Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wenye masikio na wamesikia kasoro Nape
Umesema kweli ndugu, ila mimi nataka tuipige ccm shimoni, siyo chini!Ni kweli wahenga walisema sikio la kufa halisikii dawa
hii ilitokana na kuwa kitu kinachokaribia kufa hata ukifanyie nini hakiwezi kufufuka tena
kuna baadhi ya madaktari huwaambia wagonjwa wao moja kwa moja kuwa hawawezi kupona maradhi yanayowakabili na hivyo kuwashauri waanze kuandika wosia.
Kutokana na hali ilivyo sasa chama cha ccm kinatakiwa kianze kuandika wosia wa jinsi maziko yake yanavyotakiwa kuwa.
Kwa miaka yote zaidi ya 50 wameshindwa kutoa matumaini kwa watanzania,
wameshindwa kuonyesha upi ni uhai wa nchi
hiyo ni dalili ya juu kabisa ya kufa kwa chama cha siasa.
Watanzania tuipige chini ccm 2015
Mpaka sasa wameshakuwa wapinzani!Wakati anaohijiwa na mwandishi wa TBC1 Asumpta Masoi, Jaji Joseph Warioba alisema kuwa kama CCM haitamaliza matatizo yake ya ndani basi ijiandae kukabiliana na hali ngumu huko mbele.
Amesema kuwa, kwa kuwa tumeukubali mfumo wa vyama vingi na pia kwa kuwa watu wengine wameanza kuichoka CCM na wapo pia wanaotaka mabadiliko, CCM itegemee kuwa mabadiliko yanatatokea tu na yataiweka kando. Na kwamba wasipoiangalia upya dira na itikadi za chama basi itakuwa vingumu kupona!
Kwa jinsi ninavyowajua CCM, watakurupuka kumtukana Warioba badala ya kuangalia kile alichokisema, ingawa hakusema jambo lolote jipya!
kazi ipo watanzania tujiandae kwa mabadiliko hakuna wakutuletea isipokua ni sisi wenyewe tusiishie kuonge jamvini tu