Warioba atetea mchakato wa katiba, akana tuhuma zilizotolewa na Jukwaa la Katiba

Mwana Mpotevu

Platinum Member
Sep 7, 2011
3,295
2,500
katika mkutano wake na wanahabari Warioba amesema sio kweli kuwa wanalipua na kuupeleka puta mchakato huo. Amesema kuwa wanafuata taratibu walizojiwekea na watu wote watafikiwa.

Warioba anasema kila awamu watu wanaotoa maoni na kuhudhuria kwenye mikutano wanaongezeka
 
sasa atasemaje na yeye ndiye mhusika mkuu?

Kwanza hata hayo maoni yanakuwa documented kwa mtindo upi?

Kuhakiki kiichowekwa kwenye katiba ndio kilichosema na wananchi

siamini tume hii kabisa.

Kama mazoezi mengine yote kwa uzoefu huwa muda hautoshi, wenyewe muda umewatosha kweli?
 
sasa atasemaje na yeye ndiye mhusika mkuu?

Kwanza hata hayo maoni yanakuwa documented kwa mtindo upi?

Kuhakiki kiichowekwa kwenye katiba ndio kilichosema na wananchi

siamini tume hii kabisa.

Kama mazoezi mengine yote kwa uzoefu huwa muda hautoshi, wenyewe muda umewatosha kweli?

Mzee huyu anasema sio mara ya kwanza kwa hili kufanyika Tanzania na ana uzoefu nalo kwahiyo muondoe shaka atafanya kwa ufanisi na maoni yenu yatazingatiwa

LABDA
 
wana uzoefu wa kuratibu uwekaji wa viraka kwenye katiba.

Anyway, wataongeza tu, ngoja tuone.

Mzee huyu anasema sio mara ya kwanza kwa hili kufanyika Tanzania na ana uzoefu nalo kwahiyo muondoe shaka atafanya kwa ufanisi na maoni yenu yatazingatiwa

LABDA
 
wana uzoefu wa kuratibu uwekaji wa viraka kwenye katiba.

Anyway, wataongeza tu, ngoja tuone.

Kinachonipa mashaka, wanaweza kuweka mambo wanayoyataka wao maana kauli ya Dr Sheni zenji Juzi ilikuwa ni kama kauli ya serikali na msimamo wao kuhusu muungano na sio zaidi ya hivyo.

Na kama wakiweka wanayoyataka wao, rasimu ikija tukiikata sisi wananchi, maana yake tunarudi kwenye katiba ya zamani na mchakato unaishia hapo si vinginevyo. nahisi kiza mbele ya safari
 
Kinachonipa mashaka, wanaweza kuweka mambo wanayoyataka wao maana kauli ya Dr Sheni zenji Juzi ilikuwa ni kama kauli ya serikali na msimamo wao kuhusu muungano na sio zaidi ya hivyo.

Na kama wakiweka wanayoyataka wao, rasimu ikija tukiikata sisi wananchi, maana yake tunarudi kwenye katiba ya zamani na mchakato unaishia hapo si vinginevyo. nahisi kiza mbele ya safari

Upo sahihi kabisa, mchakato huu una giza totoro mbeleni, katika maeneo mawili , iwapo serikali itakataa mapendekezo ya wananchi na kuleta ya kwao , basi kuna uwezekano wa kura ya kukataa katiba kupigwa na hapo ndio mwisho wa yote, kwa ccm ya jakaya, wala haoni tabu kwa hilo la pili kutokea, serikali ya business as usual a.k.a banana republic
 
Upo sahihi kabisa, mchakato huu una giza totoro mbeleni, katika maeneo mawili , iwapo serikali itakataa mapendekezo ya wananchi na kuleta ya kwao , basi kuna uwezekano wa kura ya kukataa katiba kupigwa na hapo ndio mwisho wa yote, kwa ccm ya jakaya, wala haoni tabu kwa hilo la pili kutokea, serikali ya business as usual a.k.a banana republic

