abdulahsaf
JF-Expert Member
- Aug 31, 2010
- 858
- 130
[h=1][/h]Written by Ahmed Omar Khamis // 12/12/2012 // Habari // 1 Comment
CCM wanaufanya mchakato ni wao, mali yao.
Serikali inawapa uso kutekeleza vitimbi viovu dhidi ya mchakato huo.
Utowaji wa maoni katika wilaya ya Mjini ratiba imepanga vituo vyote vya kutoa maoni jirani na matawi imara ya CCM ili kutoa urahisi kwa CCM kuuteka nyara
mchakato katika wilaya hii. Wakiwa katika matawi yao hayo kiasi cha wanachama 70 hivi hulala hapo tawini huku wakigharamiwa magodoro ya kulalia na vyakula. Kama hilo halitoshi CCM hulazimisha kutumika kwa vifaa vyao vya jukwaa na viti vya kukalia. Mara wakifika katika eneo la kutoa maoni hupanga viti vyao na mabenchi kwa utaratibu wao na kukalia viti hivyo. Baadhi ya viti hua vitupu na huwekwa ili kuwazuilia nafasi wenzao watakapokuja baadae. Haya ndio yaliyojitokeza leo asubuhi katika shehia ya M/Matarumbeta Jangombe.Hata hivyo wananchi ambao walidhaniwa kuwa ni wafuasi wa mkataba walifukuzwa na kupigwa huku wakiambiwa wende Pemba wakatoe maoni M/Matarumbeta pana wenyewe.
Baada ya wanamkataba kuchachamaa sheha akishirikiana na wana CCM walipiga simu polisi na ghafla gari mbili za FFU zilifika. Mara baada ya kufika waliwasikiliza wana CCM madai yao na ndipo wao waliposaidia kuwasogeza nyuma zaidi wanamkataba. Vijana wawili walijaribu kugoma na kuhoji kwa nini polisi wanafanya hivyo lakini walisombwa na kuingizwa katika defennder na kuchukuliwa na pingu mikononi.
Hivi mchana wa leo kiasi cha saa 8:00 tume ya mabadiliko ya katiba itakuwepo katika shehia ya Jangombe. Nilifika katika kituo hicho kiasi cha 5:00 asubuhi ili kuona maandalizi yanavyoendeleav katika kituo hichi. Kinyume na kawaida nilikuta jukwaa ambalo ninatarajiwa kutumiwa na tume linaendelea kujengwa katika uwanja finyu ulio ndani ya skuli hiyo na kuachwa viwanja kadhaa vilivyopo nje ya skuli hiyo. Vifaa vya jukwaa na viti ni mali ya CCM. Lengo la kuliweka jukwaa ndani ya uwanja finyu wa skuli bila shaka ni kujificha ili wanamkataba wababaike wasijue kituo kilipo na wakifika wakimbilie katika uwanja wa nje wa skuli na hivyo wana CCM wawahi nafasi zote za mbele.Ghafla kundi la wanamkataba liliwasili katika eneo hilo na kuingia ndani ya geti la skuli ili kuwahi kukaa katika foleni. Mara tu sura za wanamkataba zilipofahamika, sheha wa shehia hiyo akishirikiana na wana CCM walitumia ubavu kuwasukuma huku wakirushiana makonde na wana mkataba na kufanikiwa kulifunga geti la skuli hiyo. Wanamkataba wachache waliwahi kupenya lakini wengi wao kubaki nje. Kama kawaida yangu nilisogea na kupiga picha ya tukio hilo lakini ghafla kundi la samaki lilinijia ghafla na makelele ya matusi na kutishia usalama wangu. Hali hadi sasa ipo hivyo katika kituo hichi
Zoezi la utowaji maoni ya katiba mpya linazidi kuingia dosari na kuelekea kuharibika kabisa. Mchana huu zoezi hili linatarajia kufanyika katika kituo cha skuli ya Kidongo chekundu. Katika kuendeleza vitendo vya ubabe na kuuteka nyara kila mchakato wa kidemkrasia, CCM kwa mashirikiano na sheha huku wakipata ulinzi na uungwaji mkono wa jeshi la polisi wameamua kuifunga milango ya geti la kituo hicho na kutowaruhusu kuingia wale wote wanaodhaniwa kuwa na maoni ya muungano wa mkataba. Sheha wa shehia ya Jangombe akishirikiana na wana CCM wamebaki ndani ya geti hilo wakiwatambua wale ambao wana mawazo kama yao na kuwaruhusu kupita.
Vijana wanaozuiliwa kuingia ndani ya geti hujaribu kuhoji na kutaka kuingia kwa nguvu lakini jeshi la polisi humvamia kila anaejaribu kuingia kwa nguvu, kumpa kipigo na kumpeleka kiuoa cha polisi na pingu mkononi. Hali ni mbaya sana na inatisha. Sijui kama huu ni utowaji maoni tena unaozingatia uhuru, haki na demokrasia.
