MGOMBEA ubunge wa Jimbo la Bunda mkoani Mara kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Stephen Wasira amewaomba wapiga kura jimboni humo kutompigia kura mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa kwa madai kuwa hana uzoefu wa uongozi.
Wasira amesema, kama wakimpigia kura Dk. Slaa ni sawa na kumkabidhi dereva anayejifunza gari, usukani wa basi la abiria.
Badala yake Wasira ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, (Nec) amewataka wapiga kura hao kumpatia kura nyingi za ushindi mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete kwa kuwa ni dereva makini aliyehitimu mafunzo yote aliyeiendesha nchi kwa usalama katika miaka mitano iliyopita.
Akihutubia mkutano wa kampeni za CCM juzi kwa nyakati tofauti katika vijiji vya Bukama na
Nyabehu, Wasira alisema tofauti na Kikwete, Dk. Slaa hajawahi kushika nyadhifa zozote za kiutendaji ambazo zinaweza kutumika kushawishi watanzania wamchague kushika mamlaka makubwa ya kiutendaji.
Slaa huyu hajawahi kushika wadhifa wowote ule wa kiutendaji, hata uofisa utendaji wa kijiji ili tumwone anavyoamua mashauri mbalimbali yanayomfikia. Leo tumpe kura za urais?
Tumechanganyikiwa yaani tumpe learner gari la abiria! Akiwaangusha nani alaumiwe? Mnyimeni kura, alisema Wasira.
Wasira ambaye pia ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika alisema nafasi ya urais ipo ya juu zaidi katika muundo wa serikali na inahitaji mtu makini.
Alisema licha ya umakini wa mtu, pia anatakiwa atoke chama makini na awe amepimwa na kuonekana anafaa kwa kazi hiyo na kamwe siyo ya kutolewa kwa kila aiombaye kama majaribio.
Kuhusu hoja kwamba mgombea huyo wa Chadema ameshika nyadhifa kadhaa ikiwemo ya ubunge wa Karatu, Wasira alisema mbunge hakumaanishi kuwa unafaa kuwa rais kwani ubunge ni uwakilishi na wala siyo utendaji.
Ndugu wananchi ubunge siyo utendaji, ni uwakilishi tu. Unazidiwa na utendaji wa kijiji na kata ndio maana hawa wanaamua kesi mbalimbali tofauti na mbunge, na unaweza kukaa bungeni muda wote wewe ni kusinzia tu, alisema Wasira.
Akimwelezea Kikwete, Wasira alisema mgombea huyo amejaribiwa kupitia nyadhifa mbalimbali za kiutendaji ndani na nje ya chama ukiwamo uwaziri katika wizara za Maji, Nishati na Madini, Wizara ya Fedha na pia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Alisema, katika miaka mitano ya Rais Kikwete madarakani, ameiwezesha nchi kungara katika medani za kimataifa huku akihifadhi amani, utulivu na mshikamano ndani ya nchi.
Huyu ndiye rais anayefaa. Amejaribiwa kwa nyadhifa mbalimbali na zote alifanya vizuri. Hata tulipomkabidhi nchi mwaka 2005 ameiwezesha kubakia katika hali yake ya amani na utulivu. Tumpe kura zetu, alisema.
Wasira amesema, kama wakimpigia kura Dk. Slaa ni sawa na kumkabidhi dereva anayejifunza gari, usukani wa basi la abiria.
Badala yake Wasira ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, (Nec) amewataka wapiga kura hao kumpatia kura nyingi za ushindi mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete kwa kuwa ni dereva makini aliyehitimu mafunzo yote aliyeiendesha nchi kwa usalama katika miaka mitano iliyopita.
Akihutubia mkutano wa kampeni za CCM juzi kwa nyakati tofauti katika vijiji vya Bukama na
Nyabehu, Wasira alisema tofauti na Kikwete, Dk. Slaa hajawahi kushika nyadhifa zozote za kiutendaji ambazo zinaweza kutumika kushawishi watanzania wamchague kushika mamlaka makubwa ya kiutendaji.
Slaa huyu hajawahi kushika wadhifa wowote ule wa kiutendaji, hata uofisa utendaji wa kijiji ili tumwone anavyoamua mashauri mbalimbali yanayomfikia. Leo tumpe kura za urais?
Tumechanganyikiwa yaani tumpe learner gari la abiria! Akiwaangusha nani alaumiwe? Mnyimeni kura, alisema Wasira.
Wasira ambaye pia ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika alisema nafasi ya urais ipo ya juu zaidi katika muundo wa serikali na inahitaji mtu makini.
Alisema licha ya umakini wa mtu, pia anatakiwa atoke chama makini na awe amepimwa na kuonekana anafaa kwa kazi hiyo na kamwe siyo ya kutolewa kwa kila aiombaye kama majaribio.
Kuhusu hoja kwamba mgombea huyo wa Chadema ameshika nyadhifa kadhaa ikiwemo ya ubunge wa Karatu, Wasira alisema mbunge hakumaanishi kuwa unafaa kuwa rais kwani ubunge ni uwakilishi na wala siyo utendaji.
Ndugu wananchi ubunge siyo utendaji, ni uwakilishi tu. Unazidiwa na utendaji wa kijiji na kata ndio maana hawa wanaamua kesi mbalimbali tofauti na mbunge, na unaweza kukaa bungeni muda wote wewe ni kusinzia tu, alisema Wasira.
Akimwelezea Kikwete, Wasira alisema mgombea huyo amejaribiwa kupitia nyadhifa mbalimbali za kiutendaji ndani na nje ya chama ukiwamo uwaziri katika wizara za Maji, Nishati na Madini, Wizara ya Fedha na pia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Alisema, katika miaka mitano ya Rais Kikwete madarakani, ameiwezesha nchi kungara katika medani za kimataifa huku akihifadhi amani, utulivu na mshikamano ndani ya nchi.
Huyu ndiye rais anayefaa. Amejaribiwa kwa nyadhifa mbalimbali na zote alifanya vizuri. Hata tulipomkabidhi nchi mwaka 2005 ameiwezesha kubakia katika hali yake ya amani na utulivu. Tumpe kura zetu, alisema.