Wasanii Profesa J na Mzee Yusufu kugombea ubunge jijini Mwanza

AISEE KAMA WANANCHI WANACHAGUA MBUGE COZ OF UMAARUFU,sishangai why we are here even after
50yrs of uhuru.
 
Mzee Y. alishindwa kushauri Klabu Bingwa wa Afrika Mashariki na Kati na Vinara wa ligi kuu Vodacom ya Tz Dar. Young African.

Namjua vizuri. Hafai.
 
sugu kafungua njia, kama yeye alipata basi hata afande sele atagombea. Heshima ya bunge ilipotea alipo ingia wenje,mdee na sugu.

mganga wakienyeji MAJIMAREFU?, Au kwa kuwa ndo kawa mchawi na mtabili wenu baada yule alieshindwa kujua siku yake ya kufa kufa?,TUMEFIKA HAPA KWA UDHAIFU WA DHAIFU.
 
Hahahaha kwa kweli kuanzia leo cna muda tena wa kumsikiliza huyo ajiitae Prof Jay,mimi kwangu ccm ni kama uchafu kabisa cna haja ya kulificha hili.
 
kama J yuko hvyo basi na yeye atakuwa na mapungufu ya kimsingi sana kifikra
 
sugu kafungua njia, kama yeye alipata basi hata afande sele atagombea. Heshima ya bunge ilipotea alipo ingia wenje,mdee na sugu.

Unafiki hatutaki , hebu eleza namna Mh. Wenje, Mh. Mdee na Mh Sugu Walivyopoteza heshima ya bunge , siyo lazima kuchangia kama huna hoja , JF yote worldwide inakushangaa ndugu ! Shame on you !
 
Wakitaka kupotea kwenye sanaa wajaribu kunasiana na CCM , waangalie Bendi za CCM ZILIVYOKUFA ! Vijana jazz na TOT , Hata zikifanya maonyesho ya bure watu hawaendi ! Au wamuulize yule mdada wa Arusha Nakaaya Sumari kilichomkuta !
 
@Majebere acha kuvuruga mjadala hapa tunawajadili Profesa J na Mzee Yusuf..sasa hawa unawaingiza vipi! Kwanza nikuulize kweli mnaelekea kuishiwa mbinu kiasi hiki? basi huenda hata ya Mch. Mwakasyege kule Arusha ikawa ni kweli, ngoja tusubiri hukumu ya Lema, tujue mbivu na mbichi.

Hivi ulikusudia nini hapo kwenye red mbona umefanya kosa lilelile kwenye bold hapo?
 
Wakuu wa Fikra, heshima kwenu


Nime inasa hii katika pitapita zangu.Chanzo ni ufa wa mahusiano kati ya wafanya biashara ndogo ndogo(wamachinga) ambao ndiyo wapiga kura wengi na uongozi wa jiji la Mwanza umekuwa ukiongezeka kila kukicha na kufifisha matumaini ya kurirejesha jiji la Mwanza kuwa ngome ya ccm.

Kete ya kuchomeka mameya wa kichina imeonyesha kutokuzaa matunda kwani wakazi wengi jijini Mwanza wameonyesha hasira za wazi kama walivyokaririwa na badhi ya radio za jijini hapa.. na kuashiria kuwepo upigwaji wa kura za hasira tena dhidi ya ccm hapo 2015.

Mkakati uliopo sasa ni kutafuta watu wenye umaarufu wao binafsi na unaokubaliwa na jamii ili iwe rahisi kuwa nadi na wasanii hao ndiyo wanofikiriwa.mmoja atagombea Jimbo la Ilemela na mwingine Nyamagana.Yote hii nikuhakikisha jiji haliwi chini ya wabunge wa upinzani hasa cdm kama ilivyo kwa sasa.

Naendelea kufuatilia kwa karibu undani wa tetesi hizi, nitawajuzeni...ila chanzo changu kimedokeza kuwa baada ya sikuuku ya mwaka mpya 2013, watakuwa wakifanya show za mara kwa mara jijini Mwanza chini ya udhamini wa kigogo mmoja wa NEC-CCM(Jina kapuni kwanza)

Nawasilisha.
najua hapa reference ni kwamba mbona sugu aligombea akashinda sasa angalau sugu alikuwa ameamua kupigania umma lakini hawa kama wanakuja kwa tiketi ya wanyonyaji wasahau kila kitu
 
Mzee Yusuful ndyo yupi huyo? Hawa wazee zamu hii hatutawapigia kura hata kidogo..michango yao bungeni ni hasi! inshort they are outdated, let them go away from politics! waende wakatoe ushauri huko mashambani kilimo kikue..

Mzee Yusuph ni jina na la yule mwimbaji wa taarabu wa kundi la jahazi modern taarabu, sipati picha akiingia bungeni nadhani kuna siku atakuwa anatoa burudani ndani ya bunge
 
Back
Top Bottom