Uchaguzi 2020 Wasanii wasiwe na uchu wa madaraka kwa kutaka kila mmoja kugombea kwenye Uchaguzi

Yoyo Zhou

Member
Jun 16, 2020
72
110
Kura.jpg

Ni miezi michache tu imesalia kwa Tanzania kushuhudia wananchi wake wakijitosa kwenda kwenye vituo vya kupiga kura na kutumia demkorasia yao halali ya kuwachagua viongozi wanaowataka. Kwa wananchi wengi, uchaguzi ni hatua moja kubwa ya kuchagua viongozi ambao watakuja kulijenga au kuliporomosha taifa.

Tunafahamu kuwa kuchagua au kuchaguliwa ni haki na ni demokrasia ya kila mtu hasa endapo umetimiza umri wa kuchagua ama vigezo vya kuchaguliwa. Ndio maana hivi karibuni tumekuwa tukishuhudia wimbi kubwa la wasanii wakitangaza nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi ujao. Wimbi hili kwa sasa limezua maswali mengi sana, wengi wakishuku uwezo wa kuongoza wa wasanii hawa wanaotaka kuhama kwenye sanaa na kuingia upande wa siasa. Uongozi sasa umegeuzwa kama mchezo wa watoto ambapo kila atakaye anajiunga na kucheza. Kwa ninavyofahamu kiongozi ili uitwe kiongozi basi ni lazima kutakuwa na vigezo vyake vinavyokutambulisha kuwa wewe ni kiongozi, halikadhalika kwa msanii pia kutakuwa na vigezo vyake. Lakini kinachotia hofu ni kwamba baadhi ya wasanii wanatumia umaarufu wao waliopata kwenye usanii na kuamua kujitosa kwenye siasa. Uongozi sio lele mama, uongozi unahitaji weledi na uwezo mkubwa, lakini pia unahitaji mtu kujitoa kwa kuweka mbele maslahi ya watu waliokutuma na kukuchagua kuliko maslahi yako binafsi.

Kwa Tanzania nafasi inayoonekana kukodolewa macho na wasanii wengi ni ya ubunge. Tumesikia majina makubwa ya wasanii kama vile Rajab Abdul Kahali au maarufu kama Harmonize ambaye aliweka wazi nia yake ya kutaka kugombea ubunge kwenye jimbo la nyumbani kwao alikozaliwa huko Tandahimba Mtwara. Ingawa kwa upande mmoja ndoto ya Harmonize ilichochewa na rais Magufuli alipomwambia ajitokeze kugombea kwenye jimbo lake, lakini kabla ya kuamua kuingia mzimamzima kwanza alipaswa kujipima na kujiuliza je, kweli ninafaa kuliongoza jimbo? Wengine ni Hamisi Mwinjuma almaarufu kama Mwana FA, mtoto wa mwanasiasa mkongwe Steven Wasira ambaye anaitwa Wabiro Noel Wasira maarufu kwa jina la Wakazi, msanii wa kike anayeitwa Zuwena Mohammed anayejulikana zaidi kama Shilole, na Steven Mlengele maarufu kama Steve Nyerere, ambaye ni muigizaji na ameshaueleza umma kuwa jimbo la Iringa mjini safari hii ndilo atakalokwenda kuwania.

Huu si uchaguzi wa kwanza kushuhudia wasanii au hata wanamichezo wakitupia jicho lao kwenye siasa, mfano mzuri ni aliyekuwa mchezaji maarufu wa Liberia ambaye baadaye akaingia kwenye ulingo wa siasa, George Manneh Oppong Weah. Ni rais wa 25 nchini Liberia lakini ukiangalia huko nyuma kabla ya kuingia madarakani alipata pingamizi kubwa kwa kuonekana kwamba hana uwezo wala uzoefu wa kuendesha nchi.

Kwa suala hili la uzoefu na uwezo wa kuongoza, watu huwa wanataka viongozi wenye akili tendaji na masikio sikivu yatakayoweza kusikia vilio vya wananchi wenye shida mbalimbali. Na sio viongozi ambao wanaingia madarakani kutokana na shinikizo la mashabiki wao au kusifiwa kidogo tu kuwa wana uwezo wa kuongoza pasi na kujitathmini kwanza kujua kama kweli wanaweza kuongoza jahazi bila kulipeleka mrama.

