Wasanii toka Arusha acheni kujibagua na kupigania mkoa badala ya taifa

Kupitia huu uzii aisee wachaga hatupendwi na naisi yote ni sababu ya chuki kupandikizwa vichwani Kwa watu sababu labda Kwa maendeleo waliyonayo wachaga au sababu ya wao kubebana kwenye nafasi mbalimbali au kushiriki pamoja katamu ya mwisho wa mwka jaman punguzeni makasiriko ata kama ni wewe unaweza kumuacha ndugu yako,kabilaa lako au mtu wa mkoa mmoja kumuweka kwenye kazi wakati unaona anasifa zote nimekaa na waluguru hawabebani kabisa Aya kama mwenzake ana uwezo au sifa zote zaidi atamkandamiza sasa Kwa staili iyoo Sisi wachaga kosa letu nini kujaliana au kubebana kwetu
 
Hii kitu itakuja kuleta shida kubwa sana kwetu wasukuma miaka 20+ baadae, maana wasomi wasukuma watakua wamejaa kila kona ya Shinyanga, Mwanza,Tabora, Geita, Simiyu yaani itakua wakiitisha nafasi za kazi basi asilimia 80 ya wanao omba kazi watakua watu wa lake zone hapo ndipo wimbo utapigwa remix. Itakua vita ya wasukuma vs kanda ndogo ndogo. Jah Bless Lake zone
Hahahahahaah Acha nikwambie kilaza ww wachaga hii nchi yote wamegusa alafu wala haturingi Mzee wenu alijaribu kutumaliza Ila ndyo ivyoo Mungu naye ana mengi zaidi yetu na usitegeemee mama atabesi sehemu nyingine zaidi ya kaskazini sis hatung'ang'anii kazi tunataka Tu nafasi nyeti akikaa mmoja kama kiongozi pengine potee tutaingiza WA kwetu ata kama mtasomesha wenenu wote Ila watoto zetu watafanya kazi mikoa mwingine na kwetu mtapasikia Tu
 
Hahahahahaah Acha nikwambie kilaza ww wachaga hii nchi yote wamegusa alafu wala haturingi Mzee wenu alijaribu kutumaliza Ila ndyo ivyoo Mungu naye ana mengi zaidi yetu na usitegeemee mama atabesi sehemu nyingine zaidi ya kaskazini sis hatung'ang'anii kazi tunataka Tu nafasi nyeti akikaa mmoja kama kiongozi pengine potee tutaingiza WA kwetu ata kama mtasomesha wenenu wote Ila watoto zetu watafanya kazi mikoa mwingine na kwetu mtapasikia Tu
vizuri
 
Wameimarisha baada ya Awamu ya 4 na ya 5 hasa ya 5 kuwatenga. Tuache sindano ituingie taratibu tupone ugonjwa wa ukabila na ukanda tuliojitakia wenyewe. Wakaskazini hatuwawezi hata tutambike. Wenzetu wameshatuacha mbali
Wanatuonea wivu
 
Kupitia huu uzii aisee wachaga hatupendwi na naisi yote ni sababu ya chuki kupandikizwa vichwani Kwa watu sababu labda Kwa maendeleo waliyonayo wachaga au sababu ya wao kubebana kwenye nafasi mbalimbali au kushiriki pamoja katamu ya mwisho wa mwka jaman punguzeni makasiriko ata kama ni wewe unaweza kumuacha ndugu yako,kabilaa lako au mtu wa mkoa mmoja kumuweka kwenye kazi wakati unaona anasifa zote nimekaa na waluguru hawabebani kabisa Aya kama mwenzake ana uwezo au sifa zote zaidi atamkandamiza sasa Kwa staili iyoo Sisi wachaga kosa letu nini kujaliana au kubebana kwetu
Hakuna anayekuchukia! Uchukiwe kwa kipi ulichonacho? Watu hawataki tabia za wengi wenu kuwabania kazi wengine maofisini, kutoa maneno yanayohatarisha muungano na mshikamano wa taifa letu(mifano IPO mingi tu) etc.

Unajaribu kuishi kwenye historia za miaka ya 60 na 70, nowadays kila kabila limekuja kasi na ninyi hamna kitu tena, mnaishia kuishi kwenye conspiracy theories, vyuoni wanenu wanaburuzwa, maofisini na kila sekta, kwenye siasa ndio usiseme ni hatari.

Hatuwachukii Wachagga, hatuwaonei wivu kwa maendeleo ambayo wanadai wanayo(stories za miaka ya 80, wengi ukienda Moshi utawaonea huruma, wanaishi kwenye mazingira magumu mno, mikoani wengi ni wafanyabiashara wadogo wadogo na wachuuzi), ila tunachukia viashiria vya baadhi yenu hususani 'public figures' kutoa maneno yenye sumu ambayo ni hatari kwa mshikamano wetu.

