Was Lowassa right? HDR 2007/2008

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Nimekuwa nikisubiri ripoti hii ya Human Development na hatimaye ndio imetoka. Ukiwasikiliza watawala wetu inaonekana kuwa Taifa letu linapiga hatua kubwa ya maendeleo na wananchi wafurahie! Mgogoro wangu na Lowassa ulianza pale alipodai kuwa Tanzania inapaa, na mimi nikasema kama inapaa basi waliopaa ni viongozi huku wananchi wakiwa wameachwa kipawa wameduwaa!

Mojawapo ya ripoti inayopima maendeleo ya watu (siyo vitu) ni ripoti hii ya Umoja wa Mataifa. Kati ya nchi 177 zilizoangaliwa Tanzania imetoka kuwa nchi ya 162 na kuwa 159.. Je huku ndiko kupaa alikozungumzia Lowassa?

Kwanini baada ya FDI tunazoingiza, sifa tunazopata toka wakubwa n.k mbona inapofika kwenye kupima vinavyopimika hatuonekani? Mbona Uganda wametoka kwenye "Low Human Development" na sasa wako kwenye "Medium Human Development"? What are we doing wrong? Au hizi zote ni njama za wapinzani ambao hawataki kutoa pongezi kwa viongozi wanapofanya vitu vizuri?

Angalia hapa ripoti hizo na ulinganishe mwenyewe
 
Na kwa haraka haraka sidhani kama mtu anaweza kujitokeza hadhanrani kusema kuwa 'nimefanikiwa kutoka 162 kuja 159..we should be ashamed of ourselves!

weel we could be in a 'better' place kama tungeamua kutumia vigezo vyetu wenyewe..laikinu much as we use the so called 'washington consensus' policies, inabidi tukubaliane navyo...kwa maana kwao wanavoelewa umasikini na sisi tunavoelewa nadhani tunatofautiana
 
Tukijipima kwa kuangalia tumekuwa "wa ngapi" kamwe hatutajitendea haki. Suala la kuwa "wa ngapi" linategemea wengine wako wapi. Twaweza kupata nafasi nzuri kwa kigezo hicho, kumbe imetokana na wengine kuporomoka (mfano nchi ambazo zilikuwa stable mwaka jana na mwaka huu zina hali mbaya labda vita ukame nk), sasa hiyo siyo faida. Kukosa kwangu si kupata kwako. Ukifanya mtihani term iliyopita ukapata 70% na term iliyofuata ukipata 40% umepaa au umeporomoka? Kwa kigezo cha "wa ngapi" unaweza kujisifu kuwa umepaa, yaani term iliyopita licha ya kupata 70% kulikuwa na watu 19 wenye zaidi ya hiyo, kwa hiyo ulikuwa wa 20. Term iliyofuata licha ya kupata 40%, ni watu 9 tu waliokuzidi, kwa hiyo ulikuwa wa 10, kwa hiyo umepaa? Kumbe wale 19 waliokuzidi last term wamehama, au walikuwa wagonjwa wakati wa mtihani uliofuata nk. Tuachane na suala la "wa ngapi" tujipime kwa kiwango cha kukua. Kwamba tulikuwa na points 40 mwaka jana, mwaka huu tuna 45, zimeongezeka 5, mwaka ujao tunataka ziongezeke 10 nk, hayo ndio maendeleo, sio suala la "wa ngapi". Maana hata kama nchi zote zikifikia hatua ya juu sana ya maendeleo bado kutakuwa na "wa kwanza" hadi "wa mwisho".
 
