#COVID19 Waraka wa wazi kwa Marais wetu Wastaafu kuhusiana na hali ya Corona nchini

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,823
35,827
Kwenu marais wetu Wastaafu, Mwinyi, Mkapa na rais Kikwete.

Kwa heshima na taadhima inafikirisha kuwaandikia waraka huu baada ya kuwa kwa dhati kabisa, njia nyingi zimejaribiwa kushauri, kuhimiza, kuomba, kuisihi nk ili kuwepo mtizamo tofauti kuhusiana na ugonjwa huu.

Nchi hii ni yetu sote kiasi kuwa kwa yeyote yule, awe mkubwa au mdogo kunyamaza kimya tu wakati ni wazi kuwa labda tunakoelekea sasa siko, siyo jambo ambalo tunaweza kulichagua kama moja ya uwezekano tena.

Waheshimiwa katika nyakati tofauti mmewahi kupokea hatamu za serikali na kuiongoza nchi hii pendwa kama watakavyo kuja na kutoka wengine kwa njia za amani. Siyo siri kuwa kama marais wastaafu nafasi yenu ya kulitumikia taifa hili ingalipo. Ni wazi kuwa, katu marehemu baba wa taifa (rip) asingelikubali kuliacha taifa hili ambalo limekuwa la kupigiwa mfano siku zote kuangamia.

Waheshimiwa, msiliache taifa hili kuangamia na ugonjwa huu huku mkiangalia tu. Mnayo nafasi ya kuliunganisha taifa hili kuwa moja ili kwa pamoja tukaishinda Corona kwa salama.

Shime waheshimiwa msilinyime taifa hili hekima wala busara zenu, ambazo kwa hakika zinahitajika sana kwa sasa labda kuliko kipindi kingine chochote kilichowahi kupita.

Kwa umoja wenu kama wananchi wa nchi hii au katika nafasi zenu ka mtanzania mmoja mmoja mnayo nafasi ya kushauriana na mheshimiwa rais kwa niaba yetu sisi wananchi.

Umoja wetu utokanao na kushawishiana kwa nguvu za hoja si hoja za nguvu utatuvusha katika vita hivi.

Kama watanzania tunastahili kuushinda ugonjwa huu kama jambo la dharura kweli kweli vinginevyo kama ilivyo wazi, maisha ya wengi wetu yako hatarini mno.

Mungu ibariki Tanzania. Mungu tujalie salama tunavyomuunga kupambana na ugonjwa huu.

Nawasilisha.
 
Sasa wao watafanya nini? Washauri kuhusu nini labda? au watoe suluhu ipi? ukiona kimya jua na wao hawana majibu
 
Taifa gani linaangamia? Labda hapo ufipa

Wakati wa kikwete mlisema kikwete ameuza Nchi

Nyie Ni watu wakuwekwa kwenye kundi la mental disorders

Wewe ni zwazwa kuliko msukule. Unadhani kwa vile akili yako iko kwenye siasa basi kila mtu ni CCM au CHADEMA au chama fulani?

Au nyie ni mumiani mnaojipatia damu au nyama ya kula kwa kila mfu? Watu wa namna gani msiokuwa na chembe ya huruma nyie?

Huo uchadema unausomea wapi, msukule wahedi wee!
 
Taifa gani linaangamia? Labda hapo ufipa

Wakati wa kikwete mlisema kikwete ameuza Nchi

Nyie Ni watu wakuwekwa kwenye kundi la mental disorders

Hulijui taifa linaloangamia? Au bado ungali na maluweluwe ya kujifukiza nyungu?

Kwa mawazo yako mmeliokoa taifa na maangamizi ya ugonjwa huu kwa kupiga nyungu?

Hivi misukule nyie ni binadamu kama wengine?
 
Hatuombi mabaya lakini corona haichagui nyazifa ya mtu,Tunapopaza sauti ni kwa maslahi ya nchi na raisi akiwemo.

Mzaha mzaha siku moja mkulu hata kama amejificha Chato ila hata yeye hili janga linaweza kumpata jambo ambalo ni hatari kwani fununu zilizopo anamaradhi ya moyo kitu ambacho huu ugonjwa ukiupata ni ngumu sana kukuacha salama.

Ni kweli tunahitaji kodi ya mapato ila atambue corona haichagui kiongozi.
 
Mimi nafikiri tunachoweza kuwaambia kwa sasa ni, wavae barakoa, wanawe maji tiririka na sabuni, watumie sanitizer, watulie nyumbani...
 
Sasa wao watafanya nini? Washauri kuhusu nini labda? au watoe suluhu ipi? ukiona kimya jua na wao hawana majibu

Mkuu hawa ni wana wa nchi hii hii. Wanawajibika kama ulivyo wewe na mimi kujihusisha na ustawi wa nchi hii.

Marehemu baba wa taifa (rip) hakuwa na simile kwenye mambo yaliyogusa ustawi wa nchi yetu.

Wazee wetu wastaafu hawa tunashitakiwa sana sasa labda kuliko wakati mwingine kwa ushauri, uzoefu na kuvumiliana.

Penye wengi hakuharibiki jambo.
 
Mimi nafikiri tunachoweza kuwaambia kwa sasa ni, wavae barakoa, wanawe maji tiririka na sabuni, watumie sanitizer, watulie nyumbani...

