Wasio na vitambulisho marufuku kupiga kura Arumeru-NEC

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Tume ya Taifa ya uchaguzi imekataa maombi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CDM) ya kuitaka tume hiyo kuruhusu watu waliopoteza vitambulisho vya kupiga kura wajaze FORM NO 17 kisha waruhusiwe kupiga kura katika uchaguzi wa ubunge Arumeru Mashariki.Hii ni kutokana na ukweli kuwa wananchi wengi hasa vijana wa CDM wamepoteza vitambulisho vya kupiga kura na hivyo kukosa uhalali wa kupiga kura.

Haijajulikana ni kwa nini tume ya uchaguzi imekataa kuruhusu Form hizo kutumika kwani sheria ya uchaguzi inaruhusu kufanya hivyo kwa yeyote aliyepoteza kitambulisho cha kupigia kura.

My Take:Kwa tamko hili la NEC kuna hatari watu wanaonunua shahada za kupiga kura kutoka kwa wananchi watazidisha kasi yao kwani wanafahamu sasa tume ya uchaguzi imepiga marufuku matumizi ya FORM NO 17

Source:Nipashe
 
Tume ya taifa ya uchaguzi Inafanya kazi zake kwashinikizo la chama tawala Ili kulinda maslai yao"wao ndio mabingwa wakununua shahada kwa wananchi maskini...viongozi wa chadema onyesheni msimamo wenu kuhusu FORM NO 17 kwani upatikanaji wake UTAWAKOMESHA WANAO NUNUA SHAHADA.
 
Kinachotakiwa nchi hii ni machafuko tu kama yaliyotokea Kenya ama Rwanda kwani kuanzia hapo baada ya mazara yatakayojitokeza ndio sheria zitaanza kufuatwa. Vinginevyo tutabaki tunalalamika. Vijana bila kumwaga damu hakuna mabadiliko nchi hii.
 
Utaribu wa kuwa na F 17 unaelweka na unapaswa kufuatwa. Lakini kutokana na utunzaji wa record ulivyo manually na kwa asilimia flani tabia ya watu wetu ya ujanja ujanja na kutokuwa wakweli, mda uliopo hautoshi ku update records.
 
Tatizo la CDM wafuasi wao wengi hawana vitambulisho vya kupigia kura, wakati wenzao CCM wameviweka, sasa hapa CDM imeishapigwa bao la kisigino.
 
Kinachotakiwa nchi hii ni machafuko tu kama yaliyotokea Kenya ama Rwanda kwani kuanzia hapo baada ya mazara yatakayojitokeza ndio sheria zitaanza kufuatwa. Vinginevyo tutabaki tunalalamika. Vijana bila kumwaga damu hakuna mabadiliko nchi hii.

Dunia yako chaguo lako ukiamua kuvuta bange na kunywa gongo ndiyo maisha yako.
 
Hiyo fomu no 17 sheria inataka itumike kama haitotumika sasa wanataraji itumike lini? Sheria haiko kama mapambo na iwapo kila siku kuna wimbo kwamba nchi inaongozwa kwa kufuata utawala wa sheria ni lizima ionekane sheria inafanya kazi na si vinginevyo. Viongozi wa CDM hakikisheni mnawataka wananchi wote waliopoteza kadi za mpiga kura waende vituoni siku ya kupiga kura na waombe fomu no 17. Nani asiyejua maisha ya kimaskini ya watanzania hadi kufikia kushindwa kutunza vitu kama hivyo kwa usahihi. Kwa mfano hapo ni wangapi hawana vyeti vya kuzaliwa na bado wanatambulika kama watanzania. Sheria itafuatwa vinginevyo uchaguzi utakuwa ni batili. Huyo Sioi mbona hajaukana uraia wa Kenya na bado amepitishwa kimizengwe. CCM na tume msiingize nchi yetu kwenye machafuko.
 
