Wasomi wetu na mustakabli wa taifa

TANMO

JF-Expert Member
Apr 12, 2008
11,513
11,276
Wanajamii kuna habari nimeisoma kuhusu msimamo wa vyuo vikuu dhidi ya waraka waziri Maghembe kuwataka watumie vyeo vya mwenyekiti badala ya rais wa serikali ya wanafunzi na pia juu ya kufutwa kwa serikali za wanafunzi n.k

Kauli yao waliyoitoa juu ya waraka huo ni ya kumtaka waziri aachane na mambo hayo vinginevyo watapambana naye na hata ikibidi wataendesha kampeni dhidi yake kwenye jimbo lake la uchaguzi.

Hoja yangu siyo kujadili upande upi uko sahihi bali kutokana na msimamo wa wasomi hawa nimeshawishika kuamini kuwa tatizo la uongozi mbovu nchi yetu mara nyingine linasababishwa na ubinafsi tulionao watanzania hasa wasomi. Ni mara nyingi sana viongozi wetu wanatoa kauli au kufanya maamuzi ambayo hayana tija kwa jamii lakini sijawahi kusikia kauli ya hawa viongozi wa vyuo. Mpaka maslahi yao yanapoguswa ndiyo wanaibuka na kutaka kuishirikisha jamii.

Nadhani ni wakati sasa kwa wasomi wetu nao angalau kutoa misimamo yao pale wanapoona mambo yanafanyika ndivyo sivyo serikalini. Hii itasaidia angalau kuamsha mori ya wazalendo wengine kwa manufaa ya jamii ya watanzania wote.

Nawasilisha.
 
Wanajamii kuna habari nimeisoma kuhusu msimamo wa vyuo vikuu dhidi ya waraka waziri Maghembe kuwataka watumie vyeo vya mwenyekiti badala ya rais wa serikali ya wanafunzi na pia juu ya kufutwa kwa serikali za wanafunzi n.k

Kauli yao waliyoitoa juu ya waraka huo ni ya kumtaka waziri aachane na mambo hayo vinginevyo watapambana naye na hata ikibidi wataendesha kampeni dhidi yake kwenye jimbo lake la uchaguzi.

Hoja yangu siyo kujadili upande upi uko sahihi bali kutokana na msimamo wa wasomi hawa nimeshawishika kuamini kuwa tatizo la uongozi mbovu nchi yetu mara nyingine linasababishwa na ubinafsi tulionao watanzania hasa wasomi. Ni mara nyingi sana viongozi wetu wanatoa kauli au kufanya maamuzi ambayo hayana tija kwa jamii lakini sijawahi kusikia kauli ya hawa viongozi wa vyuo. Mpaka maslahi yao yanapoguswa ndiyo wanaibuka na kutaka kuishirikisha jamii.

Nadhani ni wakati sasa kwa wasomi wetu nao angalau kutoa misimamo yao pale wanapoona mambo yanafanyika ndivyo sivyo serikalini. Hii itasaidia angalau kuamsha mori ya wazalendo wengine kwa manufaa ya jamii ya watanzania wote.

Nawasilisha.

Ndugu, Wasomi sio kwamba hawoni madudu ya sirikali yao i think UTAKUWA UNAKUMBUKA KAMA ULIKUWEPO KIPINDI CHA NYERERE WAKATI WASOMI WALIPOKUWA WANAANDAMANA HADI IKULU KAMA HAWAPENDEZEWI JAMBO, NYERERE ALILIONA HILI NDO SIRIKALI WAKAWEKA MSIMAMO KWAMBA SIASA VYUO VIKUU HAKUNA, JIULIZE KWANINI WAGOMBEA WA UBUNGE NA URAIS HAWENDI VYUONI KUPIGA KAMPANI?? KWANINI ZITTO ALIZUIWA WAKATI ANAENDA UDSM KUUTUBIA???
 
Wanajamii kuna habari nimeisoma kuhusu msimamo wa vyuo vikuu dhidi ya waraka waziri Maghembe kuwataka watumie vyeo vya mwenyekiti badala ya rais wa serikali ya wanafunzi na pia juu ya kufutwa kwa serikali za wanafunzi n.k

Kauli yao waliyoitoa juu ya waraka huo ni ya kumtaka waziri aachane na mambo hayo vinginevyo watapambana naye na hata ikibidi wataendesha kampeni dhidi yake kwenye jimbo lake la uchaguzi.

Hoja yangu siyo kujadili upande upi uko sahihi bali kutokana na msimamo wa wasomi hawa nimeshawishika kuamini kuwa tatizo la uongozi mbovu nchi yetu mara nyingine linasababishwa na ubinafsi tulionao watanzania hasa wasomi. Ni mara nyingi sana viongozi wetu wanatoa kauli au kufanya maamuzi ambayo hayana tija kwa jamii lakini sijawahi kusikia kauli ya hawa viongozi wa vyuo. Mpaka maslahi yao yanapoguswa ndiyo wanaibuka na kutaka kuishirikisha jamii.

