Wasira: Siachii ubunge kwa vijana ni wavuta bangi..!!!

Huyu wasira kadata yaani sababu anayosema kuwa hataki kuachia madaraka kwa vijana ati ni vijana wanakula bangi…..!!!! nchi kibao wanakula mjani,Holland kule wanakula mjani,Jamaica na sehemu kibao.Sisemi hivi natetea wanala mjani ,la hasha! Sababu alioitoa ni mufilisi kwa mtu mzoefu kama Tyson ni fedheha sana na matusi kwa vijana…ni aibu kubwa kwa mtu mzima kama Wasira

….sababu yake ya kutoachia madaraka ni selfshiness yake....nilimsikia akisema alianza kuwa mbunge tangu mwaka 1970 anajisifia kwa masifa kede kede…. miaka zaidi ya 30 yuko bunge ati haachii kiti cha ubunge kisa vijana wanavuta majibangi.Mzee kama wasira waliokaa bungeni zaidi ya 30 sitetegemei awe na kauli kama hizi..….kafanya nini Tyson bana mpaka asema kuwa haachii madaraka kisa vijana wanakula mjani…...

Hii kwa wasira naiita ni kutokojiamini, hofu,ubinafsi hana lolote anaweza fanya zaidi ya kukaa bungeni…..yaani jitu kama wasira anaona hamna watu zaidi yake wanaweza kuwakilisha watu bungeni?
Hakuna uhusiano wa umri na madaraka aachie madaraka …….kauli ya hofu hizo….. kudadadeki naenda chukua fomu….kuniloga hamuwezi niko fiti….

Term limits (say two terms) za ubunge zitaondoa aina ya Mibunge kama hii........
 
hivi kwa sasa hivi wasirra ni waziri katika ofisi ya prime minister na utawala wa mikoa na serikali za mitaa? hizi data/kumbukumbu zinatoka wapi? ndio maana wassira anaongelea wavuta bange miongoni mwetu.
Hayo yameandikwa kwenye mtandao angalia tanzania politician
 
Huyu Wasira amshukuru sana marehemu Mzee Kawawa kwa kumpigia debe kurudishwa CCM ama sivyo mpaka leo angekuwa anauza samaki pale Namanga!! Anaposema vijana hawafai kuwa viongozi kwavile wanapuliza ganja ana maana hawa wakina Ngeleja, Hussein Mwinyi na Masha wamepewa ujiko na muungwana japo wanalipuuliza ganja? Wasira anazeeka vibaya na yote hiyo sababu ya njaa; pale kilimo anamuangusha Jakaya, jamaa hafanyi lolote la maana ila ni kuiba tu!!
 
Dawa ya watu kama wassira ni kutafuta vijana wenye uwezo na kuwasimika Bunda, tupige kambi kule hadi ang'oke... tuhimize vijana wote wachukue kadi za CCM, wote washiriki kwenye mchujo wa mgombea CCM halafu tupige kura; tukishamaliza tunaacha fair competition kati ya huyo kijana na wapinzani wote

Wassira is living in the past!!! Let us show him the power of our young generation
 
Mengine mnamuoneya kabisa; Wassira hajawahi kuishiwa pesa kiasi cha kuomba supu au kutembeza samaki. Alikuwa anasafirisha samaki kwenda nchi za nje na ingawa malipo yalikuwa siyo makubwa lakini alikuwa hana shida ya pesa kiasi hicho. Tatizo kubwa alilokuwa nalo ni kule kukosa madaraka baada ya kuwa nayo kwa miaka 26 mfululizo. Kitendo cha kujikuta na raia wa kwaida asiyekuwa na hata punje ya daraka kilikuwa kinamsumbua sana kisaikolojia.

Pamoja na yote hayo, Wassira ana historia ndefu sana iliyojaa bahati na mafanikio makubwa sana kisiasa. Kwanza siyo kweli kuwa alipewa madaraka kwa sababu ya kuoa binti wa Nyerere. Nitaeleza histroia yake kadri ninavyomfahamu.

