Michelle
JF-Expert Member
- Nov 16, 2010
- 7,621
- 3,513
Asante Michelle. nakubali kwamba Lema is a talented leader, visionary, and very determined. he feels the people and delivers for them. Nimefurahi kwamba anajiendeleza kielimu kwa kiwango hicho, najua wabunge kadhaa wa bunge lililopita ambao walisoma baada ya kuwa wabunge na sasa baadhi wanaendelea na ubunge.
mambo mawili naomba umshauri.
1. muombe ajaribu kutumia zaidi kiswahil anapoongea mbele za watu kwani huwa anapotumia tu maneno ya kiingereza katika mazungumzo yake anavunja kweli kweli. Ingawa ujumbe unafika, lakini sasa huwa anawapa watu nafasi ya kuanza kujiuliza maswali baadaye.
2. mwambie asiwatukane polisi. hili ni muhimu zaidi, kwamba polisi wa kawaida arusha ni wapenzi sana wa chadema lakini wana kisasi na Lema kutokana na kuwarushia maneno mabaya anapohemshwa na machalii. akifanikiwa kurudisha urafiki na polisi watamsaidia sana sana kwani hawapendi chadema ihujumiwe.
Nimemwambia na pengine naye atasoma hilo baadaye, nafurahi pia unaelewa kwamba wakati mwingine ana-behave kutokana na pressure za wananchi wake,ni ngumu sana kwake kutumia hekima yake.Natumai kabisa Mungu atamzidishia hekima na akitulia atatengeneza uhusiano wake na polisi.Asante sana Gurudumu.