Again, no one hates you!
 
Nawasalimu kwa jina la JMT.

Juzi kwenye mkesha wa Christmas, dunia imeshuhudia magwiji wa muziki Nigeria, Wizkid, Davido, na Komredi Burna Boy, wakiungana kufanya show pamoja iliyoandaliwa na Tony Olumelu wa BOA bank. Iliashiria umoja na upendo miongoni mwa wasanii huko Nigeria. Kwa pamoja wameamua kulipigania na kuliwakilisha taifa lao vyema. Hili suala lilinitafakarisha sana hasa kuhusu sanaa ya hapa Tanzania.

Watanzania wengi waliochangia maoni kwenye post zilizohusu show ya hiyo miamba walikuwa wakiwatupia lawama kali Diamond na Alikiba. Mimi niliona wako sawa kwasababu Diamond na Kiba ni kama nembo za muziki wetu wangeweza kuhamasisha mambo yakabadilika. Ila binafsi sikupenda kujikita sana kuwalaumu hao wawili kwasababu wamefanya mambo mengi makubwa kwenye sanaa ya Tanzania. Wakati nikitafakari ndo nikakumbuka hawa wasanii kutoka Arusha. Nilipatwa na hasira kali sana kuhusiana na mienendo yao.

Wasanii wa Arusha ni wenye vipaji vikubwa pia wana exposure kubwa kutokana na kukulia kwenye kitovu cha utalii. Miongoni mwa wasanii wa mwanzo kupiga show za kimataifa walikuwa kundi la X-plastaz kutoka Arusha. R.I.P father Nelly. Hata wakongwe Chindoman na wengine ni watu wanaoijua vizuri mitaa ya mabeberu. Tatizo lililopo kwa wasanii wengi wa Arusha ni hii tabia mbaya ya kujitenga. Wao kila sehemu wanataka wawe wao tu bila kujichanganya na watu toka mikoa mingine. Hii ni tabia mbaya ya ubaguzi ambayo baba wa taifa aliichukia sana. Hayati Mwalimu Nyerere angekuwa hai angewakemea wasanii wote wanaodai wao ni wa Arachuga.

Huu upuuzi umefanya muziki wa Arusha kuwa duni sana na kuishia kuwa wasanii wa hapahapa. Na hii tabia imeota mizizi hadi kwa watu wengine ambao sio wasanii. Aliyekuwa mbunge wa Arumeru Nassari alishawahi kupanda jukwaani na kuropoka kuwa kuwepo jamhuri ya watu wa kaskazini. Mkimaliza kujibagua kwamba mmetoka Arusha mtaanza kubaguana kwamba huyu katoka Kijenge yule Kaloleni au Majengo. Watu wa Arusha tujichanganye na kusimama na watanzania wengine kama taifa moja la Tanzania.
Nikumbushe msanii toka Arusha mwenye kipaji.
 
1. Joh Makini
2. Vanesa Mdee
3. Lord Eyes
4. Gnako
5. Xplastaz - hawa ni rika la kina sugu na hadi mwanzoni mwa 2000 walikuwepo kwenye chati.
6. JCB
Vp Dogo janja hamjaweka kwenye list coz dini nyingine? Wagala acheni ubaguzi
 
Watu wametoa sumu zao ila mnaruhusiwa kutoa povu tu....hizi zote ni chuki na kujijengea ile inferiority complex..sidhan kama kuna ubaguz kiasi icho hadi watu mnashambulia kiasi hicho..ebu mjitathmin wenyew kuwa ni ukabila tu au ni nyie kuwa na wivu na ukanda flan iv
 
Hakuna inferior complex hawana jipya vile hatuna Shobo nao kwanza wanaonekana kama wezi wengi wao

Ishu wanaponda watu mfano kuwasema wasukuma wakibishana kidogo wanaleta ukaskzini wana nn cha maana tuliza mshono
Mkuu kunywa maji pressure itaondoka na ww
 
Watu wa kaskazini tunaonewa wivu sana kila kukicha lazima tusemwe inaonekana tunaupiga mwingi uwanja umeinama hadi kanda zote zinaungana kutudisi
Huwa hata maskin akikaa sehem ambapo kuna watu wanapanga deal zao za hela nyingi huwa lazma aanze kujibagua kwa kuona si level zake...lazma aanze kulalama kwamba wanajiona sanaa ndo maana hawanishirksh kweny deal lao
 
37 Reactions
Reply
Back
Top Bottom