Shine
JF-Expert Member
- Feb 5, 2011
- 11,481
- 1,364
Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Mh. Godbless Lema alizuiliwa na madereva wa boda boda ya piki piki za biashara akitokea Arusha kuelekea Dodoma kwenye kikao cha Bunge.
Wafanyabiashara hawo walimzuia Lema nakutaka angalau neno lake moja kwaajili ya unyanyaswaji wanao upata kutoka kwa jeshi la police, Lema alisimama na kuongea nao kwa dakika kumi na sita kisha akaongozana nao mpaka kwenye ofisi za chama (Chadema)na kuwapatia bendera za chama kwaajili ya kueneza chama.
Baada ya Lema kuondoka katika maeneo hayo na sasa yupo mjini Dodoma wafanyabiashara hawo wamekamatwa na jeshi la Police kwa kupeperusha bendera za Chadema. Kuna uvumi unasema Lema amekamatwa huu ni uongo mkubwa sana Lema haja kamatwa na tayari kaingia mjini dodoma.
Kuhusu jeshi la police:
Huu ni uonevu wa hali ya juu sana kuzuia watu wasiwasilishi hisia zao pale wanapo ona ni muda muafaka wa kufanya hivyo, tunalaani vikali ukandamizwa huu wa kipuuzi mno na hata mjinga hawezi kuufanya na sijui nitoe jina gani litakaloweza kusimama badala ya mjinga, mungu awatie moyo wa ujasiri wale wote waliyopata misuko suko hii, safari bado ni ndefu na nilazima tusonge na tufike.
Mateso yakizidi ujue ndo neema inakaribia wanachadema tusikate tamaa kwani haya mambo yana mwisho