Stephen Masato Wasira alisoma Nyambitilwa kule Ushahi na kumalizia darasa la nane pale shule ya kati ya Kisangwa. Baada ya hapo alijishughulisha na shughuli za TYL ambayo ilikuwa inasimamiwa na Kiboko Nyerere (mdogo wa Nyerere); hivyo alianza connection angali mdogo sana. Akiwa kwenye TYL akafanikiwa kupata kazi ya serikali kama Bwana Maendeleo huko Ukerewe. Wakati akiwa Ukerewe, alijza form ya kugombea Ubunge wa Mwibara baada ya mbunge wa wakati huo Chiliko kuwa mkuu wa Wilaya huko Shinyanga. Katika kipindi cha uchambuzi wa wawagombea, Wassira akapata nafasi nyingine mjini Musoma kuwa katibu mtendaji wa TANU wa wilaya ya South Mara. Katika kinyang'anyiro kile cha ubunge wa Mwibara, Wassira alipambana na mtu anaitwa Muyenjwa, ambaye alikuwa Division Executive Secretary wa tarafa fulani hivi. Ushindi wa Wassira katika uchaguzi ule wa 1970 ulitokana na tabia ya dharau na ukatili wa Muyenjwa katika madaraka aliyokuwa nayo wakati ule; kwa hiyo watu wakamwadhibu Muyenjwa kwa kumnyima kura na kumpa mpinzani wake (yaani Wassira) ambaye alikuwa hafahamiki - hiyo ilikuwa bahati ya kwanza ya Wassira.

Akiwa mbunge, Wassira alichaguliwa kuwa waziri mdogo wa Kilimo mwaka wa 1972 kufuatia reshuffle iliyofanywa na Nyerere baada ya mauaji ya sheikh Karume; alikaa katika madaraka hayo kwa miaka kama miwili au mitatu hivi ambapo mwaka 1974 akateuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara kuchukua nafasi iliyoachwa na Ackland Mhina alipokwenda kuwa balozi wetu huko nje. Akiwa Mkuu wa mkoa ndipo alipooa mtoto wa chief Wanzagi Nyerere; kwa hiyo siyo kweli kuwa alipewa madaraka kwa kuwa alikuwa ameoa kwa Nyerere, No, alioa kule wakati akiwa na madaraka. Inawezekana ndoa ile ilimuimarisha katika nafasi ile ya ukuu wa mkoa kwa sababu alikaa pale Musoma hadi mwaka 1983, yaani karibu miaka 9 hivi. Kuna madudu kadhaa aliyofanya pale Musoma ambayo sitayataja kwa vile sina ushahidi nayo ila mwanzoni mwa mwaka 1983 watu wa Musoma walimwambia Mwalimu waziwazi pale kwenye uwanja wa shule ya Msingi Mukendo kuwa, atakapoondoka kurudi Dar es Salaam baada ya mapumziko yake ya krismas ni lazima aondoke na mtu wake (yaani Wassira)- wao walikuwa hawamtaki tena. Kwa vile Nyerere alikuwa hataki kuwaudhi zaidi ndugu zake wa Musoma (unawajua jinsi walivyo wakali), kweli akafanya hivyo; mwishoni mwa mwaka 1983 hiyo hiyo Wassira akaondolewa pale Musoma na kuwekwa Mambo ya Nje alikoishia ubalozini Washington, DC. Nashindwa kutambua kama hapo alikuwa na bahati au alikuwa amejiunganisha vizuri kisasa, lakini hakusota.

