Wasomi washauri Rais Kikwete kuwafukuza kazi washauri wake

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Date::8/20/2008
Wasomi washauri Rais Kikwete kuwafukuza kazi washauri wake
Peter Edson na Happiness Matanji
Mwananchi

WASOMI na wanasiasa nchini wamemtaka Rais Jakaya Kikwete kuwafukuza kazi washauri wake wa masuala ya siasa, uchumi na Kijamii ili kulinusuru Taifa.

Ushauri huo umetolewa siku moja baada ya utafiti wa hali ya kisiasa nchini uliofanywa na Mpango wa Utafiti na Elimu ya Demokrasia Tanzania (Redet) kuonyesha kuwa Rais Kikwete ameshuka kiutendaji.

Wakizungumza na gazeti hili jana wasomi hao walisema baadhi ya washauri wa rais hawana dhamira kumsaidia na kumshauri vizuri ili kumrahisishia utendaji wake.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, alisema washauri wa rais hawana nia ya kumsaidia kupambana na umaskini unaoliandama taifa badala yake wamekuwa wakishauri mambo yanayowanufaisha watu wachache.

"Hakuna kinachofanyika hadi sasa, badala yake maisha yanaendelea kuwa magumu kwa wananchi. Washauri wa Rais wanaendelea kuwa kimya jambo linaloonyesha dhahiri kuwa hawamshauri vizuri," alisema Kabwe.

Zitto aliikosoa ripoti hiyo ya Redet akisema kuwa si kweli kwamba rais Benjamin Mkapa alikuwa na matukio machache ya watu kudai uwajibikaji, bali hali hiyo ilijitokeza kutokana na uongozi wake kuwa wa kidikteta na mabavu.

Alisema Mkapa alitumia dola kuzima mambo mengi maovu ambayo wananchi walitaka kuyadai kama haki zao za msingi.

Kauli ya Kabwe iliungwa mkono na Mwenyekiti wa PPT Maendeleo, Peter Mzirai, aliyesema kuwa umefika wakati kwa Rais Kikwete kuwa na utawala wa mseto ili kupunguza migogoro ya kisiasa, kijamii na kiuchumi inayoendelea kutikisa nchi.

Alisema tatizo la Rais Kikwete ni kutokuwa na mikakati endelevu yenye nia ya kuonyesha mwanga wa mafanikio kwa wananchi wenye kipato cha chini na washauri wake wamechangia kupoteza dira na malengo ya maendeleo yaliyowekwa na Serikali.

"Suala la Serikali ya mseto linahitaji kuzingatiwa kwani ndiyo suluhisho la matatizo ya kisiasa Afrika," alisema Mzirai

Alisema Serikali ya Rais Kikwete imekuwa ikiyumba kutokana na kukosa timu imara ya kumshauri kuhusu mazingira utendaji wake.

Alisema kuna haja kwa Rais Kikwete na serikali yake kukumbuka sera za Azimio la Arusha kwani ndiyo msingi unaoweza kubadilisha uelekeo mbaya wa upepo unaoendelea kuleta hali ngumu ya maisha kwa watanzania.

Naye Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam, Idara ya Siasa na Utawala, Dk Mohammed Bakari, alisema Rais Kikwete ni muoga katika kutoa maamuzi magumu kwa hofu ya kuchochea machafuko jambo ambalo limeendelea kuhalalisha kuwa anawalinda mafisadi.

Alisema Mkapa aliweza kusimamia mambo magumu na kuyatolea maamuzi kwa sehemu, lakini Rais Kikwete amekuwa akishindwa kutoa maamuzi yenye lengo la kuonyesha muelekeo wa maendeleo na kutatua kero zinazowakabili wananchi.

"Kama Rais Kikwete atataja orodha ya mafisadi atakuwa amerudisha imani kwa wananchi kwa asilimia 60 kwani wananchi wengi wanahitaji kumuona akitoa maamuzi magumu kwa masilahi ya taifa," alisema Dk Bakari.

Alisema pamoja na kupoteza umaarufu kwa wananchi, Rais Kikwete anatakiwa kutambua kuwa kuendelea kukaa kimya bila kutoa maamuzi kuhusu ufisadi unaoendelea nchini ni kuwanyima haki ya msingi wananchi ambao walimwamini na kumpa kura.

Naye Bashiru Ally ambaye ni mhadhiri katika chuo kikuu cha Dar es salaam (siasa) alisema kuna kila sababu kwa rais Kikwete kuhakikisha kuwa anatatua mambo makubwa ambayo ni chanzo cha migogoro.

Alitaja matatizo hayo kuwa ni yale yanayodhalilisha utu wa mtanzania na kuwafanya watu wachache waendelee kuwa bora katika jamii.

"Ipo haja kwa Rais kutangaza majina ya mafisadi kwa uwazi ili wananchi warudishe imani kwake kwani sasa amepoteza muelekeo," alisema Ally.
 
