Ikumbukwe kuwa TAL alishambuliwa kwa risasi na watu wasijulikana takribani mwaka mmoja na nusu uliopita. Tangu aliposhambuliwa, yaani 07/09/2017 hadi hivi sasa TAL hayupo nchini kwani alipelekwa Kenya na baadaye Ubelgiji kwa matibabu.
Watanzania tumekuwa tukimuombea baraka kwa Mwenyezi Mungu apone haraka ili aweze kuendeleza gurudumu la maendeleo hasa kwa wapiga kura wake wa Jimbo la Singida Mashariki. Tumekuwa tukimsubiri kwa hamu sana katika hilo.
Ni wazi kuwa ukimya wake kwa muda huo, haukumfanya apotee kisiasa licha ya kukaa nje ya nchi. Na kauli za msimu alizozitoa zilisambaa kwa kasi na kuwa na impact kwa kiasi kikubwa katika kumfanya aendelee kuwa akilini mwa watu.
Wanaomshauri TAL kufanya ziara katika nchi za Ulaya na Amerika wanamuingiza “Chaka” kisiasa. Ziara hizo amezigeuza kuwa za kisiasa, na hivyo watu wameshazizoea na sasa ufuatiliaji umekuwa mdogo sana, in other words wameanza kumpotezea. Hii ina maana kwamba hata siku akirudi nchini hatakuwa na jipya la kuwafanya Watanzania wavutwe na kile anachokiongea. Kuna baadhi ya watu ambao hutoa kura za huruma na hasa kutokana na hali yake, kwa yeye kuwa masikioni mwa watu kila siku kunamfanya azoeleke na hivyo baadaye ataonekana wa kawaida tu na hivyo kuzikosa kura hizo.
Moja kati ya kauli za mwanzo kabisa alizozitoa TAL (source: Social media) baada ya kupata fahamu ilikuwa ni; “Mwenyekiti, I survived to tell a tale, Please keep up fighting". Watanzania tumekuwa tukisubiri kwa hamu arudi na kutumbia, ni nini alichotaka kutuambia, lakini baadaye tumejua kwamba, he planned to tell us that he will run for president in the 2020 elections.
Anayoyasema angekuja kuyasemea nyumbani pindi atakaporudi, yangemsaidia kumpa political mileage, ila kwa sasa asipokuwa makini ndio kupotea huko. Kwake naweza kusema kuwa amekuwa na “Bad Timing” ya kutangaza alichotangaza.
Watanzania tumekuwa tukimuombea baraka kwa Mwenyezi Mungu apone haraka ili aweze kuendeleza gurudumu la maendeleo hasa kwa wapiga kura wake wa Jimbo la Singida Mashariki. Tumekuwa tukimsubiri kwa hamu sana katika hilo.
Ni wazi kuwa ukimya wake kwa muda huo, haukumfanya apotee kisiasa licha ya kukaa nje ya nchi. Na kauli za msimu alizozitoa zilisambaa kwa kasi na kuwa na impact kwa kiasi kikubwa katika kumfanya aendelee kuwa akilini mwa watu.
Wanaomshauri TAL kufanya ziara katika nchi za Ulaya na Amerika wanamuingiza “Chaka” kisiasa. Ziara hizo amezigeuza kuwa za kisiasa, na hivyo watu wameshazizoea na sasa ufuatiliaji umekuwa mdogo sana, in other words wameanza kumpotezea. Hii ina maana kwamba hata siku akirudi nchini hatakuwa na jipya la kuwafanya Watanzania wavutwe na kile anachokiongea. Kuna baadhi ya watu ambao hutoa kura za huruma na hasa kutokana na hali yake, kwa yeye kuwa masikioni mwa watu kila siku kunamfanya azoeleke na hivyo baadaye ataonekana wa kawaida tu na hivyo kuzikosa kura hizo.
Moja kati ya kauli za mwanzo kabisa alizozitoa TAL (source: Social media) baada ya kupata fahamu ilikuwa ni; “Mwenyekiti, I survived to tell a tale, Please keep up fighting". Watanzania tumekuwa tukisubiri kwa hamu arudi na kutumbia, ni nini alichotaka kutuambia, lakini baadaye tumejua kwamba, he planned to tell us that he will run for president in the 2020 elections.
Anayoyasema angekuja kuyasemea nyumbani pindi atakaporudi, yangemsaidia kumpa political mileage, ila kwa sasa asipokuwa makini ndio kupotea huko. Kwake naweza kusema kuwa amekuwa na “Bad Timing” ya kutangaza alichotangaza.