Katika uchaguzi wa mwaka 1985, Wassira aligombea jimbo la Bunda ambalo wakati huo lilikuwa linashikiliwa na Mugeta. Kwa bahati mbaya kama ilivyokuwa kwa Muyenjwa, Mugeta naye alikuwa na ishu zake kiasi kuwa Mwenyekiti wa CCM wa Bunda aliyekuwa akijulikana kama Munubi Salamu, alianza kupiga kampeini kuzuia Mugeta asichagulie katika uchaguzi ufuatao, na badala yake mpinzani wake ndiye apewe kura hata kam wakati huo mpinzani halisi alikuwa hajajulikana. Baada ya jina la Wasira kuibuka, mzee Salamu akageuka ili kupiga kampeini FOR Mugeta, lakini hakuweza kuponyesha damage aliyokuwa keshafanya. Hivyo Wassira akachaguliwa kama njia ya kumwadhibu Mugeta - Hiyo ilikuwa ni bahati nyingine.

Baada ya ushindi huo Wasira akawa waziri mdogo wa serikali za mitaa na ushirika na baadaye akawa waziri kamili nadhani wa kilimo. Katika nafasi zake za uwaziri alizifanya kwa ufanishi wa kuridhisha sana, na hivyo kwa karibu miaka karibu 10 yote iliyofuata hadi 1995, Wassira alikuwa madarakani.

Hata hivyo wakati wa uchaguzi wa 1995 alijikuta akishindana na waryoba kupitia CCM na hivyo akaenguliwa kulingana na uzito aliokuwa nao waryoba kichama. Kwa mabavu yake, waryoba akahamia NCCR mageuzi ambako alishinda kiti cha Bunda dhidi ya Waryoba. Kulikuwa na ukweli kuwa Wassira alitumia njia chafu sana katika uchagzui ule ili kumshinda waryoba, hivyo mahakama kuu ikatengua ubunge wake na kumzuia asigombee position yoyote kwa miaka mitano. Kipindi hicho ndicho Wassira alipokaa benchi na pia hakuweza kushiriki uchaguzi wa mwaka 2000 kutokana na amri hiyo ya mahakama. Mwaka 2005 akagombea tena Bunda na kushinda hadi kuwa waziri, kazi aliyo nayo hadi sasa. Ushindi huo wa 2005 nadhani aliupata kutokana na jina lake kuwa kubwa na vile vile mbinu zake za kisiasa kuwa zimekomaa; ushindi huo haukuwa wa bahati tena.

Hata hivyo, kutokana na historia yake, ni wazi kuwa Wassira hana profession yoyote nje ya siasa. Kuna wanasiasa ambao walikuwa na profession zao kabla ya kuingia kwenye siasa lakini Wasira siyo mmoja wao - yeye ni career politician.
Kichuguu,
Hivi yule mama mkwe wa Wassira, mwalimu wangu Radegonda, alikuwa mke wa Chief Wanzagi kweli? Nitawauliza akina Lucy na Flora. Ukweli ni kuwa hata mpige kelele gani Wassira haondoki kwenye siasa angalau kwa sasa. Ni mmoja wa mawaziri wanaojua kuzitumia taasisi zilizo chini ya wizara anayopewa kuiongoza.
 
Wasira anfikiri vijana peke yao ndio wavuta bangi hata wazee nao huvuta bangi kwani yeye halijui hilo. Jamaa hapa karopoka. Anafikiri yeye ndo anamua? Ni wapiga kura ndo huamua nani awe Mbunge na sio yeye. Aende zake amefulia.
 
Kuna kipindi alidata hadi akafanya biashara ya sato kuleta mjini. wacheni atafute hela za uzeeni -
 
- Wassira siku zote ni mwanasiasa mjanja sana, Warioba aliposhika kiti chake cha ubunge alimpeleka majuu asirudi kumsumbua, ni mmoja wa wanasiasa wa kwanza sana kujiunga na Mtandao kwa siri, ndio maana sasa anachuma matunda yake!

- Na ni almost awe PM kama sio wazee wa nchi kuingilia kati! yupo mpaka Mtandao uishe nguvu! na akiona unaisha kama kawa ataruka viunzi na kuwahi wapya wenye nguvu zaidi! maana huko kwao ana ujanja flani unaowashinda wengi!

Respect.


FMEs!
 