Inabidi tuombe mungu hawa watu wachukue kweli maoni yetu na wasitupige changa la macho kwa kuweka maoni yao binafsi
 
Inabidi tuombe mungu hawa watu wachukue kweli maoni yetu na wasitupige changa la macho kwa kuweka maoni yao binafsi

Sasa kama wanataratibu walizojiwekea wao wenyewe, hii katiba wanayo iandaa itakuwa ya wananchi au itakuwa yao kwa taratibu zao na matakwa yao. Nisaidieni ama sijamuelewa vizuri.
 
Sasa kama wanataratibu walizojiwekea wao wenyewe, hii katiba wanayo iandaa itakuwa ya wananchi au itakuwa yao kwa taratibu zao na matakwa yao. Nisaidieni ama sijamuelewa vizuri.

Mkuu,

hawa jamaa wanakusanya maoni ya watu kisha wataandaa rasimu ya katiba. baadae hiyo rasimu tutaipigia kura ili kuikubali wananchi ama kuikataa.

sasa kama wakiweka maoni yao binafsi ama maoni ya waliowapa kazi (serikali) na kusahau kile wananchi wanachotaka, ni kwamba huenda tukaikataa sisi wananchi. na tukiikataa ni kwamba shughuli imekwisha tunarudi kwenye katiba ya zamani na kamati unakuwa imemaliza jukumu lake na shughuli inakwisha.

That's why nikasema tuombe mungu hawa akina Warioba wasiweke yale wanayoyataka wao na yale tunayotaka sisi wananchi wakayatosa
 
Inabidi tuombe mungu hawa watu wachukue kweli maoni yetu na wasitupige changa la macho kwa kuweka maoni yao binafsi

Hapa mungu anaingiaje?

Viongozi ni wabishi na pia ni wateka hoja za mabadiliko.
Wananchi ni "kichwa cha mwendawazimu", wanatamani mabadiliko bila kuyapigania na kuyasimamia.

Ninavyojua ni kuwa "viongozi" huapa kwa kushika biblia na misahafu wanapokabidhiwa dhamana. Kama wangesimamia viapo vyao basi nchi hii ingekuwa nchi ya maziwa na asali lakini walalahoi tunaishia kugawiwa ahadi hewa na umasikini.

Hata hizo tume ambazo ziliundwa kuweka viraka katiba basi waliweka vile viraka vinavyoibeba na kuibakisha CCM kwenye usukani. Kwa kauli za Jaji Warioba, tusitegemee Katiba mpya inayotokana na mawazo ya wananchi...lakini zaidi tusijidanganye kuwa itakuwa tayari 2014 ili iweze kutumika 2015.

Jukwaa la katiba limetoa wazo la kubadili baadhi ya sheria ,hasa sheria na vipengele vya kuunda Tume huru ya uchaguzi. Vyama vya upinzani bado havioni umuhimu wa hili. Tutasikia wanalalamika baada ya uchaguzi...tumechakachuliwa...kura zimechakachuliwa...matokeo yamechakachuliwa.

Kujaza mikutano kwa nguvu ya umma haitoshi na hasa kama umma wenyewe unategemea "viongozi" ndio wasimamie mageuzi.

Kwa ukimya na ugoi goi wa vyama vya upinzani juu ya kuundwa kwa Tume huru ya uchaguzi ni wazi, inawaacha CCM katika kukenua na kufurahia utekaji wa hoja ya Katiba mpya na kucheza na karata zao kwa ustadi.

Wakati ni mwamuzi bora, ifikapo 2014 tutaulizana iko wapi ile katiba mpya itokanayo na mawazo ya wananchi?

Kama haitakuwepo, basi kweli, kuanzia hapo itabidi tuombe mungu!!!!! kama ilivyo rai ya Mwana Mpotevu.
 
Back
Top Bottom