Nicholas
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 25,260
- 7,195
Huku mzee akikuna kichwa kwa style ya kushindwa pata majibu kirahisi katika suala gumu, kapanda jukwaani kujitetea kuwa waliojiunga na CDM si wanae ni wa kaka yake.
Mzee akionekana kuchoka hakuwa na majibu ya kujiamini. Naye kaingia ktk game kama ya Mkapa.
Tusubiri kama kweli si watoto wa kuzaa, atamjibu vipi kakake kama kaona watoto wa kakake si wake.
Chanzo: TBC Habari
Mzee akionekana kuchoka hakuwa na majibu ya kujiamini. Naye kaingia ktk game kama ya Mkapa.
Tusubiri kama kweli si watoto wa kuzaa, atamjibu vipi kakake kama kaona watoto wa kakake si wake.
Chanzo: TBC Habari
1st October 2012
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Stephen Wasira
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Stephen Wasira, amekana kuwa watoto walijiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) juzi si watoto wake wa kuzaa, bali ni watoto wa ndugu yake ambao wana haki ya kujiunga na chama chochote cha siasa.
Wasira amesema kwamba kutumia jina na cheo chake ni upotoshwaji mkubwa ambao umefanywa na Chadema kwa lengo la kupata umaarufu.
Wasira, alitoa kauli hiyo jana mjini Bunda katika mkutano wake na waandishi wa habari ambao aliutumia kumshambulia Katibu Mkuu wa Chedema, Dk Wilibrod Slaa, kwa kumtaka awe makini.
"Wale watoto ni wa George Wasira siyo wa Stephen Wasira, hivyo kusema ni watoto wa wWziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) na mwanasiasa mkongwe katika ukoo wetu walilenga kunisema mimi. Hawa si watoto wangu wa kuzaa, bali ni watoto wa kaka angu na ni watu wazima wana haki ya kuchagua wawe katika chama gani,"alisema na kuongeza:
"Mimi sina mtoto wa kuzaa anaitwa Lilian, lakini nawajua wale Lilian namjua na Esther ni watoto wa kaka angu anaitwa George Bukore Wasira na mama yayo Wanzita, sasa habari ilitangazwa inasema ni watoto wa Stephen Wasira hii si kweli."
Source: Nipashe