Nadhani ni wakati sasa kwa wasomi wetu nao angalau kutoa misimamo yao pale wanapoona mambo yanafanyika ndivyo sivyo serikalini. Hii itasaidia angalau kuamsha mori ya wazalendo wengine kwa manufaa ya jamii ya watanzania wote.

Nawasilisha.

Unaposema wasomi wetu, nashindwa kuelewa. hivi ina maana Tanzania nayo ina wasomi, Tanzania ina wakariri maandishi na wala haina wasomi kwa taarifa yako.ingekuwa na wasomi basi ingekuwa ina soko kubwa la kuuza mali ghafi zake na fito vyake vya thamani fikiri ni nchi ya tatu duniani kwa kuzalisha dhahabu lakini hatuna soko la kuuza dhahabu, ni mpaka South africa watusaidie kuuza. Sasa hivi hata mbao zetu ni mpaka kenya watusaidie kuuza.Shangaa tangu tulipoanza kuzalisha ges yetu ya songa mpaka leo ni mika kumi inaenda sasa lakini bado tunaagiza ges nje wakati ya kwetu ni nyingi ambayo hatutakaa tuimalize kwa hata miaka 1000. Sasa hapa kuna wasomi au kuna matope? pls usinitie hasira
 
nijuacho mimi wasomi wetu wengi ni wazuri na wanaweza kuleta mabadiliko makubwa tu, lakini system iliyopo haitaki mtu yoyote aliye above average na iko tayari kukumbatia wataalama mediocre ilimradi hawahoji, hawafikirii na watadumisha status quo

ukiona kuna wasomi wako serikalini, ujue kabisa hao ni wale wa "ndio mzee" na wamesha-trade usomi wao kupata vyeo vya kisiasa, yaani ni kama wamedenouce usomi wao

THINK ABOUT IT!
 
definition ya usomi Tanzania
inafurahisha sana........
sisi tumekuwa kama kisiwa hivi,tuna mambo yetu
ni made in Tanzania only...........
 
Unaposema wasomi wetu, nashindwa kuelewa. hivi ina maana Tanzania nayo ina wasomi, Tanzania ina wakariri maandishi na wala haina wasomi kwa taarifa yako.ingekuwa na wasomi basi ingekuwa ina soko kubwa la kuuza mali ghafi zake na fito vyake vya thamani fikiri ni nchi ya tatu duniani kwa kuzalisha dhahabu lakini hatuna soko la kuuza dhahabu, ni mpaka South africa watusaidie kuuza. Sasa hivi hata mbao zetu ni mpaka kenya watusaidie kuuza.Shangaa tangu tulipoanza kuzalisha ges yetu ya songa mpaka leo ni mika kumi inaenda sasa lakini bado tunaagiza ges nje wakati ya kwetu ni nyingi ambayo hatutakaa tuimalize kwa hata miaka 1000. Sasa hapa kuna wasomi au kuna matope? pls usinitie hasira

Wewe uko kundi gani? la wasio wasomi?
 
Kuna mwenye CV ya Prof Maghembe?................nasema hivi kwa sababu nilihudhuria conference moja ughaibuni.............wakati huo akiwa Waziri wa Utalii..............nilibaki nikijiuliza maswali meeengi sana....................
 
Wana JF nimekuwa nikijiuliza kila kukicha Tanzania wanaongelewa wasomi kila kukicha , nafasi zote za uongozi zimekuwa za wasomi , hebu tujiulize huu utitili wa wasomi tulio nao umeisaidia nini Tanzania? mbona nchi inaelekea kubaya tofauti na kipindi ambacho hatukuwa na wasomi wengi, tunawasomi hata kutengeneza SINDANO hawawezi kila kitu tunaagiza kutoka nje ya nchi, kazi yao kujidai wasomi na degree za kununua au elimu za kwenye MAKARATASI ndo maana wanakuwa na uelewa mdogo?leo hii kila msomi anataka awe kiongozi serikalini wanalenga kuiba tu hakuna cha maana, tungewatambua usomi wao kama wangeleta mabadiliko mfano kwenye elimu, afya , uchumi , wasomi wetu wamebaki kupiga kelele za kuongezewa posho ndo maana tunazalisha division 5, ni mda umefika tuwahoji wasomi wetu hizo PHD zao wameifanyia nini tanzania, kuna watu wanaelimu ya kawaida sana form iv hadi vi lakini wanauelewa kuliko mtu mwenye PHD, hivyo tukiendekeza maswala ua usomi nchi yetu itapoea, tua Ndo tumpe uongoziangalie uelewa wa mtu na ameifanyia nini nchi yetu.
 
Back
Top Bottom