"Wasiojulikana" wamepunguzwa kasi au ndio tuseme siku hizi kimeeleweka?

Miaka kama miwili iliyopita kasi za kikundi cha "Wasiojulikana" ilikuwa ya juu ajabu. Kulikuwa na tetesi nyingi kuhusu nani hasa walikuwa nyuma ya hiki kikundi, na mengi sana yalisemwa.

Kwa wengi ilikuwa ni vigumu kuamini kuwa kikundi cha "Wasiojulikana" kilikuwa hakina uhusiano na serikali kwa lojiki kwamba wale waliotekwa au kuuwawa walikuwa (victims) na "Wasiojulikana" ni wale tu walioonekana kuikosoa serikali au viongozi wa serikali, na hata Rais Magufuli. Kwa maneno mengine, ilionwa wazi kwamba uwepo wa kikundi cha "Wasiojulikana" ulikuwa kwa manufaa ya serikali iliyopo madarakani.

Na pia watu walihoji uwezo wa kifedha na ujipangaji wa kikosi hiki, ambao ni wazi haukuwa wa kikundi kisicho na mafunzo au kuwa na chanzo kikubwa cha fedha. Kwa mfano, gari aina ya Nissan Patrol mpya inayosemekana kutumika katika tukio mojawapo la "Wasijulikana" linasemakana kuchomwa moto ili kupoteza ushahidi.

Na ajabu ni kwamba mara zote matukio ya "Wasiojulikana" yalipotokea, Polisi walionekana kujiumauma katika kutoa majibu au kufanya upelelezi. Hadi leo hii, hakuna kesi hata moja inayohusu "Wasiojulikana" ambapo wahusika walikamatwa na kuhukumiwa.

Lakini sasa kikundi hiki cha "Wasiojulikana" ni kama kimepunguza kasi yake. Sintadiriki kusema kimefutwa au kukoma kuwapo. Je, ni kwa kuwa watu wameelewa kwamba katika awamu hii ukiikosoa serikali au watawala "utapotezewa" na "Wasiojulikana" ambao ni wazi wanafanya "uhalifu" kwa namna ya kuinufaisha serikali iliyopo madarakani dhidi ya kukosolewa na kutuhumiwa, huku serikali hiyo ikikana kuwafahamu au kuhusika nao. Inawezekana kuna mtu au watu wenye busara waliongea neno la hekima na "Wasiojulikana" wakawekwa gavana, kwa kuwa kuna wakati walifanya vitendo vyao kwa namna ya kuelekea kuwa kama enzi za "State Research Bureau" ya enzi ya Idd Amin wa Uganda, kikosi cha intelijensia kilichoteka na kuua yeyote aliyemkosoa Idd Amin na serikali yake.

Je, kuna siku ukweli kuhusu "Wasiojulikana" utajulikana?
Wasiojulikana wanaojulikana....Pasco Mayalla.
 
Mwache afaidi utajiri. Mtu unapewa fedha za operation ambazo hazina ukaguzi wala risiti, upewe nini zaidi ya hapo! Alikuwa anazigawa kama njugu. Ofisi yake ikawa tofauti na watu kama yeye, hata magari anayotumia - fedha kwa ajili ya kuua na kuteka watu. Labda dhamiri inamsuta ndio maana anahubiri na kulia hovyo. Damu ya mwanadamu ni nzito sana kuimwaga, hasa kwa tofauti za kisiasa tu.
He is guilty in his heart, he will be unhappy the whole of his life.
 
Kwa hili la Wasiojulikana, inabidi uwe na akili za mwendawazimu kudhani kwamba serikali haikuwa inasema ukweli juu yake. Na amini nawaambieni, kuwapo kwa Wasiojulikana na amri zilizotolewa kwao ni jambo ambalo linaweza kuwafikisha viongozi mahakama za kimataifa. Kwa sababu hiyo, upinzani hauwwezi kuachiwa uchukue madaraka 2020 kwa hali yoyote ile, kwa kuwa Upinzani wakichukua nchi jambo la kwanza kufanya itakuwa ni kupata undani wa Wasiojulikana - nani alikianzisha, nani alikisimamia, nani alitoa amri, waliotekwa wako, waliouwawa walizikwa wapi. Fikiria nani atakuwa tayari kuruhusu mazingira ya majibu kwa maswali hayo? Atakuwa tayari kufanya lolote ili mazingira ya ukweli yasipatikane.
Word
 
