Wastaafu wawe wanaandaliwa kisaikojia kabla ya kukabidhiwa mafao

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,587
215,179
Wastaafu wengi huumizwa na mafao ambayo yalilengwa kuwasaidia. Kuna mmoja alipata milioni 200, wapambe walimshauri awekeze kwenye uchimbaji mdogo wa dhahabu. Alikaa huko miezi 18. Amerudi nyumbani hana kitu bahati yake mke ni mhangaikaji ana mgahawa.

Wahanga wa matukio haya ni wengi sana. Unamkuta mfanyakazi alikua anapokea laki nne na nusu kwa mwezi ghafla anamiliki milioni 60 benki. Kuna ambao wana malengo. Alikopa huko nyuma na kununua kiwanja na kujenga nyumba ya nyuma ili aachane na kulipa kodi. Alipanga mafao ndiyo ajenge nyumba ya mbele.

Ninachoona mifuko ya jamii iajiri wataalamu wa saikolojia na pia washauri wa uwekezaji. Ile wiki msataafu anayokabidhiwia pesa zake aelewe kuwa ana pesa lakini pesa ni liquid asset na ikishamwagika haizoleki. Apewe pia mawazo katika uwekezaji sahihi kama atapenda.
 
Sure,kunamzee alioa kibinti kidangaji,binti akapura zilepesa kwa fujo,dakika za mwisho watoto wa mzee wakamchapa yule binti,mzee akasalimu amri akamuacha. kucheki bank kwenye milioni 80 mzee kabakiza milioni 12 tu.
Hao watoto wajinga nini mzee amehangaika moaka yote sasa uzeeni anataka kusasambua mbususu mbichi wanamletea za kuleta. Hawajui kuwa maisha raha yake mbususu
 
Tulijaribu kama mradi fulani ambao ulipata mfadhili CARE INTERNATIONAL wilayani Kasulu mwaka 2002 wakati watumishi wanapata retrechment,mradi huu ulikuwa na lengo la kuwajengea uwezo wastaafu kuzimiliki hela zao pindi wanapopata.

Wastafu hao walifanyiwa semina ya wiki zima na kulipwa posho kila siku na walikuwa wanapata chai na chakula cha mchana. Baada ya kupata mafao yao na kuwafatilia ili kufanya tathimini ikaonekana wote wamefanya madudu na mradi ukafa. Mfadhili hakutoa fedha tena. Yaani hawa wastaafu wakipata fedha zao huwa wanapata kichaa fulani cha gafla.
 
Tulijaribu kama mradi fulani ambao ulipata mfadhili CARE INTERNATIONAL wilayani Kasulu mwaka 2002 wakati watumishi wanapata retrechment,mradi huu ulikuwa na lengo la kuwajengea uwezo wastaafu kuzimiliki hela zao pindi wanapopata.

Wastafu hao walifanyiwa semina ya wiki zima na kulipwa posho kila siku na walikuwa wanapata chai na chakula cha mchana. Baada ya kupata mafao yao na kuwafatilia ili kufanya tathimini ikaonekana wote wamefanya madudu na mradi ukafa. Mfadhili hakutoa fedha tena. Yaani hawa wastaafu wakipata fedha zao huwa wanapata kichaa fulani cha gafla.
Maofisa wa benki pia wanatakiwa kuona hii fursa ya grey shilling. Wawe wanawaelewesha maana ya fix deposit account. Ikiwezekana mtu aache nusu ya mafao benki na ataendelea kupata faida.
 
Sasa wao waache roho mbaya mbona baba yao aliwahudumia miaka hiyo na kujinyima mambo mengi. Wao kumuhudumia akipata heart attack ndio wanaonanjambo kubwa. Mitoto nakwambia mijinga sana inajifikiria yenyewe tuu...so selfish
Mkuu yaani wazazi wawili wanaweza kulea vizuri kabisa watoto kumi lakin uzeeni kwao watoto wao hao kumi wanaweza kushindwa kuwalea wazazi wao hao wawili.
 
Uko sahihi kabisa, mi muhanga.
Mama kastaafu kapigwa mil 65 kajenga kanisa nyumbani
Waumini wote ye ndio anahudumia.
Kila anayekuja ana matatizo.
Mama ana huruma sana
Muumini badala ya kuleta sadaka ndo kwaanza anaomba nauli ya kurudi kwao.
Nilikua sijali na mambo yake ila siku aliponambia kisiri nimpe hela akawape nauli ndo nikaona sasa huu utani.
Nikavunja kanisa na
Siku niliwatimua na bange zangu hawatanisahau.
Hela zimeisha,waumini hawapo Mama anasalisha huko kanisani lutheran kama nilivyomshauri
Sasa hivi ndo matokeo,
mmoja mmoja anamfata anawaombea,wanafanikiwa na kwakweli wanamsaidia fasta kunapotokea chochote.
 