CCM wanaufanya mchakato ni wao, mali yao.
Serikali inawapa uso kutekeleza vitimbi viovu dhidi ya mchakato huo.
Utowaji wa maoni katika wilaya ya Mjini ratiba imepanga vituo vyote vya kutoa maoni jirani na matawi imara ya CCM ili kutoa urahisi kwa CCM kuuteka nyara
mchakato katika wilaya hii. Wakiwa katika matawi yao hayo kiasi cha wanachama 70 hivi hulala hapo tawini huku wakigharamiwa magodoro ya kulalia na vyakula. Kama hilo halitoshi CCM hulazimisha kutumika kwa vifaa vyao vya jukwaa na viti vya kukalia. Mara wakifika katika eneo la kutoa maoni hupanga viti vyao na mabenchi kwa utaratibu wao na kukalia viti hivyo. Baadhi ya viti hua vitupu na huwekwa ili kuwazuilia nafasi wenzao watakapokuja baadae. Haya ndio yaliyojitokeza leo asubuhi katika shehia ya M/Matarumbeta Jangombe.Hata hivyo wananchi ambao walidhaniwa kuwa ni wafuasi wa mkataba walifukuzwa na kupigwa huku wakiambiwa wende Pemba wakatoe maoni M/Matarumbeta pana wenyewe.
Baada ya wanamkataba kuchachamaa sheha akishirikiana na wana CCM walipiga simu polisi na ghafla gari mbili za FFU zilifika. Mara baada ya kufika waliwasikiliza wana CCM madai yao na ndipo wao waliposaidia kuwasogeza nyuma zaidi wanamkataba. Vijana wawili walijaribu kugoma na kuhoji kwa nini polisi wanafanya hivyo lakini walisombwa na kuingizwa katika defennder na kuchukuliwa na pingu mikononi.
Hivi mchana wa leo kiasi cha saa 8:00 tume ya mabadiliko ya katiba itakuwepo katika shehia ya Jangombe. Nilifika katika kituo hicho kiasi cha 5:00 asubuhi ili kuona maandalizi yanavyoendeleav katika kituo hichi. Kinyume na kawaida nilikuta jukwaa ambalo ninatarajiwa kutumiwa na tume linaendelea kujengwa katika uwanja finyu ulio ndani ya skuli hiyo na kuachwa viwanja kadhaa vilivyopo nje ya skuli hiyo. Vifaa vya jukwaa na viti ni mali ya CCM. Lengo la kuliweka jukwaa ndani ya uwanja finyu wa skuli bila shaka ni kujificha ili wanamkataba wababaike wasijue kituo kilipo na wakifika wakimbilie katika uwanja wa nje wa skuli na hivyo wana CCM wawahi nafasi zote za mbele.Ghafla kundi la wanamkataba liliwasili katika eneo hilo na kuingia ndani ya geti la skuli ili kuwahi kukaa katika foleni. Mara tu sura za wanamkataba zilipofahamika, sheha wa shehia hiyo akishirikiana na wana CCM walitumia ubavu kuwasukuma huku wakirushiana makonde na wana mkataba na kufanikiwa kulifunga geti la skuli hiyo. Wanamkataba wachache waliwahi kupenya lakini wengi wao kubaki nje. Kama kawaida yangu nilisogea na kupiga picha ya tukio hilo lakini ghafla kundi la samaki lilinijia ghafla na makelele ya matusi na kutishia usalama wangu. Hali hadi sasa ipo hivyo katika kituo hichi
Zoezi la utowaji maoni ya katiba mpya linazidi kuingia dosari na kuelekea kuharibika kabisa. Mchana huu zoezi hili linatarajia kufanyika katika kituo cha skuli ya Kidongo chekundu. Katika kuendeleza vitendo vya ubabe na kuuteka nyara kila mchakato wa kidemkrasia, CCM kwa mashirikiano na sheha huku wakipata ulinzi na uungwaji mkono wa jeshi la polisi wameamua kuifunga milango ya geti la kituo hicho na kutowaruhusu kuingia wale wote wanaodhaniwa kuwa na maoni ya muungano wa mkataba. Sheha wa shehia ya Jangombe akishirikiana na wana CCM wamebaki ndani ya geti hilo wakiwatambua wale ambao wana mawazo kama yao na kuwaruhusu kupita.
Vijana wanaozuiliwa kuingia ndani ya geti hujaribu kuhoji na kutaka kuingia kwa nguvu lakini jeshi la polisi humvamia kila anaejaribu kuingia kwa nguvu, kumpa kipigo na kumpeleka kiuoa cha polisi na pingu mkononi. Hali ni mbaya sana na inatisha. Sijui kama huu ni utowaji maoni tena unaozingatia uhuru, haki na demokrasia.