GHIBUU
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 4,432
- 3,006
Warioba anajichanganya mwenyewe, anasema Serikali mbili malalamiko yanaendelea kujitokeza kila kukicha , vilele anasema wanaohitaji Serikali tatu wasijidanganye kuwa zikianzishwa kero za Muungano hazitokuwapo . Amezungumzia kero kwa njia mblili zinazozungumzwa bila ya kutoa mawazo ya njia ipi itakuwa bora , au ndio SIRI KALI
Sasa warioba kama anaogopa serikali tatu za changamoto jee muungano wa EAC hauna changamoto kwa TZ ?
Mimi napinga nae kwa kaulizake kwa kusema kuwa viongozi ndio wanaotaka serikali 3 kwa maslahi yao ya kisiasa,sio kweli,wewe warioba kama wataka kujua nani anaetaka seriakli tatu lete kura ya maoni,zanzibar kuwe na chombo huru cha kukusanya maoni kwa upande wetu,na tanganyika vile vile,utapta jibu sahihi la muungano kama tunautaka au hatuutaki,kama ni serikali tatu au 2.
Habari kamili hii hapa
na Betty Kangonga. WAZIRI Mkuu mstaafu, Joseph Warioba, amesema tatizo la Muungano linasababishwa na mamlaka zinazogombea madaraka na si wananchi.
Warioba ambaye alikuwa akizungumza kupitia Televisheni ya Taifa (TBC), alisema kuwa muungano uliopo bado ni imara lakini wanaohitaji madaraka ndiyo wanaoufanya uonekane na matatizo.
Alisema wale wanaogombea madaraka wanapaswa kuchukua hatua ili isifike sehemu matatizo hayo yakawaletea shida wananchi.
Warioba alisema wapo baadhi yao wanatoa sababu kuwa kuanzishwa kwa serikali tatu kunaweza kumaliza kero ya muungano, jambo alilosema kuwa halina ukweli wowote.
Kwa mujibu wa Warioba, uwepo wa serikali mbili malalamiko yanaendelea kujitokeza kila kukicha, hivyo alishauri kuwa wanaohitaji serikali tatu wasijidanganye kuwa zikianzishwa kero za muungano hazitakuwepo tena.
Wapo wanaohitaji serikali tatu na kwamba wanaona hilo ndilo jawabu, hawajiulizi juu ya je serikali tatu hazitakuwa na changamoto zake? Na kama zikija, hizo changamoto zinamalizwaje, alihoji Warioba.
Akizungumzia kuhusu Bunge, Warioba alisema Bunge la sasa limeanza vibaya na halitoi mfano mzuri, hata lugha inayotumiwa na viongozi hao alidai sio ya staha bali ni ya kukejeliana.
Alisema Bunge limekuwa la fujo, hatua inayowafanya wananchi mitaani kuambiana kuwa iwapo unahitaji burudani basi ni bora uangalie Bunge.
Wananchi wanaambiana kuwa kama unataka burudani angalia Bunge maana unakuta malumbano hata vyama vilivyopo huoni msimamo wake sijui linaonyesha mfano gani, lazima wachukue hatua, alieleza.
Warioba alisema kuwa anaamini wabunge watakuwa wamesikia maoni ya wananchi, hivyo wanachotakiwa ni kutumia vizuri kanuni ili kurudisha nidhamu iliyopotea.
Alisema Bunge lazima lichukue maamuzi magumu pamoja na kufuata maadili na ikiwa watafanya hivyo, alisema watarudisha hamu kwa wananchi ya kulitazama Bunge hilo.
Waziri Mkuu huyo mstaafu alisema wakati wa chama kimoja wananchi walikuwa wanapenda kipindi cha Bunge kwani walitenga muda wao na kusikiliza kupitia redio, bali kwa sasa teknolojia imekuwa hivyo wanajua kinachoendelea.
Alisema pamoja na kuwepo kwa mfumo wa vyama vingi, lakini Bunge limeweza kufanyakazi nzuri, kwa madai kuwa matatizo ya nchi ni magumu lakini Bunge la mfumo huo limejitahid
Sasa warioba kama anaogopa serikali tatu za changamoto jee muungano wa EAC hauna changamoto kwa TZ ?
Mimi napinga nae kwa kaulizake kwa kusema kuwa viongozi ndio wanaotaka serikali 3 kwa maslahi yao ya kisiasa,sio kweli,wewe warioba kama wataka kujua nani anaetaka seriakli tatu lete kura ya maoni,zanzibar kuwe na chombo huru cha kukusanya maoni kwa upande wetu,na tanganyika vile vile,utapta jibu sahihi la muungano kama tunautaka au hatuutaki,kama ni serikali tatu au 2.
Habari kamili hii hapa
na Betty Kangonga. WAZIRI Mkuu mstaafu, Joseph Warioba, amesema tatizo la Muungano linasababishwa na mamlaka zinazogombea madaraka na si wananchi.
Warioba ambaye alikuwa akizungumza kupitia Televisheni ya Taifa (TBC), alisema kuwa muungano uliopo bado ni imara lakini wanaohitaji madaraka ndiyo wanaoufanya uonekane na matatizo.
Alisema wale wanaogombea madaraka wanapaswa kuchukua hatua ili isifike sehemu matatizo hayo yakawaletea shida wananchi.
Warioba alisema wapo baadhi yao wanatoa sababu kuwa kuanzishwa kwa serikali tatu kunaweza kumaliza kero ya muungano, jambo alilosema kuwa halina ukweli wowote.
Kwa mujibu wa Warioba, uwepo wa serikali mbili malalamiko yanaendelea kujitokeza kila kukicha, hivyo alishauri kuwa wanaohitaji serikali tatu wasijidanganye kuwa zikianzishwa kero za muungano hazitakuwepo tena.
Wapo wanaohitaji serikali tatu na kwamba wanaona hilo ndilo jawabu, hawajiulizi juu ya je serikali tatu hazitakuwa na changamoto zake? Na kama zikija, hizo changamoto zinamalizwaje, alihoji Warioba.
Akizungumzia kuhusu Bunge, Warioba alisema Bunge la sasa limeanza vibaya na halitoi mfano mzuri, hata lugha inayotumiwa na viongozi hao alidai sio ya staha bali ni ya kukejeliana.
Alisema Bunge limekuwa la fujo, hatua inayowafanya wananchi mitaani kuambiana kuwa iwapo unahitaji burudani basi ni bora uangalie Bunge.
Wananchi wanaambiana kuwa kama unataka burudani angalia Bunge maana unakuta malumbano hata vyama vilivyopo huoni msimamo wake sijui linaonyesha mfano gani, lazima wachukue hatua, alieleza.
Warioba alisema kuwa anaamini wabunge watakuwa wamesikia maoni ya wananchi, hivyo wanachotakiwa ni kutumia vizuri kanuni ili kurudisha nidhamu iliyopotea.
Alisema Bunge lazima lichukue maamuzi magumu pamoja na kufuata maadili na ikiwa watafanya hivyo, alisema watarudisha hamu kwa wananchi ya kulitazama Bunge hilo.
Waziri Mkuu huyo mstaafu alisema wakati wa chama kimoja wananchi walikuwa wanapenda kipindi cha Bunge kwani walitenga muda wao na kusikiliza kupitia redio, bali kwa sasa teknolojia imekuwa hivyo wanajua kinachoendelea.
Alisema pamoja na kuwepo kwa mfumo wa vyama vingi, lakini Bunge limeweza kufanyakazi nzuri, kwa madai kuwa matatizo ya nchi ni magumu lakini Bunge la mfumo huo limejitahid