Kama kawaida yetu Watanzania tuna utamaduni wa kushabikia tu kila kitu na kwenda na upepo. Lakini kuna wakati mwingine ni lazima tujiulize ili kunusuru taifa. Sio kila lifanyikalo ni kwa manufaa ya taifa kuna mengi sana ambayo viongozi wanafanya kwa manufaa yao kuonesha wenyewe ni miungu.
Kwenye hili la kutaka kushinda kwa namna yeyote 100% ya watu wote wanaochaguliwa bila kujali matakwa ya wananchi ina nia gani kwa taifa. Kwa sasa Tanzania bunge linapitisha chochote watakacho serikali, wana uongozi wote mpaka wilayani kwa 100%. Sasa jiulizeni ni yapi mapya ambayo wanatafuta?
Kwa mtazamo wa haraka haraka wanatafuta wakati ambako hata wabunge wa chama tawala kunyamazishwa. Kamati zote za bunge na CAG kunyamazishwa kabisa.
Vilevile kutafuta njia kunyamazisha hata mitandao iliyopo lakini kuwe na ubadilishaji wa sheria bila watu kujua.
Sasa kabla ya kushabikia kila kitu jiulize: Baada ya Magu kuondoka, tumeshaona muda ulivyo mfupi. Je, tukipata mtu mbinafsi itakuwaje? Mjue hii miradi mikubwa haijafika hata nusu na Magu ataondoka bila kumaliza? Treni hadi Dodoma bado; sasa itafika lini Kigoma?
Mradi wa umeme bwawa ndiyo wanasafisha njia itachukuwa miaka mingapi kuwa umeme?
Vilevile kuna uwezekano kabisa nia ya Magu ni kuwa na Bunge la kumuongezea muda madarakani kwa kisingizio cha miradi kutokukamilika na kutokuwaamini viongozi wengine.
Na kwasababu kutakuwa hakuna upinzani atasema sasa nani atazungumza kukitokea rushwa? Hivyo nia ni kuweka bunge lisiloaminika kwa wananchi na kubaki na serikali kuu pekee kama muhula mmoja tu.
Kwenye huo muhula mmoja nao wakumwamini awe mtu mmoja tu ambaye ni Rais. Sasa hivi wanatafuta mbinu za kuzuia mitandao kama hii ili Watanzania wasijue lolote.
Kwenye hili la kutaka kushinda kwa namna yeyote 100% ya watu wote wanaochaguliwa bila kujali matakwa ya wananchi ina nia gani kwa taifa. Kwa sasa Tanzania bunge linapitisha chochote watakacho serikali, wana uongozi wote mpaka wilayani kwa 100%. Sasa jiulizeni ni yapi mapya ambayo wanatafuta?
Kwa mtazamo wa haraka haraka wanatafuta wakati ambako hata wabunge wa chama tawala kunyamazishwa. Kamati zote za bunge na CAG kunyamazishwa kabisa.
Vilevile kutafuta njia kunyamazisha hata mitandao iliyopo lakini kuwe na ubadilishaji wa sheria bila watu kujua.
Sasa kabla ya kushabikia kila kitu jiulize: Baada ya Magu kuondoka, tumeshaona muda ulivyo mfupi. Je, tukipata mtu mbinafsi itakuwaje? Mjue hii miradi mikubwa haijafika hata nusu na Magu ataondoka bila kumaliza? Treni hadi Dodoma bado; sasa itafika lini Kigoma?
Mradi wa umeme bwawa ndiyo wanasafisha njia itachukuwa miaka mingapi kuwa umeme?
Vilevile kuna uwezekano kabisa nia ya Magu ni kuwa na Bunge la kumuongezea muda madarakani kwa kisingizio cha miradi kutokukamilika na kutokuwaamini viongozi wengine.
Na kwasababu kutakuwa hakuna upinzani atasema sasa nani atazungumza kukitokea rushwa? Hivyo nia ni kuweka bunge lisiloaminika kwa wananchi na kubaki na serikali kuu pekee kama muhula mmoja tu.
Kwenye huo muhula mmoja nao wakumwamini awe mtu mmoja tu ambaye ni Rais. Sasa hivi wanatafuta mbinu za kuzuia mitandao kama hii ili Watanzania wasijue lolote.