Jamani mnamlaumu dobi bure kaniki ndiyo rangi yake hiyo hata ikifuliwa masaa 24!!!! JK anaweza kufukuza watendaji wake kila mwezi, kama yeye mwenyewe hana utashi wa kufanya yale ambayo Watanzania tunataka ayafanye basi hata akiwa na watendaji malaika hakuna chochote kitakachofanyika, labda ajifukuze kazi yeye na serikali yake yote ndiyo tutaona maslahi ya nchi yetu yanawekwa mbele.
 
Nadhani hapa tatizo si washauri. Mtu unaweza kuignore ushauri na ukafanya kitu kikaonekana. JK hajafanya chochote ambacho kimeonekana kuwa huu hapa ni msimamo wa rais wetu. Siyo kila kitu kitegemee washauri. Rais lazima aonyeshe dira yake, washauri kazi yao ni kumpa pros and cons za hiyo dira, period. Je Kikwete ameonyesha dira?
 
Date::8/20/2008
Wasomi washauri Rais Kikwete kuwafukuza kazi washauri wake
Peter Edson na Happiness Matanji
Mwananchi

WASOMI na wanasiasa nchini wamemtaka Rais Jakaya Kikwete kuwafukuza kazi washauri wake wa masuala ya siasa, uchumi na Kijamii ili kulinusuru taifa.

Hao ni baadhi ya wasomi, sio wote, maana hata mimi kwa elimu niliyonayo ni msomi,Lakini siwezi kutoa wala kuzungumza utumbo kama huu wa REDET na hao wengine.

Kwanza hatujaelezwa ni wapi na lini washauri wa Rais wameshindwa kumshauri rais, research haijaelezwa with evident kuwa washauri fulani kuwa wameshindwa ushauri, naamini HII NI NAMNA NYINGINE YA KUMUINUA KIKWETE HUKU TUKIPUMBAZWA.

REDET this is fool, and we never expected wasomi kama nyie ambao mlishafanya makosa ya kumuweka kikwete mzungumze tena utumbo kama huu.

Kikwete ameshindwa kazi hii iko wazi , lolote atakalofanya kipindi hiki ni kugain popularity ni kuwapumbaza wananchi wengi.

Redet walimtwisha mzigo Kikwete, Redet hawakufanya wala kuact kama wasomi waliofunguka macho, walifanyika kundi moja na waandishi wa habari kumuinua kikwete.

Najua kuwa REDET ni wasomi mmoja wao akiwa Mkandala,msomi wa Marekani, USOMI NI NINI BASI kama akili za Mkandala ziko sawa na Rweyemamu nani msomi?

Wasomi ni taa ni foreseer, wasomi ni macho na darubini ya kuona mbali, jamii ya watanzania wengi hawajasoma , kazi ya wasomi ni kuwaamsha waliolala.LAZIMA WAJUE NA WASEME QUALITY YA RAIS INATAKIWA IWE VIPI, NINI AMBACHO KIKWETE ALIFANYA SIKU ZA NYUMA AMBACHO KILIPELEKEA WASEME ANAFAA KUWA RAIS, KAMA WALIFANYA UTAFITI NA WAKAGUNDUA ATASHINDA WHAT WAS THEIR RECOMMENDATIONS NA CONCLUSIONS.Tusidanganyane research lazima iwe na Conclusion na recommendation, kusema kuwa awafukuze washauri wake huku rezerach haionyeshi ni wapi wameshindwa kazi ni upuuzi na matusi yasiyovumilika, mnasahili kutukanwa matusi makubwa yote muyajuayo.

NATAMANI moja ya Recommendation au conclusion mwaka 2005 ingesomeka hivi ''Kutokana na utafiti tulioufanya tunaona Kikwete anaelekea kushinda uchaguzi ujao, lakini pamoja na wananchi wengi kuamini na kuona hivi, bado tunashawishika kusema kuwa Kikwete hatafaa kuingoza Tanzania, based on his previous performances'' Kama REDET wanatoa tu matokeo ya tafiti wanatofauti gani na BBC, majira, n.k ambao waliendesha tafiti zao na kuonyesha Kikwete atashinda?? they have to show difference.

Lazima ifike wakati wasomi wawe wasomi,kwa sasa naona wapumbavu au wajinga fulani wanaojiita maprofesa, huku hatuoni faida yao TANZANIA labda mtu anisaidie kuwa profesa nani Tanzania ambaye tunatumia utafiti wake? hamna?? ndio hao mwandishi wa habari anasema wasomi.wasomi hawa wanadharaulika '' kuwa wasomi wa kiafrika hawana mchango wowote kwa maendeleo ya binadamu duniani'' sitaki kuamini hivi , lakini haya si tunaona!!

