Wasaliti wa taifa!

ZeMarcopolo

Platinum Member
May 11, 2008
14,017
7,220
Neno fisadi limekuwa likitumika sana siku hizi. Hivi sasa kutokana na extravagant use neno hili limepoteza maana yake. Cha kusikitisha ni kwamba hata humu JF kumekuwa na tabia ya watu kuitana mafisadi kimzaa mzaa tu, mtu anamwita fisadi mtu asiyemfahamu!

Natahadharisha kuwa neno hili likiendelea kutumika ovyo litaendelea kupoteza uzito wake na hata wale mafisadi wa ukweli hawataona soni kuitwa hivyo.

Ndio maana kuanzia sasa nitaacha kulitumia neno fisadi na badala yake mafisadi wote nitakuwa nawaita WASALITI WA TAIFA.
 
Back
Top Bottom