Wasomi Tanzania wagawanyika

MWITONGO MAARIFA

JF-Expert Member
Aug 11, 2018
276
1,428
Nikifuatilia mswada wa mafao kwa watumishi naona hakuna Mbunge wa CCM, hakuna mtumishi wa umma Wala mwanasiasa kutoka chama tawala anayeona mapungufu ya sheria ile na kanuni zake, ila viongozi wa vyama vya upinzani, wanaharakati na viongozi wengine waliopo nje ya serikali na chama tawala wanaona mapungufu lukuki.

Je Kati ya wasomi ndani ya serikali na nje ya serikali na chama tawala ni nani anayewaza sawasawa kuhusu sheria hiyo?

Sheria ya makosa ya mtandao pia inatetewa na serikali na chama tawala na watumishi wa umma lakini asasi za kirai,wanaharakati na vyama vya upinzani wanaona kasoro lukuki. Je wasomi wapi wapo sahihi Kati ya makundi haya mawili?mbona wamesoma vyuo sawa na wote wakafaulu?

Sheria ya takwimu, CCM na watumishi wa umma walisema ni mzuri na inatija kwa taifa lakini wanaharakati na wanasiasa wa upinzani wakaukataa na baadaye wazungu wakaingilia Kati. Wazungu waliposema serikali ikawasikia kidogo lakini tofauti ya hoja ya wazungu na wanaharakati wazawa ilikuwa ni KIINGEREZA kilichopambwa na misaada.Je na hapo napo wasomi waliona makengeza?

Mswada wa vyama vya siasa hivyohivyo, kwanini wasomi wanagawanyika kwenye hoja ambazo zipo wazi? Unafiki huu unaletwa na Nini? Kati ya makundi haya mawili ya wasomi lipi linainyonya nchi? Kindi lipi limejaa wasomi wasio wazalendo na wabinafsi?

Moja jumlisha moja ni mbili lakini upo wakati inakuwa tatu na jibu hilo linasimamiwa na Dolla na kupigiwa makofi na watunga sheria
 
Hao wanaopitisha hizo sheria sijui wamelogwa na shetani. Utafikiri hawana ndugu humu uswahilini asee..

Hivi ni kulewa madaraka au ni kulogwa?
 
Kusikia kwa kenge,ni mpaka damu zimtoke masikioni.

Wabongo wanahitaji utawala wa aina hii ili wajitambue na kuwa kitu kimoja.

Awamu hii itatufundisha kudai haki zetu pasipo kujali itikadi zetu.

Awamu hii pia itapunguza tabaka la wasaliti ingawa baadhi bado wataendelea kuwepo.
 
Ukitaka upate sababu hoja yako ingejikita kwa mifano hai bila kumng'unya maneno. Sijui tulienda shule au walienda shule kwaajili ya kitu gani maana niaibu. Kwa mfano professor kaaaabud what is he doing? Kasahau kabisa na wala hazungumzii kabisa katiba mpya na ndiye mwenye zamana. Jamani tuisaidie jamii na siyo matumbo yetu na kuwatumikiamabwanaaa.
 
Serikali rudisha FAO LA KUJITOA

fao LA kukosa ajira ni kirusi na utumwa mamboleo, imagine MTU haruhusiwi kuresign

Embu pitieni kanuni za FAO LA kukosa ajira, jamani..ni hatari...uporaji mchana kweupe
 
Mijitu jobless ndio mnapiga kelele
Pathetic walahi
Pilipili iko shamba inakuwashia nini?
Nendeni mkalime mwondakane na idle mind
Duh sad
 
Kila jambo linaloletwa linawekwa au linahusishwa na siasa hata kama halistahili liwe hivyo. Tatizo linaanzia hapo.

Mswada kama huu haustahili kabisa kuangaliwa kisiasa.
 
Mijitu jobless ndio mnapiga kelele
Pathetic walahi
Pilipili iko shamba inakuwashia nini?
Nendeni mkalime mwondakane na idle mind
Duh sad
Wewe umepewa kazi za buku 7

Wasaka tonge. ..by Nape

Kazi kumpamba mfalme tu

Tumia akili aisee...Shangazi zako wanaporwa haki
 
Back
Top Bottom