Wasipokaa chini na kumaliza tofauti zao, naiona Vita kati ya Nairobi na Dodoma inakaribia

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,385
108,453
Sinema ilianzia kwa Kenya kuzuia Magari ya mizigo ya Tanzania kuingia Kwao kwenda kuuza Mahindi na Tanzania nayo ikajibu mapigo kwa kuwapandishia ' tozo ' bidhaa zao ngoma ikawa draw ( Waswahili wanasema sare )

Sinema ya pili ikaendelea tena ambapo kwa sasa kuna taarifa za chini chini kwamba Watanzania wanaoishi na kufanya Shughuli zao nchini Kenya wanapata wakati mgumu kidogo ( japo Ubalozi wetu huko unajifanya kama vile haujui kitu ) ila kuna ' jambo ' linaendelea huko nawaombeni tu fuatilieni kimya kimya mtalijua. Mara tena na huku Tanzania kupitia pale mpakani Namanga Wafanyabiashara wa Kenya nao wamekuwa wakipigwa bonge la ' pini ' kuingia bidhaa zao ' Bongo ' na hali haipo sawa.

Sinema ya tatu na ya mwisho jana tulishuhudia Mamlaka ya Tanzania ikiteketeza kwa ' moto ' Vifaranga vya Raia wa Kenya ' Mwanamama ' mmoja hali ambayo kiukweli imepokelewa kwa hisia kali sana na Wakenya wengi. Na ni leo hii hii huko nchini Kenya katika mpaka wao na Tanzania kwa upande wa Mkoa wa Mara Ng'ombe takribani 4,000 kutoka nchini Tanzania zimekutwa zimeingia katika ardhi ya Kenya kinyume cha Sheria na hivi ninavyoandika huu ' uzi ' kuna taarifa za chini chini kutokea huko Kenya zinasema kwamba huenda hao Ng'ombe nao wakachomwa moto au wakauwawa ' Kikatili ' sana ili kulipiza ' Kisasi ' cha tukio la wale Vifaranga.

Kila siku mnatuhimiza Watanzania tuwe Wazalendo hivyo basi Mimi GENTAMYCINE nawaomba Mawaziri wa Mambo za Nje wa Tanzania Balozi Mzee Mahiga na yule wa Kenya Mwanamama Balozi Amina ( kama sijakosea ) upesi sana wakae chini waweze kujadili haya mambo ambayo naona kama hayatotafutiwa ' ufumbuzi ' haraka kuna hatari ya Kenya na Tanzania kuingia ' Vitani ' au kuwa katika ' Uhasama ' mkubwa mno ambao unaweza ukaathiri hata huu ' Utengamano ' wetu wa Kikanda na wa Kijumuiya.

Tusidanganyane na kufichana hapa ukweli ni kwamba hali ya Kidiplomasia kwa sasa kati ya Tanzania na Kenya siyo nzuri na kuna wanaosema kwamba Kenya wamekuwa na ' bifu ' zaidi na Tanzania hasa baada ya kukosa lile ' dili ' la Bomba la Mafuta lakini pia inasemekana Tanzania nayo imekuwa na ' bifu ' na Kenya kupitia Raila Odinga ambaye inasemekana ana ' Urafiki ' na Mtanzania mmoja ( japo Mimi GENTAMYCINE bado sijamjua ni nani ) na pia kwa Kenya kuwa na ukaribu wa ' ajabu ' na Watu ambao Kisiasa wanaonekana kuwa na ' uadui ' na washika dola wa sasa wa Tanzania.

Naomba niishie tu hapa tafadhali ila uzuri ni kwamba nimeshatahadharisha mapema hivyo Kazi Kwenu Wahusika.

Nawasilisha.
 
Kaka huwa hashauriki kauli zake zinakinzana zenyewe tunafanyaje hapo

Ila hata na ' Uncle ' wa Kenya nae ni ' Kiburi ' sana Mkuu na ndiyo maana nimewaomba ' Wasaidizi ' wao Wakuu hao Mawaziri wawili wa Foreign na ambao kwa bahati nzuri sana wameiva vizuri ki Diplomasia na ni Mabalozi pia bila kusahau kwamba wote pia wameiva hasa Kijasusi / Kinjagu wakutane wamalize hii ' Kitu ' la sivyo moyo wangu unasita mno na kuniambia kinaweza Kikachafuka / Kikanuka siku si nyingi kwani dalili tu za awali za ' Viashiria ' vya ' machafuko ' vimeanza kujitokeza.
 
Sisi na Kenya sijui tuna nini...uadui wetu uwa hauishi...toka enzi nchi zetu zinapata Uhuru tunavutana tu kwa mambo mbalimbali...hata jumuiya ya Afrika mashariki ya kwanza migogoro mkubwa ulikuwa kati ya tz na ke...baadaye iddi amin akaambulia tu
 
Alichokifanya waziri wetu hakikuwa cha busara, kuweka zaidi vizuri sakata wamasai kukamata wale ng'ombe 4000 ni kulipiza kisasi kwa ng'ombe zao(wakenya) ,zilizoamriwa na mahakama ya tanzania kupigwa mnada ati kwa kisingizio kuingia nchini pasipo halali wakati ni kitu cha kawaida toka enzi na enzi.