Tukijipima kwa kuangalia tumekuwa "wa ngapi" kamwe hatutajitendea haki. Suala la kuwa "wa ngapi" linategemea wengine wako wapi. Twaweza kupata nafasi nzuri kwa kigezo hicho, kumbe imetokana na wengine kuporomoka (mfano nchi ambazo zilikuwa stable mwaka jana na mwaka huu zina hali mbaya labda vita ukame nk), sasa hiyo siyo faida. Kukosa kwangu si kupata kwako. Ukifanya mtihani term iliyopita ukapata 70% na term iliyofuata ukipata 40% umepaa au umeporomoka? Kwa kigezo cha "wa ngapi" unaweza kujisifu kuwa umepaa, yaani term iliyopita licha ya kupata 70% kulikuwa na watu 19 wenye zaidi ya hiyo, kwa hiyo ulikuwa wa 20. Term iliyofuata licha ya kupata 40%, ni watu 9 tu waliokuzidi, kwa hiyo ulikuwa wa 10, kwa hiyo umepaa? Kumbe wale 19 waliokuzidi last term wamehama, au walikuwa wagonjwa wakati wa mtihani uliofuata nk. Tuachane na suala la "wa ngapi" tujipime kwa kiwango cha kukua. Kwamba tulikuwa na points 40 mwaka jana, mwaka huu tuna 45, zimeongezeka 5, mwaka ujao tunataka ziongezeke 10 nk, hayo ndio maendeleo, sio suala la "wa ngapi". Maana hata kama nchi zote zikifikia hatua ya juu sana ya maendeleo bado kutakuwa na "wa kwanza" hadi "wa mwisho".


uzuri ni kuwa kama nchi zote zikiwa zimefikia hatua ya kwanza, hakutakuwa na nchi ambayo iko nyuma na badala yake zitapangwa kialfabeti badala ya jinsi walivyofikia. Ukweli pia ni kuwa kuna vitu ambavyo vinaweza kupimwa kati ya nchi na nchi. Ndio maana Marekani siyo nchi ya kwanza kimaendeleo ya wanadamu (siyo vitu). Ukishakuwa na vigezo vizuri ambavyo vinaweza kupimika kisayansi ni rahisi kujua kama nchi inasonga mbele au inarudi nyuma.
 
Kithuku babuuu Kithuku Duh hii yako kali sana yaani tujipime unene kwa suruali zetu.. au sio?..
Sasa hapa kidogo nimetoka mtupu ikiwa tumepanda kwa sababu baadhi ya nchi zimeshuka kutokana na vita,Ukame na kadhalika ina maana bado tumepanda kimaendeleo hata kama kiwango chetu ni kile kile ama kimepungua kidogo toka cha mwaka jana?..
 
Mh Kithuku,
Nimeshindwa kupata logic ya maelezo yako. Ndani ya maelezo yako naona kama vile unajikanyaga tu bila ya kuwa na hoja ya msingi. Swala lililo wazi ni kwamba idadi ya nchi washiriki ni wale wale, na kama zipo zilizopungua ama kuongezeka basi ni moja ama mbili. Kwa hiyo idadi ya wanafunzi ni ile ile tu, hakuna waliohama. Ukame hauko Tanzania peke yake wala Zimbabwe peke yake, ni swala la nchi nyingi zilizo kusini mwa jangwa la Sahara. Magonjwa na vita ni swala la kawaida kwa nchi za kwetu (Afrika), kwa hiyo bado hilo nalo lisiwe kisingizio cha kufanya vibaya kwenye HDR.

Hata kwenye darasa la wanafunzi vilaza lazima kuwe wa kwanza na wa mwisho, hata darasa la vipanga lazima kuwe na wa kwanza na wa mwisho. Kama kuna zawadi inatolewa kwa mwanafunzi bora, huwa hatuangalii amepata average ya marks ngapi bali ni je amekuwa mwanafunzi wa kwanza? Kwa hiyo swala la Tanzania kuwa ya ngapi bado liko pale pale kwamba tumeshindwa ku-perform hata kama tumelinganishwa na vilaza wenzetu/poor performers, but they are better than us. Kwa kutumia hoja yako unataka kutuambia kwamba HDR is useless, but huyo huyo Lowassa wa kwenu alitumia report ya HDR ya miaka ya nyuma katika kutuonyesha kwamba ndege inapaa, na akawataka wana CCM wasiyumbishwe na kejeri za akina Mwanakijiji (za ndege kupaa) na wapinzani!

