Wasomi mna wajibu mkubwa kuondoa umasikini-Pinda

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Wasomi mna wajibu mkubwa kuondoa umasikini-Pinda
Waandishi Wetu
Daily News; Thursday,August 07, 2008 @00:03

Waziri Mkuu Mizengo Pinda amewataka wasomi, watafiti na wanataaluma kuwa wazi kukosoa sera ya uchumi kama wanaona haiko sahihi katika kuondoa umasikini wa wananchi. Pinda alisema wasomi hao wana jukumu la kuhakikisha sera zinazotungwa na serikali zinakuwa za manufaa kwa jamii na pale wanapoona mambo hayaendi pia wanatakiwa kuwa huru kuzikosoa pale inapowezekana.

“Ndio maana nasema wataalamu lazima sasa watoe maoni yao na pale wanapoona sera tulizonazo hazisaidii kupunguza umasikini waseme na wakosoe kwa uwazi,” alisema Pinda. Waziri Mkuu aliyasema hayo wakati akifungua mkutano wa kimataifa unaojadili juu ya sera za maendeleo ambao umeandaliwa na Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM).

Mkutano huo unashirikisha wanataaluma, watafiti na watunga sera wa Tanzania na baadhi ya washiriki wanatoka katika bara la Ulaya, Afrika na India. Alisema tafiti za wasomi zina umuhimu mkubwa kwa jamii hasa katika utatuzi wa matatizo kadhaa yanayoikabili jamii katika maisha yao ya kila siku. Alisema wasomi na watafiti wanatakiwa kuhakikisha kazi zao zinatoka nje ya kuta za vyuo vikuu na kwenye maktaba.

Alisema tafiti hizo zisiishie kwenye makabati ya vitabu na kuwanufaisha watu kwani wananchi pia wana haki ya kujua tafiti wanazofanya wasomi hao. Naye Profesa Thadeus Sata wa IFM alisema wameitisha mkutano huo kwa lengo la kuangalia sera ya uchumi na mchango wa sekta ya fedha katika ukuaji wa uchumi.

Katika tukio lingine Pinda amekemea tabia ya baadhi ya madaktari na maofisa wa Afya nchini ya kuuza dawa na vifaa vya hospitali ambavyo vinapelekwa na Serikali mikoani kwa ajili ya kuhudumia wananchi. Akipokea msaada wa dawa juzi Dar es Salaam kutoka kwa Balozi wa Heshima wa Jiji la Hamburg la Ujerumani kwa Tanzania, Juergen Gotthardt kupitia taasisi ya Action Medeor, Pinda aliwataka wanaofanya vitendo hivyo kuacha mara moja.

Aliwataka madaktari wa mikoa na wilaya kusimamia kwa makini dawa zinazopelekwa katika maeneo yao ili zitumike kwa matumizi yaliyokusudiwa. Taasisi hiyo ya Ujerumani ilitoa jumla ya dawa zenye thamani ya Sh milioni 5.5 kwa ajili ya zahanati 20 na vituo vya afya vitano vya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Rukwa.
 
Hii njemba inaongea na both sides of his mouth. Alikuwa mstari wa mbele kutamka kwamba wahusika wa ufisadi wa EPA ni matajiri wakubwa wakikamatwa nchi itawaka moto. Ushauri wa kuwashughulikia mafisadi ulitolewa na Watanzania wote wakiwemo wasomi. kuhusu mikataba ya madini, Watanzania wote wakiwemo wasomi wamepiga kelele mara chungu nzima kwamba haina maslahi na nchi.

Huu ni mwaka wa tatu tangu JK aingie madarakani na mpaka hii leo hakuna chochote kilichofanyika kuhusiana na kelele hizo za Watanzania pamoja na kuwa aliahidi wakati wa kampeni kwamba mikataba hiyo itaangaliwa upya ili kufanyiwa marekebisho.

Wakati Barrick na shareholders wao wakiendelea kupata faida kubwa kutokana na bei ya juu ya dhahabu katika soko la dunia, Tanzania haiambulii chochote. Pinda kama huna cha kuzungumza wakati mwingine ni bora kunyamaza kuliko kutoa hotuba zenye tofauti kubwa na kauli zako za nyuma.
 
Hizi ndo dizaini za speech ambazo mtu unaandaliwa na wasaidizi wako halafu wakati wa kuzi-present unaanza ku-sweat vikwapani kwa kuwa unafahamu kua kila mtu anayekusikiliza anafahamu kwamba you don't mean what you say...

Muache kutuyeyusha jamani!!!!!!!!!!! Sisi si wajinga kiasi mnachofikiri.
 
Miyeyusho Pinda, je na wewe umetutengenezea uwanja gani halali wa kuikosoa serikali maana pamoja na juhudi zetu za kuikosoa serikali, serikali imeonyesha wazi kutosikiliza na kutokubali? Je wewe Pinda kwani mpaka sasa sera ya serikali ya CCM ya uchumi unaionaje? Haijakosolewa? Nadhani ni muda mwafaka kuomba kupunguziwa kutkosolewa, maana mmekosolewa zaidi ya kusifiwa na lakini bado hujajua mmekosolewa.
Tuambie Pinda, je wewe mwenyewe unakubali kujadiliana ama kukosolewa kuhusu madini, EPA, uchaguzi mkuu, nk.
Pinda, serikali yako ya CCM imeonyesha inajua kila kitu na inataka wote tuwasikilize na kufuata nyayo zao tu.
 