Swala la vifaranga hili payback yake bado haijafika inakuja,tusubiri.....
 
Leo umenena vyema, nadhani kwenye mlo wako yalikuwepo matunda,....

Nadhani vile vifaranga wasinge vichoma wange mgonga faini kubwa zaidi ya Bei ya vifaranga wote Ili siku nyingine afuate utaratibu wakuingiza mifugo nchini namba ni vyema huduma za kutoa vibali kutoka wizara ya mifugo zikawepo mipakani Mwa nchi yetu!!!
 
Sinema ilianzia kwa Kenya kuzuia Magari ya mizigo ya Tanzania kuingia Kwao kwenda kuuza Mahindi na Tanzania nayo ikajibu mapigo kwa kuwapandishia ' tozo ' bidhaa zao ngoma ikawa draw ( Waswahili wanasema sare )

Sinema ya pili ikaendelea tena ambapo kwa sasa kuna taarifa za chini chini kwamba Watanzania wanaoishi na kufanya Shughuli zao nchini Kenya wanapata wakati mgumu kidogo ( japo Ubalozi wetu huko unajifanya kama vile haujui kitu ) ila kuna ' jambo ' linaendelea huko nawaombeni tu fuatilieni kimya kimya mtalijua. Mara tena na huku Tanzania kupitia pale mpakani Namanga Wafanyabiashara wa Kenya nao wamekuwa wakipigwa bonge la ' pini ' kuingia bidhaa zao ' Bongo ' na hali haipo sawa.

Sinema ya tatu na ya mwisho jana tulishuhudia Mamlaka ya Tanzania ikiteketeza kwa ' moto ' Vifaranga vya Raia wa Kenya ' Mwanamama ' mmoja hali ambayo kiukweli imepokelewa kwa hisia kali sana na Wakenya wengi. Na ni leo hii hii huko nchini Kenya katika mpaka wao na Tanzania kwa upande wa Mkoa wa Mara Ng'ombe takribani 4,000 kutoka nchini Tanzania zimekutwa zimeingia katika ardhi ya Kenya kinyume cha Sheria na hivi ninavyoandika huu ' uzi ' kuna taarifa za chini chini kutokea huko Kenya zinasema kwamba huenda hao Ng'ombe nao wakachomwa moto au wakauwawa ' Kikatili ' sana ili kulipiza ' Kisasi ' cha tukio la wale Vifaranga.

Kila siku mnatuhimiza Watanzania tuwe Wazalendo hivyo basi Mimi GENTAMYCINE nawaomba Mawaziri wa Mambo za Nje wa Tanzania Balozi Mzee Mahiga na yule wa Kenya Mwanamama Balozi Amina ( kama sijakosea ) upesi sana wakae chini waweze kujadili haya mambo ambayo naona kama hayatotafutiwa ' ufumbuzi ' haraka kuna hatari ya Kenya na Tanzania kuingia ' Vitani ' au kuwa katika ' Uhasama ' mkubwa mno ambao unaweza ukaathiri hata huu ' Utengamano ' wetu wa Kikanda na wa Kijumuiya.

Tusidanganyane na kufichana hapa ukweli ni kwamba hali ya Kidiplomasia kwa sasa kati ya Tanzania na Kenya siyo nzuri na kuna wanaosema kwamba Kenya wamekuwa na ' bifu ' zaidi na Tanzania hasa baada ya kukosa lile ' dili ' la Bomba la Mafuta lakini pia inasemekana Tanzania nayo imekuwa na ' bifu ' na Kenya kupitia Raila Odinga ambaye inasemekana ana ' Urafiki ' na Mtanzania mmoja ( japo Mimi GENTAMYCINE bado sijamjua ni nani ) na pia kwa Kenya kuwa na ukaribu wa ' ajabu ' na Watu ambao Kisiasa wanaonekana kuwa na ' uadui ' na washika dola wa sasa wa Tanzania.

Naomba niishie tu hapa tafadhali ila uzuri ni kwamba nimeshatahadharisha mapema hivyo Kazi Kwenu Wahusika.

Nawasilisha.
Aliyekamatwa na vifaranga ni binti wa kitanzania havina uhusiano na Kenya. Wananchi wa nchi yoyote lazima wafuate sheria ya nchi wanazoishi kutembelea ama kusoma.

Watanzania walifukuzwa Mozambique kwa sab hawakuwa na vibali vya kuishi na nchi nyingi zinadeport watanzania kama Tanzania inavyodeport wageni.

Kufuata sheria ya nchi yako dhidi ya RAIA au bidhaa za kigeni sio chuki uhasama au kisasi.
 
Back
Top Bottom