Kama hayo hayatoshi juzijuzi tu tumesikia tena msanii nguli nchini Marekani Kanye West akitangaza kupitia twitter kwamba kwenye uchaguzi wa rais wa Novemba 3 mwaka huu naye pia atawania. Kanye anasema anawania kwasababu “Mungu amemfumbua macho na kumwambia kwamba sasa ndio wakati wenyewe”

Ni kweli dini ni muhimu kwa muumini yeyote yule, lakini hapa tunazungumzia kuongoza taifa. Mana kipindi ugonjwa wa corona ulipoibuka baadhi ya viongozi wa dini pia walisema wameoteshwa na Mungu usingizini dawa ya corona, cha ajabu hakuna hata mmoja wao aliyetoa dawa hiyo, na kibaya zaidi miongoni mwa haohao waliosema wameoteshwa dawa, sasa wameshatangulia mbele ya haki kwa ugonjwa wa COVID-19. Kwa hiyo kabla ya kufanya jambo lolote ni lazima kwanza tungekaa na kutafakari.
 
Sioni cha maana ulichoandika kazi alizofanya Prof jay bungeni huwezi zifananisha na Job spika katika jimbo lake
 
Mkuu ukiachana tu na title yao ya usani, wale nao Ni Watanzania Kama wewe na Wana haki ya kugombea nafasi yeyote Kama sifa wanakidhi.
Kwahiyo wewe usiume kwa maamuzi yao ambayo yapo sawa kikatiba. Waachie wananchi ndo wataamua kwenye box la kura.

Note; Siyo kila anaechukua fomu ya kugombea atapita na siyo kila anaepita kwenye mchujo wa chama ndo ashakuwa Mbunge, hivyo Basi bado Ni mapema mno kuwalaumu Hawa Watanzania wenzako juu ya haki Yao kikatiba.
 
Mkuu ukiachana tu na title yao ya usani, wale nao Ni Watanzania Kama wewe na Wana haki ya kugombea nafasi yeyote Kama sifa wanakidhi.
Kwahiyo wewe usiume kwa maamuzi yao ambayo yapo sawa kikatiba. Waachie wananchi ndo wataamua kwenye box la kura.

Note; Siyo kila anaechukua fomu ya kugombea atapita na siyo kila anaepita kwenye mchujo wa chama ndo ashakuwa Mbunge, hivyo Basi bado Ni mapema mno kuwalaumu Hawa Watanzania wenzako juu ya haki Yao kikatiba.

Ubunge ni kazi kama kazi nyingine lakini ubunge mtamu zaidi kimaslahi........ Thinking of Nasari
 
Ni miezi michache tu imesalia kwa Tanzania kushuhudia wananchi wake wakijitosa kwenda kwenye vituo vya kupiga kura na kutumia demkorasia yao halali ya kuwachagua viongozi wanaowataka. Kwa wananchi wengi, uchaguzi ni hatua moja kubwa ya kuchagua viongozi ambao watakuja kulijenga au kuliporomosha taifa.

Tunafahamu kuwa kuchagua au kuchaguliwa ni haki na ni demokrasia ya kila mtu hasa endapo umetimiza umri wa kuchagua ama vigezo vya kuchaguliwa. Ndio maana hivi karibuni tumekuwa tukishuhudia wimbi kubwa la wasanii wakitangaza nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi ujao. Wimbi hili kwa sasa limezua maswali mengi sana, wengi wakishuku uwezo wa kuongoza wa wasanii hawa wanaotaka kuhama kwenye sanaa na kuingia upande wa siasa. Uongozi sasa umegeuzwa kama mchezo wa watoto ambapo kila atakaye anajiunga na kucheza. Kwa ninavyofahamu kiongozi ili uitwe kiongozi basi ni lazima kutakuwa na vigezo vyake vinavyokutambulisha kuwa wewe ni kiongozi, halikadhalika kwa msanii pia kutakuwa na vigezo vyake. Lakini kinachotia hofu ni kwamba baadhi ya wasanii wanatumia umaarufu wao waliopata kwenye usanii na kuamua kujitosa kwenye siasa. Uongozi sio lele mama, uongozi unahitaji weledi na uwezo mkubwa, lakini pia unahitaji mtu kujitoa kwa kuweka mbele maslahi ya watu waliokutuma na kukuchagua kuliko maslahi yako binafsi.