Hapana mkuu hawa wanaweza kuwa pekee wakombozi wetu kwa hali ya sasa.
 
Hatuombi mabaya lakini corona haichagui nyazifa ya mtu,Tunapopaza sauti ni kwa maslahi ya nchi na raisi akiwemo.

Mzaha mzaha siku moja mkulu hata kama amejificha Chato ila hata yeye hili janga linaweza kumpata jambo ambalo ni hatari kwani fununu zilizopo anamaradhi ya moyo kitu ambacho huu ugonjwa ukiupata ni ngumu sana kukuacha salama.

Ni kweli tunahitaji kodi ya mapato ila atambue corona haichagui kiongozi.

Mkuu sielewi kwa nini waungwana wanakuwa na kigugumizi.

Hadi sasa haupo mkakati wa kuutokomeza huu ugonjwa. Ugonjwa huu hauwezi kuondoka wenyewe kama mvua.

Tunapaswa kuwa na mkakati uliokuwa wazi wa kupambana na hili gonjwa.

That's the only way out.
 
Hulijui taifa linaloangamia? Au bado ungali na maluweluwe ya kujifukiza nyungu?

Kwa mawazo yako mmeliokoa taifa na maangamizi ya ugonjwa huu kwa kupiga nyungu?

Hivi misukule nyie ni binadamu kama wengine?
Usiwe kapumbavu!

Wewe unapemdekeza hatua gani.?

Huu ni ugonjwa wa dunia nzima, hauna dawa, tahadhali za kuchukua unaambiwa kila siku.

Sasa unataka hao wastaafu wafanyaje? Wana dawa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usiwe kapumbavu!

Wewe unapemdekeza hatua gani.?

Huu ni ugonjwa wa dunia nzima, hauna dawa, tahadhali za kuchukua unaambiwa kila siku.

Sasa unataka hao wastaafu wafanyaje? Wana dawa?

Sent using Jamii Forums mobile app

Wewe kapu***vu endelea kufuka nyungu! Huku unatafuta nini? Bado hujakolea.

Wastaafu wana mengi ya kufanya. Unadhani wao ni mazwazwa kama wewe?

Waache wazee wetu wautendee haki uzee wao. Kwa sasa wao ni tegemeo kubwa kwetu.

Wewe chochea nyungu sorry we don't need you. Zaidi ya matusi, you have nothing to offer.

Msukule wahedi wee!
 
Kwenu marais wetu Wastaafu, Mwinyi, Mkapa na rais Kikwete.

Kwa heshima na taadhima inafikirisha kuwaandikia waraka huu baada ya kuwa kwa dhati kabisa, njia nyingi zimejaribiwa kushauri, kuhimiza, kuomba, kuisihi nk ili kuwepo mtizamo tofauti kuhusiana na ugonjwa huu.

Nchi hii ni yetu sote kiasi kuwa kwa yeyote yule, awe mkubwa au mdogo kunyamaza kimya tu wakati ni wazi kuwa labda tunakoelekea sasa siko, siyo jambo ambalo tunaweza kulichagua kama moja ya uwezekano tena.

Waheshimiwa katika nyakati tofauti mmewahi kupokea hatamu za serikali na kuiongoza nchi hii pendwa kama watakavyo kuja na kutoka wengine kwa njia za amani. Siyo siri kuwa kama marais wastaafu nafasi yenu ya kulitumikia taifa hili ingalipo. Ni wazi kuwa, katu marehemu baba wa taifa (rip) asingelikubali kuliacha taifa hili ambalo limekuwa la kupigiwa mfano siku zote kuangamia.

Waheshimiwa, msiliache taifa hili kuangamia na ugonjwa huu huku mkiangalia tu. Mnayo nafasi ya kuliunganisha taifa hili kuwa moja ili kwa pamoja tukaishinda Corona kwa salama.

Shime waheshimiwa msilinyime taifa hili hekima wala busara zenu, ambazo kwa hakika zinahitajika sana kwa sasa labda kuliko kipindi kingine chochote kilichowahi kupita.

Kwa umoja wenu kama wananchi wa nchi hii au katika nafasi zenu ka mtanzania mmoja mmoja mnayo nafasi ya kushauriana na mheshimiwa rais kwa niaba yetu sisi wananchi.

Umoja wetu utokanao na kushawishiana kwa nguvu za hoja si hoja za nguvu utatuvusha katika vita hivi.

Kama watanzania tunastahili kuushinda ugonjwa huu kama jambo la dharura kweli kweli vinginevyo kama ilivyo wazi, maisha ya wengi wetu yako hatarini mno.

Mungu ibariki Tanzania. Mungu tujalie salama tunavyomuunga kupambana na ugonjwa huu.

Nawasilisha.
Brazaj kwanini hujamtag Mzee Mtei?
 
Brazaj kwanini hujamtag Mzee Mtei?

Mzee Mtei ndiyo nani? Kwa nini wewe hujamtag?

Au mkuu bandiko lako ni kwa uzi upi?

Angalieni vijana isije kuwa hizi nyungu na kitu cha Arusha kimo. Si unajua uchizi hakunaga hodi?
 
Back
Top Bottom