Kwa hili la Wasiojulikana, inabidi uwe na akili za mwendawazimu kudhani kwamba serikali haikuwa inasema ukweli juu yake. Na amini nawaambieni, kuwapo kwa Wasiojulikana na amri zilizotolewa kwao ni jambo ambalo linaweza kuwafikisha viongozi mahakama za kimataifa. Kwa sababu hiyo, upinzani hauwwezi kuachiwa uchukue madaraka 2020 kwa hali yoyote ile, kwa kuwa Upinzani wakichukua nchi jambo la kwanza kufanya itakuwa ni kupata undani wa Wasiojulikana - nani alikianzisha, nani alikisimamia, nani alitoa amri, waliotekwa wako, waliouwawa walizikwa wapi. Fikiria nani atakuwa tayari kuruhusu mazingira ya majibu kwa maswali hayo? Atakuwa tayari kufanya lolote ili mazingira ya ukweli yasipatikane.

Nakuunga mkono kwa maelezo haya, hii ndio maana chaguzi zinanajisiwa na hata zisipofanyika hao wafanya maovu hawajali ili miradi wanaendelea kukaa madarakani, maana usalama wao upo tu kama wataendelea kuwepo madarakani. Hivyo hilo kundi la watu wasiojulikana halijafa kabisa bali lengo lako la kuwatia wananchi woga limefanikiwa kwa kiwango fulani. Ikitokea tu wananchi wanaanza kuhoji kwa uwazi mambo ya serikali, hilo kundi litarudi tena kazini, na wahanga watakuwa vinara wa kuhoji.
 
Miaka kama miwili iliyopita kasi za kikundi cha "Wasiojulikana" ilikuwa ya juu ajabu. Kulikuwa na tetesi nyingi kuhusu nani hasa walikuwa nyuma ya hiki kikundi, na mengi sana yalisemwa.

Kwa wengi ilikuwa ni vigumu kuamini kuwa kikundi cha "Wasiojulikana" kilikuwa hakina uhusiano na serikali kwa lojiki kwamba wale waliotekwa au kuuwawa walikuwa (victims) na "Wasiojulikana" ni wale tu walioonekana kuikosoa serikali au viongozi wa serikali, na hata Rais Magufuli. Kwa maneno mengine, ilionwa wazi kwamba uwepo wa kikundi cha "Wasiojulikana" ulikuwa kwa manufaa ya serikali iliyopo madarakani.

Na pia watu walihoji uwezo wa kifedha na ujipangaji wa kikosi hiki, ambao ni wazi haukuwa wa kikundi kisicho na mafunzo au kuwa na chanzo kikubwa cha fedha. Kwa mfano, gari aina ya Nissan Patrol mpya inayosemekana kutumika katika tukio mojawapo la "Wasijulikana" linasemakana kuchomwa moto ili kupoteza ushahidi.

Na ajabu ni kwamba mara zote matukio ya "Wasiojulikana" yalipotokea, Polisi walionekana kujiumauma katika kutoa majibu au kufanya upelelezi. Hadi leo hii, hakuna kesi hata moja inayohusu "Wasiojulikana" ambapo wahusika walikamatwa na kuhukumiwa.

Lakini sasa kikundi hiki cha "Wasiojulikana" ni kama kimepunguza kasi yake. Sintadiriki kusema kimefutwa au kukoma kuwapo. Je, ni kwa kuwa watu wameelewa kwamba katika awamu hii ukiikosoa serikali au watawala "utapotezewa" na "Wasiojulikana" ambao ni wazi wanafanya "uhalifu" kwa namna ya kuinufaisha serikali iliyopo madarakani dhidi ya kukosolewa na kutuhumiwa, huku serikali hiyo ikikana kuwafahamu au kuhusika nao. Inawezekana kuna mtu au watu wenye busara waliongea neno la hekima na "Wasiojulikana" wakawekwa gavana, kwa kuwa kuna wakati walifanya vitendo vyao kwa namna ya kuelekea kuwa kama enzi za "State Research Bureau" ya enzi ya Idd Amin wa Uganda, kikosi cha intelijensia kilichoteka na kuua yeyote aliyemkosoa Idd Amin na serikali yake.

