Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
@KYAMTUMBU, hayo uyasemayo ni kweli na nukuu yako ni sahihi, lakini tatizo linakuja kwenye kuipenda CHADEMA, kama kweli kingekuwa mbadala wa ccm, basi muda mrefu tu ningekuwa mkereketwa wake. Tatizo lilipo ni kwamba Chadema wameonyesha mapungufu mengi wakiwa nje ya dola, sasa tukiwapa dola itakuwaje?
Wassira amemwambia Sitta "kama unaona serikali inaendeshwa kwa rushwa jiuzuru", akaendelea kusisitiza, "huwezi kuwa kwenye serikali hiyo hiyo bado unaisema ni serikali ya kifisadi wakati na wewe ni sehemu ya serikali."
Wassira pia aliongeza yafuatayo, "huwezi kuisema serikali vibaya wakati na wewe ni sehemu ya serikali hiyo, vinginevyo ndugu Sitta aachie ngazi la sivyo huu utakuwa utapeli wa kisiasa".
Aidha, katika kuimalizia hoja yake hii aliuliza swali, "samaki mmoja akioza, wote wanaoza, sasa yeye (akimaanisha Sitta) atasalimika vipi?"
My take;
Mhe. Sitta nadhani ana hitaji kukopeshwa busara kidogo, katika hatua hii huwezi kujifanya una chukizwa na madudu ya serikali ambayo kwa kipindi chote hiki amekuwa akiitumikia, amekuwa sehemu ya serikali hiyo na kama akisema kuna madudu, na yeye tuseme ni miongoni mwa wazalisha madudu hayo.
Mhe. Sitta, kiu ya urais isikufanye uonekane kituko mbele ya watanzania, kuwa mpole na usubiri wakati muafaka, kwani tabia hizi za kuropoka ropoka ndani ya CCM hatunazo, tuwaachie hii tabia wasaka dola bila mbinu (CHADEMA).
Wassira amemwambia Sitta "kama unaona serikali inaendeshwa kwa rushwa jiuzuru", akaendelea kusisitiza, "huwezi kuwa kwenye serikali hiyo hiyo bado unaisema ni serikali ya kifisadi wakati na wewe ni sehemu ya serikali."
Wassira pia aliongeza yafuatayo, "huwezi kuisema serikali vibaya wakati na wewe ni sehemu ya serikali hiyo, vinginevyo ndugu Sitta aachie ngazi la sivyo huu utakuwa utapeli wa kisiasa".
Aidha, katika kuimalizia hoja yake hii aliuliza swali, "samaki mmoja akioza, wote wanaoza, sasa yeye (akimaanisha Sitta) atasalimika vipi?"
My take;
Mhe. Sitta nadhani ana hitaji kukopeshwa busara kidogo, katika hatua hii huwezi kujifanya una chukizwa na madudu ya serikali ambayo kwa kipindi chote hiki amekuwa akiitumikia, amekuwa sehemu ya serikali hiyo na kama akisema kuna madudu, na yeye tuseme ni miongoni mwa wazalisha madudu hayo.
Mhe. Sitta, kiu ya urais isikufanye uonekane kituko mbele ya watanzania, kuwa mpole na usubiri wakati muafaka, kwani tabia hizi za kuropoka ropoka ndani ya CCM hatunazo, tuwaachie hii tabia wasaka dola bila mbinu (CHADEMA).
6 mnafiki.
mkuu mzee 6, mnafiki sana!
tuwaachie hii tabia wasaka dola bila mbinu (CHADEMA).
Wassira amemwambia Sitta "kama unaona serikali inaendeshwa kwa rushwa jiuzuru", akaendelea kusisitiza, "huwezi kuwa kwenye serikali hiyo hiyo bado unaisema ni serikali ya kifisadi wakati na wewe ni sehemu ya serikali."
Wassira pia aliongeza yafuatayo, "huwezi kuisema serikali vibaya wakati na wewe ni sehemu ya serikali hiyo, vinginevyo ndugu Sitta aachie ngazi la sivyo huu utakuwa utapeli wa kisiasa".
Aidha, katika kuimalizia hoja yake hii aliuliza swali, "samaki mmoja akioza, wote wanaoza, sasa yeye (akimaanisha Sitta) atasalimika vipi?"
My take;
Mhe. Sitta nadhani ana hitaji kukopeshwa busara kidogo, katika hatua hii huwezi kujifanya una chukizwa na madudu ya serikali ambayo kwa kipindi chote hiki amekuwa akiitumikia, amekuwa sehemu ya serikali hiyo na kama akisema kuna madudu, na yeye tuseme ni miongoni mwa wazalisha madudu hayo.
Mhe. Sitta, kiu ya urais isikufanye uonekane kituko mbele ya watanzania, kuwa mpole na usubiri wakati muafaka, kwani tabia hizi za kuropoka ropoka ndani ya CCM hatunazo, tuwaachie hii tabia wasaka dola bila mbinu (CHADEMA).
Huyu Six ni mnafiki sana na anafikiri watu tumesahau ushenzi wake alipokuwa Spika?