Kwa Tanzania nafasi inayoonekana kukodolewa macho na wasanii wengi ni ya ubunge. Tumesikia majina makubwa ya wasanii kama vile Rajab Abdul Kahali au maarufu kama Harmonize ambaye aliweka wazi nia yake ya kutaka kugombea ubunge kwenye jimbo la nyumbani kwao alikozaliwa huko Tandahimba Mtwara. Ingawa kwa upande mmoja ndoto ya Harmonize ilichochewa na rais Magufuli alipomwambia ajitokeze kugombea kwenye jimbo lake, lakini kabla ya kuamua kuingia mzimamzima kwanza alipaswa kujipima na kujiuliza je, kweli ninafaa kuliongoza jimbo? Wengine ni Hamisi Mwinjuma almaarufu kama Mwana FA, mtoto wa mwanasiasa mkongwe Steven Wasira ambaye anaitwa Wabiro Noel Wasira maarufu kwa jina la Wakazi, msanii wa kike anayeitwa Zuwena Mohammed anayejulikana zaidi kama Shilole, na Steven Mlengele maarufu kama Steve Nyerere, ambaye ni muigizaji na ameshaueleza umma kuwa jimbo la Iringa mjini safari hii ndilo atakalokwenda kuwania.

Huu si uchaguzi wa kwanza kushuhudia wasanii au hata wanamichezo wakitupia jicho lao kwenye siasa, mfano mzuri ni aliyekuwa mchezaji maarufu wa Liberia ambaye baadaye akaingia kwenye ulingo wa siasa, George Manneh Oppong Weah. Ni rais wa 25 nchini Liberia lakini ukiangalia huko nyuma kabla ya kuingia madarakani alipata pingamizi kubwa kwa kuonekana kwamba hana uwezo wala uzoefu wa kuendesha nchi.

Kwa suala hili la uzoefu na uwezo wa kuongoza, watu huwa wanataka viongozi wenye akili tendaji na masikio sikivu yatakayoweza kusikia vilio vya wananchi wenye shida mbalimbali. Na sio viongozi ambao wanaingia madarakani kutokana na shinikizo la mashabiki wao au kusifiwa kidogo tu kuwa wana uwezo wa kuongoza pasi na kujitathmini kwanza kujua kama kweli wanaweza kuongoza jahazi bila kulipeleka mrama.

Kama hayo hayatoshi juzijuzi tu tumesikia tena msanii nguli nchini Marekani Kanye West akitangaza kupitia twitter kwamba kwenye uchaguzi wa rais wa Novemba 3 mwaka huu naye pia atawania. Kanye anasema anawania kwasababu “Mungu amemfumbua macho na kumwambia kwamba sasa ndio wakati wenyewe”

Ni kweli dini ni muhimu kwa muumini yeyote yule, lakini hapa tunazungumzia kuongoza taifa. Mana kipindi ugonjwa wa corona ulipoibuka baadhi ya viongozi wa dini pia walisema wameoteshwa na Mungu usingizini dawa ya corona, cha ajabu hakuna hata mmoja wao aliyetoa dawa hiyo, na kibaya zaidi miongoni mwa haohao waliosema wameoteshwa dawa, sasa wameshatangulia mbele ya haki kwa ugonjwa wa COVID-19. Kwa hiyo kabla ya kufanya jambo lolote ni lazima kwanza tungekaa na kutafakari.
Kwanza nani atawapigia kura wahuni hao?
 
Nakuunga mkono. Unajua watanzania sijajua kwa namna siku zinavyozidi kwenda ni kama uwezo wetu wa kureason unazidi kushuka kwa kasi kwa kujifanya tunafikiri kama wazungu.

Unajua kila jamii ina value zake na standard. Naona sisi tunaanza kupuuza zetu na kuanza kuchanganya standard za hovyo hovyo kiasi kwamba zinaanza kutuathiri na kuanza kuzalisha kizazi cha ajabu. Nitakupa mifano:

Kuna speech moja ya nyerere alizungumzia kiongozi ambae alikutwa na skendo ya kutembea na kahaba huko ulaya na ikajulikana hadi katika vyombo vya habari. Yule kiongozi aliandika barua ya kujiuzuru na kuachia wadhifa wake mara moja.