Watu wakisema Tume ya uchaguzi ina chochea machafuko nchini wanaonekana wa'ahaini'. Hivi tume ina mamlaka ya kufuta sheria iliyotungwa na kukubalika na Bungeni kisha Rais kuikubali itumike ?
 
chadema walitaka kupeleka vijana wa arusha kupiga kura arumeru.

ukipoteza kitambulisho imetoka hawajali wewe chadema au ccm. magwanda kulalamika ndio wenyewe hawajiamini.
 
madaktari wakigoma wanaropoka hawajafuata sheria na wananchi wanadanganyika. Hii nchi haina sheria,inapelekwa tu kwa hisia za wachache. Sheria ya uraia wameshaikataa, kwa bashe ilitumika hiyo hiyo. Sheria ya gharama za uchaguzi ndo usiseme, na hii nayo wameikataa kwani haina maslahi kwao. Wamegundua hilo ni eneo lenye vijana wengi hivyo watakosa kura. Hii nchi ni bora tuingie vitani ili wengine tupunguze kiwingu. NI BORA TUSHIKISHANE ADABU KAMA KENYA. Huu ujinga tumeuchoka! Tuingize nchi vitani kuna vitu baada ya hapo vitanyooka.
 
Jiulize kwanini hao vijana wengi wa Chadema wapoteze vitambulisho vyao? Ni irresponsility au ndio propaganda zimeanza mwisho muitumie hii kama excuse?
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) haina interest ya kuona Watanzania wengi zaidi, wenye sifa ya kupiga kura wanapiga kura. Ni kwa sababu malengo ya kazi yao si kuhakikisha kuwa Watanzania wanachagua viongozi wao kwa uhuru na haki bali kuhakikisha CCM inabaki madarakani. Kubadili tabia hii kunawezekana tu kama tutapata Katiba mpya ambapo Tume hii itachaguliwa kwa mujibu wa Katiba hiyo na itawekewa malengo ya kazi chini ya Katiba hiyo. Napendekeza yafuatayo:

Tume iwekewe lengo la kuongeza idadi ya wanaopiga kura katika kila chaguzi (kama TRA na kodi). Ni lazima kuwe na ongezeko la wanaopiga kura kwa sababu idadi ya watu inaongezeka. Idadi ya wapiga kura ikishuka tu, ama wapunguziwe mishahara au watimuliwe kabisa kwa kushindwa kutimiza malengo. Kwa Arumeru Mashariki, kwa mfano, waliojiandikisha kupiga kura ni 150,000. Waliopiga kura uchaguzi uliopita ni 60,000. Uchaguzi huu mdogo ni lazima watu si chini ya 100,000 wapige kura. Chini ya hapo Tume imeshindwa kutimiza lengo.

Iwe ni jukumu la Tume kuhakikisha watu wengi zaidi wanashiriki katika kuamua hatma ya nchi yao. Hatuwezi kuendelea kuwa na watu wanaolipwa mishahara lakini malengo ya kazi zao hayaewekwi wazi. Mijitu inaamka kila siku asubuhi kwenda na kurudi kazini lakini ukimsimamisha barabarani muulize nini malengo ya kazi yako, hajui. Ndio Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
 
Its too late, kweli sasa nimeamini Chadema imeenda Arumeru kujenga chama, ikitoka hapo inahamia bububu.
 
madaktari wakigoma wanaropoka hawajafuata sheria na wananchi wanadanganyika. Hii nchi haina sheria,inapelekwa tu kwa hisia za wachache. Sheria ya uraia wameshaikataa, kwa bashe ilitumika hiyo hiyo. Sheria ya gharama za uchaguzi ndo usiseme, na hii nayo wameikataa kwani haina maslahi kwao. Wamegundua hilo ni eneo lenye vijana wengi hivyo watakosa kura. Hii nchi ni bora tuingie vitani ili wengine tupunguze kiwingu. NI BORA TUSHIKISHANE ADABU KAMA KENYA. Huu ujinga tumeuchoka! Tuingize nchi vitani kuna vitu baada ya hapo vitanyooka.
Ni kweli kabisa, hata Yesu alikufa msalabani ndio wengine wakakombolewa
 
Back
Top Bottom