Wakubwa, mbona mmeisahau mizee mingine nayo ina kauli hizo hizo? Mbona hata Makweta kasema hivyo, na Malechela? Wote manyang`au tu hawa, 2010 tuwapige chini!
 
- Wassira siku zote ni mwanasiasa mjanja sana, Warioba aliposhika kiti chake cha ubunge alimpeleka majuu asirudi kumsumbua, ni mmoja wa wanasiasa wa kwanza sana kujiunga na Mtandao kwa siri, ndio maana sasa anachuma matunda yake!

- Na ni almost awe PM kama sio wazee wa nchi kuingilia kati! yupo mpaka Mtandao uishe nguvu! na akiona unaisha kama kawa ataruka viunzi na kuwahi wapya wenye nguvu zaidi! maana huko kwao ana ujanja flani unaowashinda wengi!

Respect.

FMEs!
Warioba hakumpeleka majuu Wassira.
 
Huyu naye sasa anachemsha. Anajeuri gani ya kusema kuwa aachi ubunge? Kwa mtazamo wangu, wapiga kura wake ndo wenye uwezo wa wakusema kuwa aachie au asiachie.

Ningekuwa mimi ni kijana kwenye jimbo lake la uchaguzi nisingempigia kura kabisa, kwani amemaanisha vijana wote ni wavuta bangi, wakati wao ni sehemu kubwa ya kura zilizomweka madarakani.

Hawa vijani wa jimbo lake wambane ili aoneshe wavutabangi anaowataja na akishindwa wafungulie mashtaka.
 
Wassira naye ni one of those 'bushed' polititians ambao wameishiwa sera vichwani wanaishia kutoa maneno ya kibaguzi yenye kukera. We are not at 'war' here between the old and young. Hata statement yake itafsiriwe vipi amefanya kosa la kudhalilisha vijana kwamba hawafai kuachiwa uongozi na kwa sababu ya bangi.

What is being suggested/asked is that at least wazee ambao wamekuwa wabunge tangu ujana wao wawaachie na wengine hususan vijana wa sasa nao washike nafasi hizo. Is that unreasonable and too much to ask to warrant insulting the youth?
 
Huyu naye sasa anachemsha. Anajeuri gani ya kusema kuwa aachi ubunge? Kwa mtazamo wangu, wapiga kura wake ndo wenye uwezo wa wakusema kuwa aachie au asiachie.
Ningekuwa mimi ni kijana kwenye jimbo lake la uchaguzi nisingempigia kura kabisa, kwani amemaanisha vijana wote ni wavuta bangi, wakati wao ni sehemu kubwa ya kura zilizomweka madarakani.
Hawa vijani wa jimbo lake wambane ili aoneshe wavutabangi anaowataja na akishindwa wafungulie mashtaka.
Hii ndiyo jeuri ya viongozi wetu. Wanafikiri ni haki yao peke yao kuwa wabunge. Ndiyo maana wakisikia mwingine anagombea wanaanza kujiliza oh anatumiwa na mafisadi, oh wanataka kuchukua jimbo langu....what is this?
 
Wassira naye ni mvuta bangi ,na tena huenda naye anamiliki shamba la Bangi ndio maana akajua kuwa vijana wanavuta kwani wanaenda kununua kwake.
 
Mwenye historia yake kifamilia, I mean mke, watoto, atumuvuzishie....
 
mwenye historia yake kifamilia, I mean mke,watoto, atumuvuzishie....

Mimi ninajua familia yake vizuri lakini sidhani kama ina maana yoyote kuzungumza mambo ya familia yake kwenye forum kama hii kwa vile wao hawajihusishi na siasa. Ni lazima tuheshimu privacy yao kwa vile hawajataka kujiweka hadharani. Kuna viongozi ambao mambo ya familia yao ni haki ya kila mtanzania kwa vile familia nzima zimejikita kwenye siasa, lakini familia ya Wasira haiko hivyo; kwa hilo ni lazima tuwaheshimu.
 
Back
Top Bottom