Donatila
JF-Expert Member
- Oct 23, 2014
- 7,557
- 21,512
Mahakama kuu ya Tanzania imeridhia dhamana kwa washitakiwa watatu wa mamlaka ya mapato Tanzania TRA wanaokabiliwa na mashitaka ya kutoa makontena 329 bandarini bila kulipiwa kodi na kuisababishia serikali hasara ya shilingi bilioni 12.7.
Maamuzi hayo ya mahakama kuu ya Tanzania yametokana na ombi lililowakilishwa mahakamani hapo na washtakiwa watatu wakiongozwa aliyekuwa Kamishina wa Forodha wa TRA Bw Tiagi Masamaki.
Jaji wa mahakama hiyo Bi Wilfrida Koroso, alisema dhamana kwa washitakiwa hao watatu iko wazi kama watatimiza masharti sita yakiwemo ya kulipa hundi ya shilingi bilioni 2.6 kila mmoja huku pia wakitakiwa kuwasilisha hati zao za kusafiri na kutakiwa kuwa na wadhamini watakaokuwa na uwezo wa kusaini hundi ya shilingi milioni 20 kila mmoja.
Mshitakiwa namba moja katika kesi ya kuhujumu uchumi, aliyekuwa Naibu Kamishna wa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA), Tiagi Masamaki (Kulia) akiwa na wenzake aliyekuwa Meneja wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja, Habibu Mponezya na Bulton Mponezya wakiwa katika Mahakama Kuu Tanzania jijini Dar es Salaam jana wakisomewa shtaka linalowakikabili la makosa ya jinai na uhujumu uchumi.
Chanzo: mpekuzihuru.com