Wasindikizaji wa msafara wa Lema watawanywa na Polisi mkoani Manyara

Kila jambo lina wakati,wakati wa magamba kukwanguliwa umefika.Wasifikiri Mh G Lema yupo pekee yake!amebeba ujumbe mzito nyuma ya pazi.Ujumbe huo ni kilio cha wanyonge.hata ikitokea akatangulia mbele ya haki athari atayoiacha ni pigo kubwa kwa wanan wa magamba na madhalimu wote katika nchi hii.Fikra mgando hazina mashiko mbele ya jamii iliyodharauliwa na kupuuzwa na kikundi cha watu wachache wenye kuitumia taasisi hii ya uaris vibaya.Ikulu si mahali pa kucheka cheka na kukaribisha washoga.Ikulu ni mahali patakatifu.ukitaka kwenda ikulu uwe na uthubutu wa kuwaambia watoto wako kuwa urais wangu si wa familia yangu,dhamana niliyopewa na Watanzania si dhamana ya kujilimbikizia mali na kuwapachika watoto wa shangazi,mashemeji na nyumba ndogo.Ikulu si sehemu ya kulipiza kisasi kisa waziri mkuu wako kaambiwa muongo.Ukiweza kuwaambia watoto wako na mkeo hivyo basi hata wale matapeli hawatathubutu kukusogelea na kukuletea dili za kuiangamiza nchi

Mwisho,mwacheni G.Lema afanye kazi yake,anatumwa na dhamira iliyojaa uzalendo na mapenzi kwa wananchi na taifa lake.Interejensia itumike vizuri kuwakamata Al shabab na siyo kudhibiti demokrasia nchini.Lema ni mtu mdogo sana ila mwenye dhamira ya kweli kwa ukombozi wa kifikra toka mikono dhalimu ya wakoloni weusi.Wamepita wanaharakati wengi kama Che Guevera na wenzake,harakati zao zilipingwa na madhalimu wote wenye lengo baya lakini athari yake imesimama miongo kwa miongo.Matunda ya kina Che Guevera ni mazalia mapya ya chimbuko la kina Lema.Atapita Lema impact atayoiacha ni kubwa kuliko nguvu zinazotumika kuzima fikra pevu za wanaharakati wachepuao.viva Lema viva.Aluta Continua mapambano ndo kwanza yanashika kasi
 
kitendo cha kufanya mikutano ya hadhara bila kibali tayari ni uvunjaji wa sheria! Anafikiri yeye ni nani? Ndio maana nimesema atakuwa na matatizo. Kama mbunge ingetakiwa yeye ndiye awe mstari wa mbele kupigania utawala bora wa sheria.

Sio kila kitu lazima tukizungumzie kisiasa. Watu wanaenda kusalimia kijijini kwao kundi la watu linawalaki ije kuwa hii ya Lema? It is simple: Ulikuwa unasafiri`, ukakutana na watu wakataka kukusalimia, wengine waliopo karibu walivyoona wenzao wanakusalimu na wao nao wakaja (kundi likazidi kuongezeka) je huo ni mkutano bila kibali? Je kwavile wewe ni mwanasiasa unatakiwa uwafukuze? Kama mambo ndio hayo mbona xmas hii mtakamata wengi mno; labda hao viongozi usafiri wao uwe wa angani peke yake. Just think loud!!
 
Uko uhuru wa maoni. Kama kwa assessment yako mtu fulani ni MJINGA, basi una haki ya kutoa hayo maoni na kusema ni mjinga. Kama Lema amesema Mkuu wa Mkoa wa Arusha ni MJINGA, hiyo ni haki yake ya kimsingi. Freedom of opinion.

Tumefika mahali ambapo mwanasiasa anahitaji kibali cha polisi ndipo asalimiane na wananchi?
 
kitendo cha kufanya mikutano ya hadhara bila kibali tayari ni uvunjaji wa sheria! Anafikiri yeye ni nani? Ndio maana nimesema atakuwa na matatizo. Kama mbunge ingetakiwa yeye ndiye awe mstari wa mbele kupigania utawala bora wa sheria.

Mkutano wa hadhara. Kusalimia watu. Kuongea na watu. Freedom of speech. Haki za binadamu. Uzalendo. Akili za kawaida. Ujasiri. Tatizo liko wapi?
 
Something is wrong with this guy
am with you, why only him?ifike sasa tuache kumtetea this guy is full of bullshit...nahisi amelewa sifa, kuwa mbunge hakukupi PASSPRORT ya kufanya unavyotaka, lazima uwe mfano ila kwa huyu Mhe sijajifunza lolote la maana toka achaguliwe....Trouble maker.
 
am with you, why only him?ifike sasa tuache kumtetea this guy is full of bullshit...nahisi amelewa sifa, kuwa mbunge hakukupi PASSPRORT ya kufanya unavyotaka, lazima uwe mfano ila kwa huyu Mhe sijajifunza lolote la maana toka achaguliwe....Trouble maker.

