Naisujaki Lekangai
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 1,340
- 1,377
Mimi napenda sana mizaha, ucheshi na kucheka ili kuniondolea stress za maisha.Hapa jf jukwaa la utani udaku na gossip nalitembelea sana ili kujifurahisha.Pia kwenye tv zetu ikitangazwa kwamba kuna kipindi cha comedy lazima nikitazame.
Bahati mbaya sana comedy za kwenye tv hapa tz si comedy zenye maana ya comedy - ni kitu kingine kabisa.Kwenye comedy ya kweli lazima mtu utabasamu na kucheka sana kwa mizaha na matani ya wahusika - misemo na maneno ya kuchekesha nk. Lakini comedy za hapa tz ni wahusika kufokeana, kukimbizana na kukatana mtama na magumi juu! Eti hiyo ni comedy! Mtu mzima (mimi) sicheki nikiona watu wakifokeana kukimbizana na kukatana mtama kushikana mashati.Hiyo inawachekesha watoto zaidi.
Kuna kituo kimoja cha tv mwanza kila alhamisi saa 3.30 usiku wanaonesha huo upuuzi wa kufukuzana na kukatana mtama na kuita eti ni comedy! Rimoti yangu imechakaa kwa ajili yao.Hata hiyo iitwayo ze komedi ya EATV ni sarakasi hizohizo, si comedy.
Enyi wasanii wa comedy tanzania chunguzeni vizuri maana ya comedy ili mfanye vitu vya komedi kweli mbali na kufokeana, kushikana mashati nk.
Hii ni wazi kabisa kwamba kama komedi ya kikundi mnachemsha hata standup comedy itakuwa shida.
Bahati mbaya sana comedy za kwenye tv hapa tz si comedy zenye maana ya comedy - ni kitu kingine kabisa.Kwenye comedy ya kweli lazima mtu utabasamu na kucheka sana kwa mizaha na matani ya wahusika - misemo na maneno ya kuchekesha nk. Lakini comedy za hapa tz ni wahusika kufokeana, kukimbizana na kukatana mtama na magumi juu! Eti hiyo ni comedy! Mtu mzima (mimi) sicheki nikiona watu wakifokeana kukimbizana na kukatana mtama kushikana mashati.Hiyo inawachekesha watoto zaidi.
Kuna kituo kimoja cha tv mwanza kila alhamisi saa 3.30 usiku wanaonesha huo upuuzi wa kufukuzana na kukatana mtama na kuita eti ni comedy! Rimoti yangu imechakaa kwa ajili yao.Hata hiyo iitwayo ze komedi ya EATV ni sarakasi hizohizo, si comedy.
Enyi wasanii wa comedy tanzania chunguzeni vizuri maana ya comedy ili mfanye vitu vya komedi kweli mbali na kufokeana, kushikana mashati nk.
Hii ni wazi kabisa kwamba kama komedi ya kikundi mnachemsha hata standup comedy itakuwa shida.