Wastaafu ATCL bado hawajalipwa licha Waziri Mkuu kueleza umma vinginevyo

kisingi

JF-Expert Member
Apr 9, 2014
516
377
Muda usiopungua miaka kumi na hadi sasa wapo wastaafu wa Air Tanzania Company Limited wanadai mafao ya PPF sasa PSSSF hawajalipwa. Wastaafu wa ATCL wanadai haki yao kwa kuwa walikatwa kutoka katika mishahara lakini haikupelekwa PSSSF (PPF) hivyo kuwafanya waambulie mafao kidogo wakati wa kustaafu na pensheni ya kila mwezi kuwa ndogo sana.

Suala hili Rais Samia Suluhu Hassani analifahamu, bunge wanalifahamu, Katibu mkuu kiongozi marehemu Kijazi alikwisha agiza wizara Ujenzi na Uchukuzi kutekeleza malipo na apate mrejesho. Mahakama Kuu ilisha pitisha hukumu wazee hawa wastaafu wa ATCL walipwe lakini hadi leo hawajalipwa.

Waziri mkuu ana nadi serikali kutoa pesa kulipa wastaafu kauli ambayo wastaafu wanaiona kama ni siasa kwa kuwa PSSSF wanasema pesa inayolipwa na serikali ni kupunguza deni serikali ilikopa na sio ya wastaafu moja kwa moja hivyo hela hiyo hutumika kuendeshea taasisi au mfuko huo wa PSSSF.

Tunaomba Raisi Samia simamia suala hili ili wazee hawa walipwe maana hata huko wizara ya Fedha na wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kuna watendaji hawataki haya madai ya wastaafu wa ATCL yalipwe. Bila ya Raisi kuwa imara vizazi na vizazi vya wastaafu na jamaa zao watakosa upendo na imani kwa serikali kitu ambacho wewe ndio SULUHU.
 
hand to mouth economy. twasubiri abiria watoe nauli kisha mishahara/marupurupu ilipwe/yalipwe
 
Mambo ya ATCL yananichanganya. Juzi tu Msigwa ametuhabarisha kwamba serikali imelipa mabilioni kulipia ndege mpya. Wakati huohuo taarifa nyingine inasema deni la ATCL pasua kichwa, leo tena kuna wastaafu hawajalipwa mafao.

Tukiacha kazi kudai mafao seriakali inasema mpaka uzeeke kwanza ndo ulipwe mafao. Ukizeeka ukakosa mafao unapata msongo wa mawazo unakufa bila kupata hizo hela ulizoahidiwa.

Tukubaliane tu kwamba nchi ni tajiri ila tunaongozwa na fikra za kimaskini
 
Inasikitisha wastaafu hawa wanapungua zaidi ya kumi na wamefariki. Jana 6/09/2021 amefariki mstaafu mwingine Medhod Barabara
Hii inasikitisha sana kwa kuwa kama angekuwa amelipwa madai haya ya mafao yangemsaidia kupata matibabu stahiki. Sio yeye pekee na wengi wa hao waliofariki ugumu wa kupata tiba stahiki umepelekea vifo.
 
Ina maana hata yule aliyekuwa anajinadi kama mtetezi wa wanyonge naye alishindwa kulimaliza!
 
Ni lini itatokea wastaafu kuthaminiwa iwapo serikali haioni umuhimu wao.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom