figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,491
- 54,884
Mwanza. Mhandisi wa Kivuko cha MV Nyerere, Alphonse Agustine Charahani aliyekaa majini kwa zaidi ya saa 48, amesema nahodha aliyekuwa zamu kivuko hicho kilipopinduka Septemba 20 ni msomi na mtaalamu mzoefu na si deiwaka (kibarua) kama inavyodaiwa.
Katika mazungumzo kwa njia ya simu leo Oktoba 7, 2018, mhandisi Charahani amesema, nahodha huyo Abel Constatine Mahatine ambaye pia alifariki katika ajali hiyo, alikuwa mhitimu na alikuwa amefanya shughuli hiyo kwa zaidi ya miaka 10.
"Hayo madai kwamba marehemu alikuwa ‘deiwaka’, nimekuja kuyasikia hapa nje. Kwa nini watu wasijiulize kwamba ‘deiwaka’ angepataje fursa ya kupeleka chombo kama kile kwa muda mrefu kiasi hicho?," Alihoji mhandisi.
Aliongeza kwamba, nahodha (marehemu) alikuwa zamu siku hiyo, wapo wawili wanapokezana na wala si deiwaka kama inavyodaiwa.
Kuhusu kupakia abiria na mizigo kupita kiasi, amesema hilo hawezi kulijibu kwa kuwa wakati wote wa shughuli ya upakiaji kazi yake inakuwa kuangalia na kurekebisha mitambo na kuhakikisha kwamba chombo kipo imara kwa ajili ya kuanza safari.
"Yani baada ya kufika hapa nje sasa ndiyo nimekutana na mambo mengi, hivi kweli itakuaje mimi nianze kuangalia idadi ya watu na mizigo badala ya kufungua na kujaribu injini kama ziko sawa? Mimi jukumu langu ni kuhakikisha kivuko kinang’oa na kutia nanga salama," amesema mhandisi Alphonse.
Amesema licha ya kwamba kuna baadhi ya wenzake bado wapo chini ya ulinzi kwa ajili ya mahojiano ameishukuru Serikali kwa kumruhusu kwenda nyumbani kwake.
Mhandisi huyo mkazi wa Kigongo Ferry, wilayani Misungwi amesema hana sababu maalum ya kuikacha kazi ya uhandisi majini akitolea mfano mafundi wa magari kwamba wakati gari linapopata ajali, mafundi na madereva wanaendelea na kazi kama kawaida.
"Hii ni ajali kama nyingine na siwezi kusema kwamba nimeacha kuwa mhandisi, hii ni mipango ya Mungu ukizingatia maili chache zilizokuwa zimebaki kabla ya kivuko kutia nanga," amesema.
Kuhusu kukaa majini kwa zaidi ya saa 48, amesema ni miujiza ya Mungu na kushukuru kwamba wakati kivuko hicho kinapinduka, alikuwa kwenye ofisi yake akiendelea na shughuli kama kawaida.
"Siwezi kusema moja kwa moja kwamba ninajua sababu ya kuzama kwa MV Nyerere lakini tu nahisi ni bahati mbaya baada ya nahodha kupotea kidogo na kutoka kwenye mstari. Nadhani katika kushtuka kwake ndipo aligeuza kivuko ghafla na kusababisha uzito kuelekea upande mmoja. Sina uhakika lakini," amesema Alphonse.
Mhandisi huyo amekana kuzungumzia suala la kuwa chini ya ulinzi mkali akiwa katika Hospitali ya Rufaa Bugando na kuongeza kwamba wakati wa kuzungumza hilo utafika.
Pia amebainisha kwamba kati ya watu 41 waliookolewa majini, watatu walikuwa wafanyakazi kwenye kivuko hicho na wanafanyiwa mahojiano.
Mhandisi Charahani aliokolewa zaidi ya saa 48 baada ya kupinduka kwa kivuko cha MV Nyerere katika kijiji cha Bwisya eneo la Ukara wilayani Ukerewe. Ni ajali ambayo ilisababisha vifo vya zaidi ya watu 225.
Chanzo: Mwananchi.
MY TAKE:
Watu wamekuwa wakilalamikia Washauri na wanaomfikishia taarifa rais kwamba wanampa taarifa zisizo sahihi, Natokeo yake anapohutubia taifa au kuonge kwenye vyombo vya habari anakuwa anakosea bila kujua.
Taarifa ya Ikulu ilisema Nahodha ailikuwa deiwaka. Rais Magufuli amedokeza mambo yaliyosababisha kutokea kwa ajali hiyo kuwa ni pamoja na nahodha wa kivuko hicho kuwa si mwenyewe ila ‘deiwaka.
Ni wakati wa kujitafakari, Mnapofikisha habari kwa rais, kumbuka anawakilisha wananchi wote na neno lake ni sheria. Anaweza saini adhabu ya kifo mtu akanyongwa kimakosa. kuweni makini
Habari zaidi, soma=>Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa! - JamiiForums
Katika mazungumzo kwa njia ya simu leo Oktoba 7, 2018, mhandisi Charahani amesema, nahodha huyo Abel Constatine Mahatine ambaye pia alifariki katika ajali hiyo, alikuwa mhitimu na alikuwa amefanya shughuli hiyo kwa zaidi ya miaka 10.
"Hayo madai kwamba marehemu alikuwa ‘deiwaka’, nimekuja kuyasikia hapa nje. Kwa nini watu wasijiulize kwamba ‘deiwaka’ angepataje fursa ya kupeleka chombo kama kile kwa muda mrefu kiasi hicho?," Alihoji mhandisi.
Aliongeza kwamba, nahodha (marehemu) alikuwa zamu siku hiyo, wapo wawili wanapokezana na wala si deiwaka kama inavyodaiwa.
Kuhusu kupakia abiria na mizigo kupita kiasi, amesema hilo hawezi kulijibu kwa kuwa wakati wote wa shughuli ya upakiaji kazi yake inakuwa kuangalia na kurekebisha mitambo na kuhakikisha kwamba chombo kipo imara kwa ajili ya kuanza safari.
"Yani baada ya kufika hapa nje sasa ndiyo nimekutana na mambo mengi, hivi kweli itakuaje mimi nianze kuangalia idadi ya watu na mizigo badala ya kufungua na kujaribu injini kama ziko sawa? Mimi jukumu langu ni kuhakikisha kivuko kinang’oa na kutia nanga salama," amesema mhandisi Alphonse.
Amesema licha ya kwamba kuna baadhi ya wenzake bado wapo chini ya ulinzi kwa ajili ya mahojiano ameishukuru Serikali kwa kumruhusu kwenda nyumbani kwake.
Mhandisi huyo mkazi wa Kigongo Ferry, wilayani Misungwi amesema hana sababu maalum ya kuikacha kazi ya uhandisi majini akitolea mfano mafundi wa magari kwamba wakati gari linapopata ajali, mafundi na madereva wanaendelea na kazi kama kawaida.
"Hii ni ajali kama nyingine na siwezi kusema kwamba nimeacha kuwa mhandisi, hii ni mipango ya Mungu ukizingatia maili chache zilizokuwa zimebaki kabla ya kivuko kutia nanga," amesema.
Kuhusu kukaa majini kwa zaidi ya saa 48, amesema ni miujiza ya Mungu na kushukuru kwamba wakati kivuko hicho kinapinduka, alikuwa kwenye ofisi yake akiendelea na shughuli kama kawaida.
"Siwezi kusema moja kwa moja kwamba ninajua sababu ya kuzama kwa MV Nyerere lakini tu nahisi ni bahati mbaya baada ya nahodha kupotea kidogo na kutoka kwenye mstari. Nadhani katika kushtuka kwake ndipo aligeuza kivuko ghafla na kusababisha uzito kuelekea upande mmoja. Sina uhakika lakini," amesema Alphonse.
Mhandisi huyo amekana kuzungumzia suala la kuwa chini ya ulinzi mkali akiwa katika Hospitali ya Rufaa Bugando na kuongeza kwamba wakati wa kuzungumza hilo utafika.
Pia amebainisha kwamba kati ya watu 41 waliookolewa majini, watatu walikuwa wafanyakazi kwenye kivuko hicho na wanafanyiwa mahojiano.
Mhandisi Charahani aliokolewa zaidi ya saa 48 baada ya kupinduka kwa kivuko cha MV Nyerere katika kijiji cha Bwisya eneo la Ukara wilayani Ukerewe. Ni ajali ambayo ilisababisha vifo vya zaidi ya watu 225.
Chanzo: Mwananchi.
MY TAKE:
Watu wamekuwa wakilalamikia Washauri na wanaomfikishia taarifa rais kwamba wanampa taarifa zisizo sahihi, Natokeo yake anapohutubia taifa au kuonge kwenye vyombo vya habari anakuwa anakosea bila kujua.
Taarifa ya Ikulu ilisema Nahodha ailikuwa deiwaka. Rais Magufuli amedokeza mambo yaliyosababisha kutokea kwa ajali hiyo kuwa ni pamoja na nahodha wa kivuko hicho kuwa si mwenyewe ila ‘deiwaka.
Ni wakati wa kujitafakari, Mnapofikisha habari kwa rais, kumbuka anawakilisha wananchi wote na neno lake ni sheria. Anaweza saini adhabu ya kifo mtu akanyongwa kimakosa. kuweni makini
Habari zaidi, soma=>Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa! - JamiiForums