Yah ndio siasa ya bongo hiyo.Kaongea maneno mazuri ila ndio hivyo kama ilivyosemwa na wajumbe waliotangulia ushauri wanapewa kila kukicha ila utekelezaji zero.
Sasa wapo ndio pia inakuja kazi ya waandishi na sisi kwa ujumla kuwauliza mbona ushauri mwingi umetolewa tu ila ndio hivyo ............
 
Ni kweli kwamba wasomi wana wajibu mkubwa wa kuondoa umasikini katika taifa lolote lile laikini si tanzania.maana Tanzania mwanasiasa huwa anasikilizwa zaidi ya wasomi hao ambao wanawalilia, shida hapa ni kwamba wanasema wasiyoweza kyatenda na wanatenda wasiyoweza kuyasema ilamradi tu wasikike wamesema.naamini hiyo speech ameandaliwa siyo yake na hilo ndo tatizo kubwa la wanasiasa wtu na ndo maana hata wasomi sasa wameamua kufuata hukohuko nao wakafaidi.
 
Kukosolewa hapa JF ndio order of the day.. au hawasomi maoni, ushauri n.k unaotolewa hapa?? Rhetorics as usual!
 
Hivi kuna mtu anajua ni kiasi gani cha pesa serikali inatoa kwa ajili ya tafiti katika vyuo vikuu na vituo vya utafiti?
 
Chenge kasoma Havard.

I mean havard lakini Mwizi Mwongo na ni mtu wa makusudi.

Sasa msomi huyu wa Havard na Kaperiensi yake yote anapwaya kiasi hicho! Ukitaka kumsahuri usemi wako wa kwanza utakuwa nini?

Mijitu ndani ya serikali ya CCM inafanya mambo yote ya Ovyo kwa juhudi za makusudi.
Kibaya zaidi, mambo mengi ya ovyo yanasukwa kwa muda mrefu tena kwa kutumia mianya ya sheria na ukiritimba wa madaraka na uzuzu wa kinyang'au.

Hivi tunaweza kushauri watu wanaopenda Pesa kuliko Familia zao wenyewe?
Tunaweza kuwashauri watu ambao mitoto yao mikorofi wanaileta uhamishoni hapa USA ili iharibikiwe zaidi?
Unaweza kuwashauri Viongozi wa serikali wenye mawazo mabaya kuliko ya mkoloni wa Kiingereza?
Unaweza ukawashauri Viongozi wanaamini wanajuakila kitu?

Unaweza kuwashauri viongozi ambao silaha zao kubwa ni Kusema uongo kisha ukweli ukibainika wanajificha nyuma ya mitunduru?

Ni rahisi kumshauri mnyama Simba kuwa Vegetarian kuliko kuwashauri Viongozi wa serikali ya CCM kuacha tamaa za kifisifisi.

Ushauri wetu mkubwa ni huu; waige mfano wa Wakiri Dharimu, sivyo siku ikifika si ndani wala nje kutakako kalika.
 
Wasomi wamewafichua wezi na wahujumu Uchumi wa Taifa Mh.Pinda mmewapeleka wapi mafisadi waliofichuliwa ni bora kwanza ukaueleza umma kutokana na jitihada walizochukuwa wasomi na kuwawekea wazi wizi unaofanywa ndani ya serikali ,yaani mmepewa ushahidi kabisa na mambo yapo wazi.
Mnapozungumza msiwe mnakurupuka tu halafu wakiwapigia makofi mkaona mmesema mambu ya maana kumbe mmewavuruga akili yao badala ya kukasirika inawabidi wacheke kicheko cha Uchungu,inakuwaje kiongozi wa Serikali analisemea jambo linahusu Serikali eti analirudisha CCM ,jaribuni kutenganisha shuguli za Chama na Serikali mnapokuwa mmechaguliwa kuongoza Taifa.
 
Wasomi mna wajibu mkubwa kuondoa umasikini-Pinda
....."Ndio maana nasema wataalamu lazima sasa watoe maoni yao na pale wanapoona sera tulizonazo hazisaidii kupunguza umasikini waseme na wakosoe kwa uwazi," alisema Pinda....

Wanasiasa wa Tanzania kweli wana mambo!!...Ati sasa kazi ya kuondoa umasikini nchini weshatupia wasomi. Wao wanasiasa waendelea kutesa na migari yao ya nguvu huku wakiiuza nchi yetu bila hata ya haya. Sasa kazi yao huko bungeni na serikalini itakuwa ni nini? Ama kweli Tz ni shamba la wajinga!
 
Wanasiasa wa Tanzania kweli wana mambo!!...Ati sasa kazi ya kuondoa umasikini nchini weshatupia wasomi. Wao wanasiasa waendelea kutesa na migari yao ya nguvu huku wakiiuza nchi yetu bila hata ya haya. Sasa kazi yao huko bungeni na serikalini itakuwa ni nini? Ama kweli Tz ni shamba la wajinga!
Raisi mashaka matupu na Waziri mkuu nae mashaka matupu ,nina wasiwasi kuwa hawa watu wametekwa kweli ,maana zile kasi ,makeke na nguvu zao zote sasa wanaonekana hata miguu yao haishiki tena.
 
Mimi ni msomi, na ninataka kumfundisha Waziri Mkuu Pinda somo rahisi sana ambalo mababu zetu hawakusubiri wasomi wawafundishe:

Ukitaka kunyoosha chuma kilichopinda, lazima kwanza ukiweke kwenye moto mkali sana kiungue mpaka kiwe chekundu, halafu unyooshaji wenyewe unaufanya kwa kukipiga kwa nyundo nzito sana haraka haraka tena kwa nguvu sana kingali cha moto.

Je yeye na rafiki zake wako tayari kwa prescription hiyo?
 
Back
Top Bottom