WASOMI WENGI WAMESOMA abroad niliamini kuwa WANAJUA QUALITY YA RAIS, NA VIGEZO , mostly IS BASED ON WHAT THEY DID PREVIOUS, KWELI WASOMI WETU HAWA HAWAJUI HILI?? Hii haihitaji kusoma ulaya wala PhD. ili ujue ili.

Eti wanasema atangaze majina ya mafisadi! akishatangaza basi!, wanataka kikwete awe mdaku! siyo mchukua hatua.Kuna lipi kafanya Kikwete asilaumiwe? aliyesema inatakiwa serikali ya mseto two thumbs up! wengine wameongea uozo ambao mpaka wake zenu wanawashangaa!!, Zito kaka be careful usiiingie kwenye lugha za kipropaganda, eti awafukuze kazi washauri, wewe mwenyewe ni mshauri wa Kikwete!

Maoni mengi ya hao wasomi bado yanaonyesha '' grace period kwa Kikwete'' kuwa bado anaweza kazi, miezi, miaka, siku vinaenda huku hali za watanzania zikiwa duni leo afadhali ya jana!

Unajua kuwa profesa ni rahisi sana bongo, swala ni utafanya nini na usomi wako.maoni mengi waliyotoa ni ya kiuoga, kikwete anafaa aachie ngazi, wasomi wasiposema hivi nani aseme?? wamekalia matumbo yao,magari na maisha mazuri they dont have problem.

Nimeona mbwa wengi ulaya wanakula, wanakunywa. wanapelekwa hospitali,wanapanda na kusafiri kwenye magari mazuri sana ya kufahari, lakini hawa ni mbwa, they are remotely uncomparable far away from human value! hawana na hawataweza kuwa na thamani ya sawa na mwanadamu.
Inapotokea msomi, mwanasiasa anawaza kula, kulala, kusafiri na kuvaa vizuri, na kutoa statement kama hizo,then thats is final of his thought, hana tofauti na mbwa, tena mbwa huyu mbaya kwa maana anaweza kuongea na kurubuni watu.na mwandishi wa habari akaripoti kama hivi! eti '' wasomi washauri kikwete kuwafukuza kazi washauri wake.

washauri wa Rais ni wananchi , tumemweleza tunataka achukue hatua kuhusu EPA, RICHMOND, IPTL, rada, ndege yake, Kiwira, maliasili, madini n.k hataki mnataka ''washauri wake'' waseme nini tena?? au sisi unshauri wetu haukubaliki? kwa sababu siyo special?


Habari ndiyo hiyo!!!

waberoya
I have come to the conclusion that politics are too serious a matter to be left to the politicians''. Charles De Gaulle (1890 - 1970)
 
Last edited:
Baada ya kuisoma taarifa hii napata picha ya haraka kwamba mwandishi anajaribu kutuambia kwamba Kikwete ni safi na ni mchapa kazi mzuri, ila washauri wake ndio wanamwangusha. Hali halisi kwa jinsi tunavyoifahamu iko kinyume kabisa na jinsi ndugu mwandishi anavyojaribu kumpamba Mheshimiwa Rais.

Kikwete ni Amiri Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, lakini hatekelezi majukumu yake kama amiri jeshi mkuu. Tatizo lake kubwa ni ameshindwa kutumia executive power aliyonayo kwani yeye kama Chief Executive wa United Republic of Tanzania anatakiwa kutekeleza majukumu tuliyompatia mwaka 2005 kwa kura zetu ki-executive, na si vinginevyo. Mambo ya kuunda kamati kila siku, hata kwenye issues zisizohitaji kuundiwa kamati, yanaonyesha jinsi anavyoshindwa ku-make executive decisions by himself.

Kikwete anahitajika kubadilika ili kulinusuru taifa letu. Tusijaribu kumpamba na kusema kwamba washauri wake ndio wana matatizo... Ni yeye mwenyewe ndiye mwenye matatizo.
 
washauri wa Rais ni wananchi , tumemweleza tunataka achukue hatua kuhusu EPA, RICHMOND, IPTL, rada, ndege yake, Kiwira, maliasili, madini n.k hataki mnataka ''washauri wake'' waseme nini tena?? au sisi unshauri wetu haukubaliki? kwa sababu siyo special?


Habari ndiyo hiyo!!!

waberoya
I have come to the conclusion that politics are too serious a matter to be left to the politicians’’. Charles De Gaulle (1890 - 1970)


It doesn't work that way.

Wanasiasa hawatasikiliza ya wananchi wala mama yake mwananchi, hali kadhalika ya wasomi. Watatekeleza na kufanya mambo kwa maslahi yao tu isipokuwa kama kuna pressure ya kutosha kutoka kwa wadanganyika; kulalama na kupiga mayowe ndani ya daladala si mojawapo ya "pressure" ninazoongelea.

Btw, haya ameyasema Prof. Issa Shivji wa UDSM majuzi (not exact words).



.
 
Awafukuze wangapi? na washauri wengi toka mawaziri mpaka wakuu wa majeshi na polisi na Hosea................
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom