Wasafi Media ubabaishaji mwingi, sijui ndo ugeni kwenye Tasnia?

Ncha Kali

JF-Expert Member
Sep 19, 2019
14,497
26,986
Mzee kasema tujiandae kupiga shangwe, basi tujiweke sawa.

Leo nipo na Wasafi Media, kuna machache kati ya mengi siyaelewi tusaidiane kuwaweka sawa.

Kuna mifano michache ya ‘Vipindi’ ama ‘shows’ ambazo zimekuwa hazichukui round hewani, ghafla zinapotea na kupisha wengine, hapa tatizo ni maslahi au mikataba magumashi au namna gani?

Kwa mfano Show ya ‘Bongo Dar es Salaam’ ya Dude, ilianza kwa mbwembwe nyingi ghafla ikapotelea kusikojulikana.

Kulikuwa na Show ya vichekesho iliitwa ‘Cheka Point’ ya kina Carpoza (Wanyabe), ishapigwa chini kuna Jambo na Vijambo.

Mifano ipo mingi, unaweza kuongezea, mi naishia hapo.

Hebu wajuzi mtupe mwanga, kuna harufu gani hapa kwenye hii so called mega media baba lao?

Ni kwamba wenye shows wanashindwa kuprove uwezo au magumashi kwenye maslahi?
 
Bado hawajajipanga inabid mejiment ikae ipange vipind vizur maana ni hovyo hovyo


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Microphone check out, tunajaribu tunajaribu. WASAFI bado majaribio, tunatesti mitambo.
 
Tv E ndio mpango. Wao watutengenezee nyimbo bzuri basi

komesha korona
 
Bongo dar es salaam inaenda kwa season
Huwa kuna muda wa kuzalisha program kwa vipindi fulani halafu ukimaliza unairusha hewani inawezekana season ikawa na episode labda 20

Zikiisha hizo then wanapotea kwenda kuzalisha season nyingine itayofuata so ni kawaida
Ni kama kipindi cha keeping up with the Kardashians pale kituo cha E!TV cha USA
 
Bongo dar es salaam inaenda kwa season
Huwa kuna muda wa kuzalisha program kwa vipindi fulani halafu ukimaliza unairusha hewani inawezekana season ikawa na episode labda 20

Zikiisha hizo then wanapotea kwenda kuzalisha season nyingine itayofuata so ni kawaida
Ni kama kipindi cha keeping up with the Kardashians pale kituo cha E!TV cha USA

Asante kwa taarifa.
 
Tatizo wanatamani kuwa top ilihali hawajajipanga... So wanaamini kila kipindi kitawaweka juu kumbe chenga
 
Back
Top Bottom