atakachokikoroga anatakiwa anywe mengine tunayaoga kabisa! Kama ni dimbwi Basi nilitumbukia dubwiii.. sahivi nahangaika na mapengo yangu! Kweli kiberenge ni kiberenge tu..😭
Aliponiblock nami si tu ya kwamba nikamblock bali nilimubuloku!.. haikuisha hapo aliacha kunitafuta nami si tu nikaacha kumtafuta bali nilimfuta kabisa!.. mambo ya jino kwa jino hayo!
Nae wala hakuisha visanga akafanya kimbwanga nami nikafanya tena huku nikijipa moyo kwani yeye nani?
Sahivi nimeshajua yeye ni nani na Mimi ni nani!.. yeye ni nyonga mkalia ini wangu nami ni komamanga tu!! Hii jino kwa jino sahivi inanitesa! Kumbe nilisahau nilikuwa na mapengo 😭
Mkimuona mwambieni moyo wangu unamfikiria yeye!, yeye ndo kimwana cha jahazi kilichobeba ukopakopa wote unaonisibu!..
Waswahili si kila kitu mtu atakachokikoroga anatakiwa anywe mengine tunayaoga kabisa! Kama ni dimbwi Basi nilitumbukia dubwiii.. sahivi nahangaika na mapengo yangu! Kweli kiberenge ni kiberenge tu..😭