brave one
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 4,876
- 7,366
Joto la upinzani wa matamasha ya music kati ya fiesta na wasafi festival linazidi kupanda kiasi Kila upande unatumia aina yoyote ya promo ili mradi kuvuta watu.
Katika tangazo la clouds msanii mkongwe Fid Q ameonekanda akiwaponda wasafi kwa kuanzisha tamasha hilo
Fid Q amesema "yaani nyie mnasubiri watu wanaongoja si tufanye ndio nao wafanye afu mtulinganishe!? Acheni ufala".
kauli hii imezua mpasuko kwa mashabiki huku wangine wakiponda msanii kuchagua upande.
NB: kuongezeka kwa matamasha na ushindani ni habari njema kwa wasanii kwani kutafanya mifuko yao kutanuka, ni vyema wasanii kuwa makini namna ya kutumika ili kutofungamana na upande wowote, maana wanasema kupe hachagui damu.
Katika tangazo la clouds msanii mkongwe Fid Q ameonekanda akiwaponda wasafi kwa kuanzisha tamasha hilo
Fid Q amesema "yaani nyie mnasubiri watu wanaongoja si tufanye ndio nao wafanye afu mtulinganishe!? Acheni ufala".
kauli hii imezua mpasuko kwa mashabiki huku wangine wakiponda msanii kuchagua upande.
NB: kuongezeka kwa matamasha na ushindani ni habari njema kwa wasanii kwani kutafanya mifuko yao kutanuka, ni vyema wasanii kuwa makini namna ya kutumika ili kutofungamana na upande wowote, maana wanasema kupe hachagui damu.