Wabunge wanapolilia mkia wa kondoo
Joseph Mihangwa
Toleo la 049
1 Oct 2008
Hoja yao ilizimwa na kelele za wananchi kupitia vyombo vya habari. Hiyo ikimfanya Rais Jakaya Kikwete aliambie Taifa kuwa Wabunge bila shaka ni watu wazima, lazima wamesikia.
Lakini Spika Samuel Sitta, alifunga hoja hiyo kwa kuwapa matumaini Wabunge hao akisema, kwa vyovyote vile, maslahi ya wabunge yataendelea kushughulikiwa na taasisi zinazohusika serikalini, kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa, akaongeza kwamba, hizo ndizo siasa na gharama za kuwa mwanasiasa,
Wakati wabunge hawa wanadai mkia wa kondoo, zaidi ya Watanzania milioni 18 wanaishi kwa kipato duni chini ya 400/= kwa siku; watano kati ya sita hawana hakika ya mlo wa siku, na mmoja kati ya watatu hapati mahitaji muhimu ya maisha. (Mr Six hana huruma na watanzania kama anavyojipambanua)
..Bunge limevamiwa na wafanyabiashara walioingia si kwa lengo la kutumikia, bali kuendeleza na kulinda biashara zao kwa nguvu za kisiasa? Hawa wanataka mishahara mikubwa na marupurupu manono kufidia muda na biashara zao walizoziacha?
Bunge limevamiwa na wasomi na wanataaluma walioziacha taaluma zao kukimbilia mkia wa kondoo? Wanadai vinono kufidia posho nono, pensheni na ten per cent zilizoua mashirika na taasisi za umma walikotokea kwa kuipa jina baya Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Ni utamaduni huu ulizaa kashfa za EPA, Richmond / Dowans na nyingine. Makundi yote mawili yameingia bungeni bila wito bali kwa lengo la kujinufaisha na kutumikiwa?
Wabunge wetu wangeonyesha busara na kuweza kuheshimiwa, kwa kupeleka muswada bungeni kuongeza mishahara ya wafanyakazi, au kwa lengo la kuwapunguzia wakulima ukali wa maisha, kuonyesha kwamba wanawajali wapiga kura wao.
Tuangalie toka Mwanahalisi
Nyuma ya pazia la posho za wabunge(Mr Six alikomalia mpaka wakajiongeza posho wakati watanzania wakifa na njaa)
Na Joster Mwangulumbi - Imechapwa 22 June 2011
Nyuma ya pazia
Hata hivyo, kuna sababu zilizofichika ambazo Waziri mkuu hawezi kuweka wazi. Uamuzi wa kuwapa posho wabunge, wanajeshi na hata polisi ni mpango wa nchi nyingi duniani hasa za Afrika kupunguza uwezekano wa serikali zilizoko madarakani kukataliwa na kuondolewa.
Katika nchi ambazo demokrasia bado ni changa kama Tanzania, wabunge wote wa chama tawala, kazi kubwa bungeni ni kuunga mkono hoja na kudhoofisha hoja za upinzani. Wao hujiweka nafasi ya mawaziri kuzima hoja za wapinzani.
Wanadhani kuwa wakikosoa kwa uhuru wao watakuwa wamesaidia serikali kuondolewa madarakani; wanahofu wasipounga mkono wanaweza kukosa nafasi za uteuzi. Hivyo wanaipa tuzo serikali kwa kuipigia makofi kwa kila jambo ili nayo ilipe fadhila kwa kuwapa wabunge posho kwa kazi ambayo wanalipwa mshahara.
Ujinga wote huu ulibarikiwa na Mr Six
Wassira amemwambia Sitta
"kama unaona serikali inaendeshwa kwa rushwa jiuzuru", akaendelea
kusisitiza, "huwezi kuwa kwenye serikali hiyo hiyo bado unaisema ni
serikali ya kifisadi wakati na wewe ni sehemu ya serikali."
Wassira pia aliongeza yafuatayo, "huwezi kuisema serikali vibaya wakati
na wewe ni sehemu ya serikali hiyo, vinginevyo ndugu Sitta aachie ngazi
la sivyo huu utakuwa utapeli wa kisiasa".
Aidha, katika kuimalizia hoja yake hii aliuliza swali, "samaki mmoja
akioza, wote wanaoza, sasa yeye (akimaanisha Sitta) atasalimika vipi?"
My take;
Mhe. Sitta nadhani ana hitaji kukopeshwa busara kidogo, katika hatua hii
huwezi kujifanya una chukizwa na madudu ya serikali ambayo kwa kipindi
chote hiki amekuwa akiitumikia, amekuwa sehemu ya serikali hiyo na kama
akisema kuna madudu, na yeye tuseme ni miongoni mwa wazalisha madudu
hayo.
Mhe. Sitta, kiu ya urais isikufanye uonekane kituko mbele ya watanzania,
kuwa mpole na usubiri wakati muafaka, kwani tabia hizi za kuropoka
ropoka ndani ya CCM hatunazo, tuwaachie hii tabia wasaka dola bila mbinu
(CHADEMA).