Wastaafu wengi huumizwa na mafao ambayo yalikengwa kuwasaidia. Kuna mmoja alipata milioni 200, wapambe walimshauri awekeze kwenye uchimbaji mdogo wa dhahabu. Alikaa huko miezi 18. Amerudi nyumbani hana kitu bahati yake mke ni mhangaikaji ana mgahawa.

Wahanga wa matukio haya ni wengi sana. Unamkuta mfanyakazi alikua anapokea laki nne na nusu kwa mwezi ghafla anamiliki milioni 60 benki. Kuna ambao wana malengo. Alikopa huko nyuma na kununua kiwanja na kujenga nyumba ya nyuma ili aachane na kulipa kodi. Alipanga mafao ndiyo ajenge nyumba ya mbele.

Ninachoona mifuko ya jamii iajiri wataalamu wa saikolojia na pia washauri wa uwekezaji. Ile wiki msataafu anayokabidhiwia pesa zake aelewe kuwa ana pesa lakini pesa ni liquid asset na ikishamwagika haizoleki. Apewe pia mawazo katika uwekezaji sahihi kama atapenda.
Tatizo wasitaafu walio wengi niwa bishi sana kisikiliza mtu yoyote, na pia hawajazoea pesa nyingi lazima zipotee kwanza ndo watafute zingine za biashara huo ndo mfumo wao.
 
Uko sahihi kabisa, mi muhanga.
Mama kastaafu kapigwa mil 65 kajenga kanisa nyumbani
Waumini wote ye ndio anahudumia.
Kila anayekuja ana matatizo.
Mama ana huruma sana
Muumini badala ya kuleta sadaka ndo kwaanza anaomba nauli ya kurudi kwao.
Nilikua sijali na mambo yake ila siku aliponambia kisiri nimpe hela akawape nauli ndo nikaona sasa huu utani.
Nikavunja kanisa na
Siku niliwatimua na bange zangu hawatanisahau.
Hela zimeisha,waumini hawapo Mama anasalisha huko kanisani lutheran kama nilivyomshauri
Sasa hivi ndo matokeo,
mmoja mmoja anamfata anawaombea,wanafanikiwa na kwakweli wanamsaidia fasta kunapotokea chochote.
Daaah!!!
Mzee ulimuacha sanaa!!
Experience inaonesha hakuna mstaafu aliyepewa mafweza akataka kuyamiliki mwenyewe alafu akatoka salama hakuna hata mmoja.

Hao inatakiwa kuwasaidia wasipokubari kwa hiari walazimishwe.

Ungeingilia kati mapema pengine asingepoteza kiasi hicho.

Nategemea Kumpangia mama kila kitu pindi atakapostaafu kwa sababu nikishindwa kufanya hivyo mm mwanae

Wapo mambulula huko nje they will do it instead of me.

Ingilia kati kumsaidia mzazi wako asife mapema.

Atakuchukia mwanzo lkn kadiri akili zinavyorudi ndo atakua anajua umuhimu wako.

Wastaafu
 
Tatizo wasitaafu walio wengi niwa bishi sana kisikiliza mtu yoyote, na pia hawajazoea pesa nyingi lazima zipotee kwanza ndo watafute zingine za biashara huo ndo mfumo wao.
Katika ubishi wao wanajiamini kweli wanakuambia wanaanza biashara. Wanaamini ndani ya muda mfupi watakua wamezalisha mara tatu ya ile hela ya mafao. Hapa unabishana na mtu ana miaka 60 na hajawahi kufanya biashara maishani mwake.
 
Daaah!!!
Mzee ulimuacha sanaa!!
Experience inaonesha hakuna mstaafu aliyepewa mafweza akataka kuyamiliki mwenyewe alafu akatoka salama hakuna hata mmoja.

Hao inatakiwa kuwasaidia wasipokubari kwa hiari walazimishwe.

Ungeingilia kati mapema pengine asingepoteza kiasi hicho.

Nategemea Kumpangia mama kila kitu pindi atakapostaafu kwa sababu nikishindwa kufanya hivyo mm mwanae

Wapo mambulula huko nje they will do it instead of me.

Ingilia kati kumsaidia mzazi wako asife mapema.

Atakuchukia mwanzo lkn kadiri akili zinavyorudi ndo atakua anajua umuhimu wako.

Wastaafu
Mzee wangu aliweza japo miaka ya Kati alichukua mkopo pssf walikuwa wanaita mikopo ya nyumba

Alifanikiwa kujenga na nyingine kununua pickup sasa hapo kwenye pickup ndipo alipigwa japo ni 6 mln,, pickup haikuwahi kutembea ikauzwa milioni 2 kama scrapper.

Alivyochukua pesa ya kustaafu rasmi tulimsaidia tuu kusimamia ujenzi wa nyumba za kupanga ,alijenga chumba sebule 20 na nyumba mpya ya kuishi japo hatujawahi jua alistaafu na sh.ngapi but kwa haraka haraka si chini ya mil.60
 
41 Reactions
Reply
Back
Top Bottom