Id yako inajieleza jinsi ulivyo
 
Jamani kwani kamanda wetu G LEMA hawezi akapapewa kibari cha miezi 6 hili haepukane na mitego hii ya magamba .nyie ccmpolisi LEMA kipenzi cha watu hata mfanyaje pipo pawa haizuiriki ni kama maji ya mto yaliyopasua kingo zake magamba ziiiiiiii...
 
Hiyo yote ni uthibitisho wa kwamba katiba ya sasa haikidhi uhuru kamili wa Mtanzania, maana badala ya kusema ni haki mtu kuandamana au kukusanyika wanaanza na maneno " kama haitaathiri", Mambo yanaendeshwa utafikiri tuko miaka ya hamsini chini ya sheria za mkoloni
 
am with you, why only him?ifike sasa tuache kumtetea this guy is full of bullshit...nahisi amelewa sifa, kuwa mbunge hakukupi PASSPRORT ya kufanya unavyotaka, lazima uwe mfano ila kwa huyu Mhe sijajifunza lolote la maana toka achaguliwe....Trouble maker.
hapa sasa tunaenda sambamba..tungekuwa watu 10 wenye mawazo kama haya, huyu jamaa angebadilika. Angeacha kulewa na sifa za kijijnga anazopambwa nazo.
Hebu wananchi wa Arusha watueleze, kwa mwaka wote huu wa ubunge wake, Lema amewafanyia nini?
 
Hata Raisi wa Awamu ya kwanza baada ya fikra zake za kuacha uaalimu na kuamua kujiweka kitanzi kwa kudai uhruru kila alipopita watanganyika walimtaka jabo aseme neno juu ya ukombozi: sasa ni zamu ya mkuu wa nchi kumzuia pindi Mheshimiwa Lema atakapo pita eneo la ikulu Dar
Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Mh. Godbless Lema alizuiliwa na madereva wa boda boda ya piki piki za biashara akitokea Arusha kuelekea Dodoma kwenye kikao cha Bunge.

Wafanyabiashara hawo walimzuia Lema nakutaka angalau neno lake moja kwaajili ya unyanyaswaji wanao upata kutoka kwa jeshi la police, Lema alisimama na kuongea nao kwa dakika kumi na sita kisha akaongozana nao mpaka kwenye ofisi za chama (Chadema)na kuwapatia bendera za chama kwaajili ya kueneza chama.
Baada ya Lema kuondoka katika maeneo hayo na sasa yupo mjini Dodoma wafanyabiashara hawo wamekamatwa na jeshi la Police kwa kupeperusha bendera za Chadema. Kuna uvumi unasema Lema amekamatwa huu ni uongo mkubwa sana Lema haja kamatwa na tayari kaingia mjini dodoma.

Kuhusu jeshi la police:
Huu ni uonevu wa hali ya juu sana kuzuia watu wasiwasilishi hisia zao pale wanapo ona ni muda muafaka wa kufanya hivyo, tunalaani vikali ukandamizwa huu wa kipuuzi mno na hata mjinga hawezi kuufanya na sijui nitoe jina gani litakaloweza kusimama badala ya mjinga, mungu awatie moyo wa ujasiri wale wote waliyopata misuko suko hii, safari bado ni ndefu na nilazima tusonge na tufike.j
 
Siku zote nchi hii haipendi watetezi... Lema ndiye mtetezi wa watanzania 42 milioni kwenye kipato duni....

Tuko naye na tunapambana hadi kieleweke.... hukusu huyo anayesema something is wrong with lema... let me set the record straight with you... We don't fear you and we don't need your comment nor your support.... and for your information this battle will be won come 2015...
 
sasa lipi la kweli hapo?
Hebu tupeni source ya taarifa hizi: Lema amekamatwa au hajakamatwa? Waboda boda wamekamatwa au hawajakamatwa?
Jamani which is which?
 
Kwani kumtaja mtu kwa Tabia yake ambayo ni kweli anayo ni kosa???
Tuseme kama mtu ni mlevi ukawa unawadithia wenzako na kumtaja huyo jamaa kua ni mlevi ni kosa???!!!
Ingekua kasingiziwa hapo sawa!!!
 
Kwani kumtaja mtu kwa Tabia yake ambayo ni kweli anayo ni kosa???
Tuseme kama mtu ni mlevi ukawa unawadithia wenzako na kumtaja huyo jamaa kua ni mlevi ni kosa???!!!
Ingekua kasingiziwa hapo sawa!!!
Shark hebu fafanua kidogo, ina maana unataka kuhalalisha Lema kumwita RC mjinga?
 
Back
Top Bottom