Tunzo
JF-Expert Member
- Feb 1, 2013
- 4,017
- 2,291
Nimekua nikifanya shuguli za udalali wa nyumba, magari, viwanja nk kwa mda sasa hasa kwa kutangaza hapa JF, Zoom, Instagram na kwingine, Kila kazi ina changamoto zake.
Leo nimeamua niongelee swala la nyumba hasa hapa jijini DSM, kwa kipindi kirefu madalali tumekua msaada mkubwa wa kuwatafutia wateja nyumba na wa kuwaunganisha na wenye nyumba, sikatai kuna ambao ni waaminifu na wengine si waaminifu,
View attachment 701331
Leo kuna swala nataka niwahusie wenye nyumba za kupangisha, hakuna asiejua hali ya uchumi kwa sasa, vyuma vimekaza, hata kama basi ni hivyoo basi kodi zenu ziendane na nyumba halisi, kuna wanaosema eti madalali wanapandisha bei ili wapate chochote, la hasha, dalali tunafurahi pale mteja anapopata nyumba anipe ya mwezi, mimi niko radhi kama nyumba nibya 400k nikienda na mteja nimbembelezee hata apate kwa 350k nipate yangu ya mwezi, mana madalali tupo wengi siku hizi, mteja wangu asipoichukua basi badae naweza nisiikute.
Ila changamoto ni pale mwenye nyumba anakuambia umtaftie mteja anakutajia dau la kodi kwa mwezi ambalo haliendani hata na nyumba yenyewe, unakuta hata mm dalali naangalia ile nyumba hadhi yake na seheme ilipo ni shilingi 200k ila mwenye nyumba anakuambia 350k, unamshauri bosi kua fanya hata 200k anakujibu ni heri ikae, na nikweli inakaa hata miezi sita ndio anaanza kukurupuka!
Kusema kweli kuna nyumba ambazo ziko ovyo sana ila hiyo kodi hata mm nikimpeleka mteja roho inanisuta kua nampotezea mteja mda wake, Ila ukweli kwa sasa ni kwamba nyumba nyingi kodi si rafiki, nyumba ya vyumba viwili ukitaka mteja aridhike basi mpeleke ya kuanzia 300,000 na kuendelea,hapo naongelea maeneo ya, ubungo,kimara,knyama,makumbusho, kinondoni, mwenge, na maeneo kama haya, yani hata huko boko na tegeta!,
Yani kwa sasa hata ukitaka chumba na sebule ya 200,000k kupata ya kuridhisha ni kazi! Mfano mwaka jana kama mwezi wa nne kuna mteja mikocheni alifika kodi Dola 1500 kwa mwezi, mwenye nyumba alikomaa Dola 2000, basi jamaa akaacha, ile nyumba mpaka leo anakaa mfanyakazi wa kuilinda, hata 1000$ hapati tena,
Ushauri wangu kwa wenye nyumba za kupanga Dar, acheni kukomaa na bei zenu, mnatupa kazi kubwa sisi tunaowatafutia wateja, hata kama mteja alietoka alikua analipa 300k ukipata mteja yupo tayari kulipa hata 270k na yupo serious chukueni mpunga kuliko nyumba ikae miezi 6,
Pia angalieni pia kodi zenu, angalieni kwa upande wenu je hiyo kodi ya 500k kwenye hiyo nyumba yako ingekua wewe unaepanga ungeiridhia? Nyumna nyingi za 400k basi uhalisia wake nyingi ni 300k, angaliene uhalisia wa kodi zenu na nyumba!
Nawasilisha! Povu ruksa
Leo nimeamua niongelee swala la nyumba hasa hapa jijini DSM, kwa kipindi kirefu madalali tumekua msaada mkubwa wa kuwatafutia wateja nyumba na wa kuwaunganisha na wenye nyumba, sikatai kuna ambao ni waaminifu na wengine si waaminifu,
View attachment 701331
Leo kuna swala nataka niwahusie wenye nyumba za kupangisha, hakuna asiejua hali ya uchumi kwa sasa, vyuma vimekaza, hata kama basi ni hivyoo basi kodi zenu ziendane na nyumba halisi, kuna wanaosema eti madalali wanapandisha bei ili wapate chochote, la hasha, dalali tunafurahi pale mteja anapopata nyumba anipe ya mwezi, mimi niko radhi kama nyumba nibya 400k nikienda na mteja nimbembelezee hata apate kwa 350k nipate yangu ya mwezi, mana madalali tupo wengi siku hizi, mteja wangu asipoichukua basi badae naweza nisiikute.
Ila changamoto ni pale mwenye nyumba anakuambia umtaftie mteja anakutajia dau la kodi kwa mwezi ambalo haliendani hata na nyumba yenyewe, unakuta hata mm dalali naangalia ile nyumba hadhi yake na seheme ilipo ni shilingi 200k ila mwenye nyumba anakuambia 350k, unamshauri bosi kua fanya hata 200k anakujibu ni heri ikae, na nikweli inakaa hata miezi sita ndio anaanza kukurupuka!
Kusema kweli kuna nyumba ambazo ziko ovyo sana ila hiyo kodi hata mm nikimpeleka mteja roho inanisuta kua nampotezea mteja mda wake, Ila ukweli kwa sasa ni kwamba nyumba nyingi kodi si rafiki, nyumba ya vyumba viwili ukitaka mteja aridhike basi mpeleke ya kuanzia 300,000 na kuendelea,hapo naongelea maeneo ya, ubungo,kimara,knyama,makumbusho, kinondoni, mwenge, na maeneo kama haya, yani hata huko boko na tegeta!,
Yani kwa sasa hata ukitaka chumba na sebule ya 200,000k kupata ya kuridhisha ni kazi! Mfano mwaka jana kama mwezi wa nne kuna mteja mikocheni alifika kodi Dola 1500 kwa mwezi, mwenye nyumba alikomaa Dola 2000, basi jamaa akaacha, ile nyumba mpaka leo anakaa mfanyakazi wa kuilinda, hata 1000$ hapati tena,
Ushauri wangu kwa wenye nyumba za kupanga Dar, acheni kukomaa na bei zenu, mnatupa kazi kubwa sisi tunaowatafutia wateja, hata kama mteja alietoka alikua analipa 300k ukipata mteja yupo tayari kulipa hata 270k na yupo serious chukueni mpunga kuliko nyumba ikae miezi 6,
Pia angalieni pia kodi zenu, angalieni kwa upande wenu je hiyo kodi ya 500k kwenye hiyo nyumba yako ingekua wewe unaepanga ungeiridhia? Nyumna nyingi za 400k basi uhalisia wake nyingi ni 300k, angaliene uhalisia wa kodi zenu na nyumba!
Nawasilisha! Povu ruksa