Je, kuna siku ukweli kuhusu "Wasiojulikana" utajulikana?
Na DAB naye siku hizi yupo kimyaa... sijui ni coincidence au ndo hao hao..!!
 
Nadhani Watanzania tumefikia hapo. Tutafanywa lolote na viongozi wetu na kutulia tuli. Nyerere alikosea kusema kwamba Watanzania hawatavumilia kuona viongozi wachache wakiwanyima haki zao. Hakujua kuwa Watanzania sio Watunisia.

Mkuu tufanywe hivyo mara mbili? Kama uchaguzi mkubwa wa serikali za mitaa umetoa viongozi wasio na uhalali wa umma na inaonekana ni sawa, hapo unategemea nini?
 
Miaka kama miwili iliyopita kasi za kikundi cha "Wasiojulikana" ilikuwa ya juu ajabu. Kulikuwa na tetesi nyingi kuhusu nani hasa walikuwa nyuma ya hiki kikundi, na mengi sana yalisemwa.

Kwa wengi ilikuwa ni vigumu kuamini kuwa kikundi cha "Wasiojulikana" kilikuwa hakina uhusiano na serikali kwa lojiki kwamba wale waliotekwa au kuuwawa walikuwa (victims) na "Wasiojulikana" ni wale tu walioonekana kuikosoa serikali au viongozi wa serikali, na hata Rais Magufuli. Kwa maneno mengine, ilionwa wazi kwamba uwepo wa kikundi cha "Wasiojulikana" ulikuwa kwa manufaa ya serikali iliyopo madarakani.

Na pia watu walihoji uwezo wa kifedha na ujipangaji wa kikosi hiki, ambao ni wazi haukuwa wa kikundi kisicho na mafunzo au kuwa na chanzo kikubwa cha fedha. Kwa mfano, gari aina ya Nissan Patrol mpya inayosemekana kutumika katika tukio mojawapo la "Wasijulikana" linasemakana kuchomwa moto ili kupoteza ushahidi.

Na ajabu ni kwamba mara zote matukio ya "Wasiojulikana" yalipotokea, Polisi walionekana kujiumauma katika kutoa majibu au kufanya upelelezi. Hadi leo hii, hakuna kesi hata moja inayohusu "Wasiojulikana" ambapo wahusika walikamatwa na kuhukumiwa.

Lakini sasa kikundi hiki cha "Wasiojulikana" ni kama kimepunguza kasi yake. Sintadiriki kusema kimefutwa au kukoma kuwapo. Je, ni kwa kuwa watu wameelewa kwamba katika awamu hii ukiikosoa serikali au watawala "utapotezewa" na "Wasiojulikana" ambao ni wazi wanafanya "uhalifu" kwa namna ya kuinufaisha serikali iliyopo madarakani dhidi ya kukosolewa na kutuhumiwa, huku serikali hiyo ikikana kuwafahamu au kuhusika nao. Inawezekana kuna mtu au watu wenye busara waliongea neno la hekima na "Wasiojulikana" wakawekwa gavana, kwa kuwa kuna wakati walifanya vitendo vyao kwa namna ya kuelekea kuwa kama enzi za "State Research Bureau" ya enzi ya Idd Amin wa Uganda, kikosi cha intelijensia kilichoteka na kuua yeyote aliyemkosoa Idd Amin na serikali yake.

Je, kuna siku ukweli kuhusu "Wasiojulikana" utajulikana?
Wanajulikana ila wanaowajua hawakuguswa ndiomaana ikawa kweli hawajulikani.