Kwann ilibidi kufanya vile?! Lile ni tendo la kutii na kuheshimu jamii anayoongoza na kuheshimu miiko waliyojiwekea. Kitendo cha kiongozi kutembea na kahaba ni ishara kuwa unaongoza jamii ya watu wafuska wapenda ngono, wasiojielewa na wasio na maadili. Hivyo kiongozi wa namna hii hapaswi hata kuwa mfano wa raia wa kawaida na hatakiwi kuwapo katika nafasi ya uongozi.

Sisi pia kama wa Tanzania tunayomiiko ambayo katu haibatilishwi na watu wachache wasioiheshimu. Nitawapa mfano, leo kuna mabinti kama akina wema sepetu, akina jokate, akina irene uwoya, akina irene wolper, akina shilole na vijana wa kiume kama akina Diamond, alikiba, harmonize na wengineo tunaowaona kila uchao na matukio yao kwenye mitandao ya jamii ..... Hawa ni wanajamii sawa na ni raia wenzetu ila mienendo yao inatupa alama za viulizo vichwani tunapohoji uhalali wa wao kushiriki shughuli za uongozi tukiamini wapo hapo kulisaidia taifa....

Kwa nijuavyo mimi kiongozi si mtu maarufu au mashuhuri tu bali ni mtu ambaye mwenendo wake ni umestaarabika na ni mfano wa kuigwa. Kila mwanadamu anakosea ila sasa kuna kiwango cha utomvu wa nidhamu si cha kupuuza......

Jamii ifike wakati ifanye mchujo serious wa nani anakwenda kukaa hata katika uongozi ngazi ya shina na hata serikali ya mtaa.

Watu ambao history zao zinakiuka miiko ya uongozi na sifa za raia wa kawaida wabakie kufanya shughuli zao, sio mtu akijisikia tu kuwa anataka kutafuta maisha kupitia siasa basi anavaa suti na kujifanya anauchungu na taifa. Thats a big no.

Tuna vijana wengi hawajulikani ila ni watendaji wazuri sana na wanaspirit ya maendeleo na hawapo kwaajiri ya masilahi yao binafsi.

Leo unakwenda kumuweka kingwendu, Steve nyerere, sijui wema sepetu, joketi, irene uwoya, jb sijui na nani ambaye amekuja pale kutafuta maisha hivi atatuwakilishaje katika mipango ya maendeleo ambayo kutwa kucha inapigwa vita na mataifa jirani na mataifa ya magharibi.

Hivi steve nyerere anajua nini kuhusu mfumo wa elimu, kuhusu BOT, kuhusu mfumuko wa bei, kuhusu soko la mitaji, Maswala ya Nishati na madini, bei za soko la dunia za malighafi mbali mbali, anajua nini kuhusu socioeconomic za watanzania, effect ya kupanda na kushuka kwa thamani ya fedha, gharama za miundo mbinu.... Nini anajua....

Hebu tuwe tunakagua kwanza background..... Kizazi chetu sio cha kukiambia nitajenga shule, nitajenga barabara, nitaleta maji na umeme..... Hiki ni kizazi kipya chenye changamoto za tofauti.

Hebu tuwe serious. Kuna vijana ni wasomi na wapo ambitious and capable kwenye maendeleo achaneni na hawa wapuuzi sijui gwajima mtu anabwabwaja hovyo, analala na wanawake video zinavuja na nyie mnaona sawa tu, sijui mchungaji gani tena yule mwingine.... Hebu tuweni makini jamani.... Tuwe serious. Na hizi viti maalumu zifutwe maana naona zinapeleka wabunge sanamu tu pale. Wanakwenda kukaa hakuna wanalofanya zaidi kugonga meza na kuuza sura wakichat na kupiga selfie.....
 
Kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania kila mwananchi ana haki ya kuchagua na kuchaguliwa, hasa akitimiza matakwa ya Katiba hiyo.
Kuhusu kupata uongozi dhaifu ndani ya bunge, huo utakuwa uamuzi wa wapiga kura wenyewe.
Hata hivyo, tujiulize mbunge kama Abdallah Mtolea wa Temeke ambaye anajitambulisha kuwa mwanasheria au mbunge wa Kinondoni wamechangia kipi kikubwa kwenye majimbo yao kumshinda msanii profesa J wa Mikumi?
Waacheni Wagombee, maana hata hawa akina Nassari tuliowaamini wametuangusha
 
Back
Top Bottom