uvivumwiko
Member
- Mar 22, 2010
- 20
- 1
Wengi wa Wasimamizi na makarani wa vituo vya kupigia kura Jimbo la MONDULI kwa uchaguzi utakaofanyika 31/10/2010 ni wahitimu wa darasa la saba. Ni ukweli dhahiri kuwa mhitimu wadarasa la saba hana uelewa wa kutosha kumwezesha kuwa msimamizi wa kituo cha kupigia kura. Madhara ninayofikiri kuwa yatasababishwa na watu hawa ni :
- kuchelewesha wapiga kura kupiga kura
- kutofuata sheria na kanuni za uchaguzi ipasavyo
- kudanganyika kwa urahisi na kusababisha kutolewa matokeo yasiyo sahihi