Kumbuka:-
1. Juma Ighondu baada ya kufanya mipango iliyofeli ya kumuua Dr Ulimboka, ametoweka mpaka leo hayupo Tanzania.
2. Aliye mnyoshea siraha Waziri Nape Yuko Wete Pemba, watu wamemuona huko Sasa anaishi maisha ya kujifichaficha
3. Waliompiga risasi Tundu Lisu, msimamizi wao anagombano na baadhi ya wakuu wa wilaya mkoani kwake hapakaliki

Kifupi nchi hii ni yetu tunawajua wote ila hawajatoa betri sehemu yenye mizizi

Ahsante Sana Chief

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Miaka kama miwili iliyopita kasi za kikundi cha "Wasiojulikana" ilikuwa ya juu ajabu. Kulikuwa na tetesi nyingi kuhusu nani hasa walikuwa nyuma ya hiki kikundi, na mengi sana yalisemwa.

Kwa wengi ilikuwa ni vigumu kuamini kuwa kikundi cha "Wasiojulikana" kilikuwa hakina uhusiano na serikali kwa lojiki kwamba wale waliotekwa au kuuwawa walikuwa (victims) na "Wasiojulikana" ni wale tu walioonekana kuikosoa serikali au viongozi wa serikali, na hata Rais Magufuli. Kwa maneno mengine, ilionwa wazi kwamba uwepo wa kikundi cha "Wasiojulikana" ulikuwa kwa manufaa ya serikali iliyopo madarakani.

Na pia watu walihoji uwezo wa kifedha na ujipangaji wa kikosi hiki, ambao ni wazi haukuwa wa kikundi kisicho na mafunzo au kuwa na chanzo kikubwa cha fedha. Kwa mfano, gari aina ya Nissan Patrol mpya inayosemekana kutumika katika tukio mojawapo la "Wasijulikana" linasemakana kuchomwa moto ili kupoteza ushahidi.

Na ajabu ni kwamba mara zote matukio ya "Wasiojulikana" yalipotokea, Polisi walionekana kujiumauma katika kutoa majibu au kufanya upelelezi. Hadi leo hii, hakuna kesi hata moja inayohusu "Wasiojulikana" ambapo wahusika walikamatwa na kuhukumiwa.

Lakini sasa kikundi hiki cha "Wasiojulikana" ni kama kimepunguza kasi yake. Sintadiriki kusema kimefutwa au kukoma kuwapo. Je, ni kwa kuwa watu wameelewa kwamba katika awamu hii ukiikosoa serikali au watawala "utapotezewa" na "Wasiojulikana" ambao ni wazi wanafanya "uhalifu" kwa namna ya kuinufaisha serikali iliyopo madarakani dhidi ya kukosolewa na kutuhumiwa, huku serikali hiyo ikikana kuwafahamu au kuhusika nao. Inawezekana kuna mtu au watu wenye busara waliongea neno la hekima na "Wasiojulikana" wakawekwa gavana, kwa kuwa kuna wakati walifanya vitendo vyao kwa namna ya kuelekea kuwa kama enzi za "State Research Bureau" ya enzi ya Idd Amin wa Uganda, kikosi cha intelijensia kilichoteka na kuua yeyote aliyemkosoa Idd Amin na serikali yake.

Je, kuna siku ukweli kuhusu "Wasiojulikana" utajulikana?
Mbona ekweli na ushahidi uko wazi. Ni usalama wa taifa nje ya usalama wa taifa chini ya kiongozi mwenye baraka za magogoni asiye kuwa na akili kwa maamuzi na maslahi ya mgonjwa wa akili.
 
.Kwa wengi ilikuwa ni vigumu kuamini kuwa kikundi cha "Wasiojulikana" kilikuwa hakina uhusiano na serikali
.
Na ajabu ni kwamba mara zote matukio ya "Wasiojulikana" yalipotokea, Polisi walionekana kujiumauma katika kutoa majibu au kufanya upelelezi. Hadi leo hii, hakuna kesi hata moja inayohusu "Wasiojulikana" ambapo wahusika walikamatwa na kuhukumiwa.

Je, kuna siku ukweli kuhusu "Wasiojulikana" utajulikana?
Mkuu Synthesizer , kumbe tulikuwa tunaionea serikali yetu bure, kwa kuihisi ni serikali inahusika na wasiojulikana hawa, kumbe...
P
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom