Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Wadau – kuna masuala yananitatiza hapa kuhusu hawa wasimamizi wa uchaguzi ambao tunaambiwa ni wafanyakazi wa Tume ya Uchaguzi (NEC) kwa hivyo wako huru. Lakini pia tunajua hawa ni watumishi wa umma yaani wakurugenzi wa wilaya (ma-DED) walioteuliwa na serikali ya CCM katika nyadhifa hizo.
Maswali yangu - na mkazo nimeweka katika suali la mwisho:
1. NEC yenyewe ina mamlaka kiasi gani katika maamuzi ya kutwateua hawa au katika kuwahamisha vituo? Yaani NEC huwa inashirikishwa katika maamuzi hayo?
2. Hivi wapo hawa ma-DED ambao ni wa vyama vya upinzani yaani CUF au Chadema?
3. Nakumbuka katika uchaguzi wa 2005 kuna msimamizi mmoja wa NEC mkoani Tanga ambaye alikuwa DED aliondolewa katika kazi hiyo ya usiomamizi wa uchaguzi kwa sababu alikuwa waziwazi anamshabikia mgombea wa CCM. Hiyo hatua ilikuwa sawa – lakini jee, yule mbadala aliyeteuliwa, NEC ilishirikishwa?
4. Mwaka huu CCM imevunja rekodi kwa wagombea wake wa Ubunge kupita bila kupingwa na kati ya hao kuna baadhi wameenguliwa kutokana na pingamizi zilizowekwa na wagombea wa CCM ambazo zilikubaliwa na hawa ma-DED na zile za wapinzani kutupwa (isipokuwa moja ya Mbowe). Jee hii haitii wasiwasi ya maamuzi ya hawa ma-DEd ambao ni makada wa CCM?
5. Katika jimbo la Nyamagana ambako pingamizi la mgombea wa CCM – Lawrence Masha (ambaye ni waziri wa Mambo ya Ndani) lilikubaliwa kwamba yule mpinzani wake wa Chadema siyo raia wa Tanzania. Jee, Msimamizi wa uchaguzi ana mamlaka ya kuamua (baada ya kupata vielelezo) kwamba fulani ni raia au la? Haya mamlaka kayapata wapi? Navyofahamu mimi mamlaka ya masuala ya uraia panapokuwa na utata ni mahakama. Isitoshe, tusisdahau hapa kwamba Masha ni Waziri ambaye Idara ya Uhamiaji iko chini yake. Kweli haki imeonekana kutendeka, achilia mbali iwapo imetendeka?
Maswali yangu - na mkazo nimeweka katika suali la mwisho:
1. NEC yenyewe ina mamlaka kiasi gani katika maamuzi ya kutwateua hawa au katika kuwahamisha vituo? Yaani NEC huwa inashirikishwa katika maamuzi hayo?
2. Hivi wapo hawa ma-DED ambao ni wa vyama vya upinzani yaani CUF au Chadema?
3. Nakumbuka katika uchaguzi wa 2005 kuna msimamizi mmoja wa NEC mkoani Tanga ambaye alikuwa DED aliondolewa katika kazi hiyo ya usiomamizi wa uchaguzi kwa sababu alikuwa waziwazi anamshabikia mgombea wa CCM. Hiyo hatua ilikuwa sawa – lakini jee, yule mbadala aliyeteuliwa, NEC ilishirikishwa?
4. Mwaka huu CCM imevunja rekodi kwa wagombea wake wa Ubunge kupita bila kupingwa na kati ya hao kuna baadhi wameenguliwa kutokana na pingamizi zilizowekwa na wagombea wa CCM ambazo zilikubaliwa na hawa ma-DED na zile za wapinzani kutupwa (isipokuwa moja ya Mbowe). Jee hii haitii wasiwasi ya maamuzi ya hawa ma-DEd ambao ni makada wa CCM?
5. Katika jimbo la Nyamagana ambako pingamizi la mgombea wa CCM – Lawrence Masha (ambaye ni waziri wa Mambo ya Ndani) lilikubaliwa kwamba yule mpinzani wake wa Chadema siyo raia wa Tanzania. Jee, Msimamizi wa uchaguzi ana mamlaka ya kuamua (baada ya kupata vielelezo) kwamba fulani ni raia au la? Haya mamlaka kayapata wapi? Navyofahamu mimi mamlaka ya masuala ya uraia panapokuwa na utata ni mahakama. Isitoshe, tusisdahau hapa kwamba Masha ni Waziri ambaye Idara ya Uhamiaji iko chini yake. Kweli haki imeonekana kutendeka, achilia mbali iwapo imetendeka?