Wasukuma na ulaji wa korodani za ng'ombe na kichuri

Sigara Kali

JF-Expert Member
May 28, 2017
3,623
8,428
Ukizunguka mitaa mbalimbali hapa jijini Mwanza hasa mida ya jioni kuanzia mjini kati, Igoma, Buswelu, National na mitaa mingine mingi basi utakutana na moshi mwingi unaofuka kwenye majiko watu wakiwa busy kuchoma mishikaki ya moyo, maini, korodani, maziwa na maviungo mengine ya ng'ombe.

Kanda ya ziwa hasa Mwanza hakuna kiungo cha ng'ombe kinachotupwa, labda pembe na kwato tu. Huku kuna kitu kinaitwa kichuri, ni mchanganyiko wa mavi ya ng'ombe na nyongo. Wenyeji wanakula nyama choma ugali mwekundu wanashushia na kichuri yaani mavi na nyongo.

Ukitaka mishikaki ya kila kitu basi huku inapatikana, korodani, maini, moyo, utumbo, maziwa na madude mengine.

Kuishi Mwanza raha sana.
 
Aiseeeeh,
Naona wahusika hawajafika.
Subiria dakika siyo nyingi sana watafika.
 
hii kitu naipenda sana kila weekend napitia pale vingunguti mambo yote uliyosema yanapatikana
 
Kichuri sio mavi ya Ng'ombe.

Ile ni zile nyasi ambazo mnyama kama mbuzi au Ng'ombe anakua amekula ziko kwenye utumbo mwembamba zikimeng'enywa kabla hazijahamia utumbo mpana kua mavi.

So ni sawa na ile wanaita work in progress, sio nyasi na sio mavi. So bado inakua ina virutubisho vyote vya yale majani, ndio inatolewa inamiksiwq na nyongo.

Makabila mengi wanakula hiyo kitu sio wa mwanza tu, na sio wasukuma wanakula hiyo, hiyo ni ya jamii ya wakurya wote wa mkoa wa mara.

Kichuli, ile ni kama appetiser, unaweza kula mbuzi nzima, achana na kichuri.
 
Kichuri sio mavi ya Ng'ombe.

Ile ni zile nyasi ambazo mnyama kama mbuzi au Ng'ombe anakua amekula ziko kwenye utumbo mwembamba zikimeng'enywa kabla hazijahamia utumbo mpana kua mavi.

So ni sawa na ile wanaita work in progress, sio nyasi na sio mavi. So bado inakua ina virutubisho vyote vya yale majani, ndio inatolewa inamiksiwq na nyongo.

Makabila mengi wanakula hiyo kitu sio wa mwanza tu, na sio wasukuma wanakula hiyo, hiyo ni ya jamii ya wakurya wote wa mkoa wa mara.

Kichuli, ile ni kama appetiser, unaweza kula mbuzi nzima, achana na kichuri.
Kama Kuna mtu hajakuelewa, niruhusu nimfuate nyuma na Nissan nyeupe mkuu....

Nimependa hapo unaweza jikuta unakula mbuzi mzima
 
Back
Top Bottom