FikraPevu
JF-Expert Member
- Jan 2, 2010
- 303
- 236
Kutokana na kasi ya wanachama wa vyama vya upinzani kuhama vyama vyao na kukimbilia Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa lengo la kuunga mkono juhudi za rais John Magufuli za kupambana na ufisadi, wachambuzi wa siasa wameitafsiri hali hiyo kuwa ni kutafuta maslahi ya kisiasa.
Hamahama ya wanachama ilishika kasi baada ya Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu kujiuzuru nafasi yake ya ubunge kutoka CCM kwenda Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Kuondoka kwake kulifungua milango kwa viongozi wa vyama vingine vya upinzania kuwa na ujasiri wa kujiuzuru nafasi zao za uongozi na kukimbilia katika chama tawala.
Siku chache zilizofuata wanachama kutoka vyama vya upinzani walianza kuingia CCM ambapo mwishoni mwa wiki iliyopita Mbunge wa Kinondoni (CUF), Maulid Said Mtulya alitangaza kujivua uanachama na kuomba ridhaa ya kuingia CCM kwa hoja zinazofanana na wanachama wanaoingia katika chama hicho tawala.
Wachambuzi wa Siasa za Afrika Mashariki wamejitokeza na kusema kasi hiyo inatafsiri nyingi ikiwemo ya ubinafsi na kutafuta maslahi ya kujinufaisha kisiasa ambayo yanatokana na kukosekana kwa utashi wa kisiasa na mfumo wa kisheria unaosimamia haki za vyama vya siasa kuendesha shughuli zao kwa uhuru na uwazi.
Akizungumzia suala hilo, aliyewahi kuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Mwesiga Baregu amesema ubinafsi wa wanasiasa ambao hauzingatii maslahi mapana ya wananchi ndio sababu inayowafanya wabadilike kila mara na kukimbilia katika vyama vingine ili kutafuta ahueni ya maisha.
Zaidi, soma hapa => Kasi ya wapinzania kuhamia CCM yawaibua wasomi nchini | FikraPevu
Hamahama ya wanachama ilishika kasi baada ya Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu kujiuzuru nafasi yake ya ubunge kutoka CCM kwenda Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Kuondoka kwake kulifungua milango kwa viongozi wa vyama vingine vya upinzania kuwa na ujasiri wa kujiuzuru nafasi zao za uongozi na kukimbilia katika chama tawala.
Siku chache zilizofuata wanachama kutoka vyama vya upinzani walianza kuingia CCM ambapo mwishoni mwa wiki iliyopita Mbunge wa Kinondoni (CUF), Maulid Said Mtulya alitangaza kujivua uanachama na kuomba ridhaa ya kuingia CCM kwa hoja zinazofanana na wanachama wanaoingia katika chama hicho tawala.
Wachambuzi wa Siasa za Afrika Mashariki wamejitokeza na kusema kasi hiyo inatafsiri nyingi ikiwemo ya ubinafsi na kutafuta maslahi ya kujinufaisha kisiasa ambayo yanatokana na kukosekana kwa utashi wa kisiasa na mfumo wa kisheria unaosimamia haki za vyama vya siasa kuendesha shughuli zao kwa uhuru na uwazi.
Akizungumzia suala hilo, aliyewahi kuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Mwesiga Baregu amesema ubinafsi wa wanasiasa ambao hauzingatii maslahi mapana ya wananchi ndio sababu inayowafanya wabadilike kila mara na kukimbilia katika vyama vingine ili kutafuta ahueni ya maisha.
Zaidi, soma hapa => Kasi ya wapinzania kuhamia CCM yawaibua wasomi nchini | FikraPevu