technically
JF-Expert Member
- Jul 3, 2016
- 11,975
- 48,843
Washauri wa Rais popote mlipo iwe Dar, Dodoma au Chato, Naomba mshaurini Rais wetu mpendwa anyamaze mpaka corona ipite, Ninapoona speech za rais ambazo zinaacha maswali mengi na washauri ndio wanaonekana ni tatizo kwa kumshauri vibaya Rais wetu so please Mwambieni ukweli anyamaze kuna mambo anaongea yanamshushia heshima kweli.
Najua Rais ni taasisi kama mnamshauri anakataa bora mjiuzulu hamna kazi mnayofanya hebu angalieni effect za speech zake kwenye vyombo vya habari ya kimataifa kama BBC, VOA etc. na madhara ya speech zake kule WHO.
Atulie tu kwani anakosa nini kule Chato anyamaze janga la Corona litapita then tutarejea kwenye maisha ya kawaida kunyamaza kimya ni bora kuliko kuongea mambo yanayoacha maswali mengi zaidi ya majibu.
Rais kauli zake zina nguvu sana ndio maana unaona zinafuatiliwa sio tu Tanzania zaidi nje ya nchi clip zake zinazunguka zikiwa zimefanyiwa tafsiri ya lugha mbali mbali.
Najua Rais ni taasisi kama mnamshauri anakataa bora mjiuzulu hamna kazi mnayofanya hebu angalieni effect za speech zake kwenye vyombo vya habari ya kimataifa kama BBC, VOA etc. na madhara ya speech zake kule WHO.
Atulie tu kwani anakosa nini kule Chato anyamaze janga la Corona litapita then tutarejea kwenye maisha ya kawaida kunyamaza kimya ni bora kuliko kuongea mambo yanayoacha maswali mengi zaidi ya majibu.
Rais kauli zake zina nguvu sana ndio maana unaona zinafuatiliwa sio tu Tanzania zaidi nje ya nchi clip zake zinazunguka zikiwa zimefanyiwa tafsiri ya lugha mbali mbali.