M-mbabe
JF-Expert Member
- Oct 29, 2009
- 13,203
- 23,020
Je, kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii wasanii na watu wengine maarufu wanatoa kauli gani kuhusu Mh Tundu Lissu kushambuliwa na risasi jana?
Uzi huu umeanzishwa specially kwa ajili ya kufuatilia kauli za watu wa jinsi hiyo - tutiririke watu wa Mungu!
Ninaanza hapa chini na nukuu kutoka kwa baadhi ya wanasoka maarufu hapa nchini (Gazeti la Mwananchi leo).
Wachezaji watumia mitandao ya kijamii kumtakia afya njema Lissu.
By Fredrick Nwaka, Mwananchi; fnwaka@mwananchi.co.tz
Dar es Salaam.
Tukio la kupigwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu limewagusa wachezaji mbalimbali.
Wachezaji hao wamekuwa wakutumia akaunti zao za mitandao ya kijamii kumtakia kheri mbunge huyo.
Mbwana Samatta katika ukurasa wake wa Instagram ameeleza mshtuko wake baada ya tukio hilo.
"Hili ni tukio baya, tumuombee mheshimiwa Lissu," ameandika nahodha huyo wa Taifa Stars anayeichezea Genk ya Ubelgiji.
Mshambuliaji wa Simba, Shiza Kichuya aliweka picha ya Lissu kwenye ukurasa wake wa Instagram na kusema anamuomba Mungu ampe nafuu Tundu Lissu.
Mchezaji mwingine aliyeweka picha ya Lissu kwenye ukurasa wake ni kipa wa Simba, Aishi Manula.
Kwa sasa Lissu yuko Nairobi nchini Kenya anakopatiwa matibabu katika Hospitali ya Aga Khan
Uzi huu umeanzishwa specially kwa ajili ya kufuatilia kauli za watu wa jinsi hiyo - tutiririke watu wa Mungu!
Ninaanza hapa chini na nukuu kutoka kwa baadhi ya wanasoka maarufu hapa nchini (Gazeti la Mwananchi leo).
Wachezaji watumia mitandao ya kijamii kumtakia afya njema Lissu.
By Fredrick Nwaka, Mwananchi; fnwaka@mwananchi.co.tz
Dar es Salaam.
Tukio la kupigwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu limewagusa wachezaji mbalimbali.
Wachezaji hao wamekuwa wakutumia akaunti zao za mitandao ya kijamii kumtakia kheri mbunge huyo.
Mbwana Samatta katika ukurasa wake wa Instagram ameeleza mshtuko wake baada ya tukio hilo.
"Hili ni tukio baya, tumuombee mheshimiwa Lissu," ameandika nahodha huyo wa Taifa Stars anayeichezea Genk ya Ubelgiji.
Mshambuliaji wa Simba, Shiza Kichuya aliweka picha ya Lissu kwenye ukurasa wake wa Instagram na kusema anamuomba Mungu ampe nafuu Tundu Lissu.
Mchezaji mwingine aliyeweka picha ya Lissu kwenye ukurasa wake ni kipa wa Simba, Aishi Manula.
Kwa sasa Lissu yuko Nairobi nchini Kenya anakopatiwa matibabu katika Hospitali ya Aga Khan