Leo kwa kuwa HDR imewaumbua mnakuja na hoja kwamba tusitumie report hiyo kwa kuwa inaweza kuwa ina mislead bali tuangalie tumefanya vipi. Kumbuka kwamba unapojitahidi ku-score more marks na wenzako nao wanafanya hivyo hivyo kama wewe, lengo likiwa ni kuwa bora kuliko wote. Kwa hiyo whether umeongeza point 5 au 10 bado kuna wenzako wanaongeza points 20 au zaidi na matokeo yake unajikuta uko huko huko nyuma.

Hoja muhimu ingekuwa ni kwamba, je Tanzania iko above average? Jibu lake nadhani liko kwenye report hiyo na hivyo kabla ya kutoa comments kwamba tusiangalie tumekuwa wa ngapi tunatakiwa kuisoma report kwa makini na ndipo tuje na hoja kama ya kwako. Sijawahi kusikia Mlimani wameshindwa kupata wanafunzi wa kuanza mwaka wa kwanza eti kwa kuwa hakukuwa na wanafunzi wengi waliopata Div I! Kila mwaka lazima kuna wanafunzi wanaingia Mlimani bila kujali wamepata A's au wamepata makarai!
 
Tuleteeni Tanzania Poverty and Human Development Report 2007 tafadhali. Serikali imeshaitoa rasimu yake kwenye wiki ya umaskini wiki iliyopita. Hapo tutaweza kumwumbua zaidi chotara wa Kimasai

Asha
 
Watu wa WB/IMF wana sababu zao za kutoa hizi ripoti. Kuna watu ambao wanatumia takwimu hizi kufanikisha mambo yao, kama tukiwa wajinga tunaweza kujitazama kwa kutimia kioo cha ripoti hiyo, lakini ukweli wa mambo mengi yanawekwa kwa mehesabu yanayosuit economic interests zao. Kama vile kuthibitisha mikopo na investments ambazo in a long run zinawanufaisha wao zaidi kuliko sisi. Jaribuni kuosma kitabu cha CONFESSIONS OF ECONOMIC HIT MEN
 
Kithuku babuuu Kithuku Duh hii yako kali sana yaani tujipime unene kwa suruali zetu.. au sio?..
Sasa hapa kidogo nimetoka mtupu ikiwa tumepanda kwa sababu baadhi ya nchi zimeshuka kutokana na vita,Ukame na kadhalika ina maana bado tumepanda kimaendeleo hata kama kiwango chetu ni kile kile ama kimepungua kidogo toka cha mwaka jana?..

..kwa ufupi alichosema ni kuwa huwezi kupima kuendelea kwako kwa kutazama nafasi uliyopo kimpangilio wa namba!"kama wengine wamehama"?

..kukua kwa uchumi,kuongezeka kwa ajira,kukua kwa miradi ya maendeleo,kukua kwa standard of living,kukua kwa miundombinu!na mengine mengi,ndio hutoa picha ya kweli ya maendeleo ya nchi na si hizi orodha zinazochukulia toka kwenye orodha zilizokusanywa vibaya!
 
Watu wa WB/IMF wana sababu zao za kutoa hizi ripoti. Kuna watu ambao wanatumia takwimu hizi kufanikisha mambo yao, kama tukiwa wajinga tunaweza kujitazama kwa kutimia kioo cha ripoti hiyo, lakini ukweli wa mambo mengi yanawekwa kwa mehesabu yanayosuit economic interests zao.

..kama nilivyosema hapo juu!hiyo report haitoi picha halisi,mbaya zaidi ni usahihi wa hizo data!

..na mara nyingi data hizi hutumika kutengeneza ajenda zao za kuendelea kututawala!na hivyo kuhalalisha misaada ambayo ukiitizama vizuri ni mashimo marefu!
 
Back
Top Bottom