Waraka wa wanafunzi wa elimu ya juu kwa rais jk.

Sitachoka

JF-Expert Member
Nov 17, 2011
3,030
1,303
Ufuatao ni waraka wa wanafunzi
wa elimu ya juu nchini kwa
Serikali, kuhusu migomo na
maandamano ya mara kwa mara
hapa nchini. Umeandikwa na
jopo la viongozi wa wanafunzi
wa vyuo vikuu na wameupeleka
serikalini. Wanatoa ushauri
maridhawa wa namna ya
kukomesha migomo kwa
kuboresha sekta ya elimu, hasa
kwa kuwapa fursa wanafunzi
wote bila ubaguzi. Waraka huu ni
mrefu na JAMHURI itauchapisha
wote kuanzia leo. Endelea…
Tunapenda kuchukua fulsa hii
kwanza kuomba msamaha na
kuwataka radhi wazazi wetu
mliotutuma kwenda kutafuta
elimu vyuo vikuu hapa nchini,
kutokana na vurugu, migomo na
maandamano ya mara kwa mara.
Mambo hayo mmekuwa
mmekuwa mkiyasikia au
mkiyaona kupitia vyombo vya
habari yakitokea katika vyuo
mbalimbali hapa nchini.
Pia tunaomba radhi kutoka
mioyoni mwetu kwa walimu
wetu (lecturers) kwa adha
inayowakuta inapotokea
migomo na maandamano.
Pia tunawaomba msamaha
viongozi wetu wa dini ambao
kwa namna moja ama nyingine,
wamekuwa wakitulea kiroho na
kimaadili. Lakini tutakuwa
hatujawatendea haki Watanzania
ambao kodi zao ndizo
zinazogharamia elimu yetu hapa
chini.
Bila shaka walitarajia kutuona
tukisoma kwa bidii na kufaulu
vuzuri, ili tutakaporudi katika
jamii zetu tutumie elimu
tuliyoipata kuwakomboa
Watanzania wenzetu, ambao
hadi sasa wanalia na kuangamia
na vita kubwa ya Ujinga,
Umaskini, Maradhi na Ufisadi,
lakini wameendelea kushuhudia
migomo na maandamano ya
mara kwa mara yasiyo na
kikomo.
Baada ya kutafakari kwa kina
kama wasomi, tukaona kama
hatutakaa chini na kufanya utafiti
(research) wa vyanzo na sababu
zinazotufanya tuwe na migomo,
tuandamane na kufanya vurugu
za mara kwa mara vyuoni.
Hatutaeleweka na tutaonekana
kweli sisi ni wahuni, au
tunatumiwa na watu ama
wanasiasa wakati hizi ni tuhuma
ambazo hazina ukweli hata
chembe ndani yake.
Lakini tunapenda kuwataarifu
viongozi wetu, wazazi na
Watanzania kwa jumla, kwamba
matatizo haya yanatokana na
vitendo vichafu vya baadhi ya
watumishi pamoja na sera
mbovu za kikandamizaji,
kibaguzi, manyanyaso na uonevu
uliovuka mipaka kwa wanafunzi
wa elimu ya juu (vyuo vikuu).
Na hatutaeleweka kwa walimu
wetu waliojitolea kwa uzalendo
wao wa hali ya juu, kutufundisha
japo masilahi yao ni madogo
ukilinganisha na kazi kubwa
wanayoifanya.
Pia kama tungekaa kimya,
viongozi wetu wa dini ambao ni
walezi wetu wa kiroho na
maadili wasingetuelewa. Vilevile
hatutaeleweka zaidi kwa
Watanzania ambao wanatozwa
kodi kwa ajira ya kugharamia
elimu yetu ya juu, ili tusome kwa
bidii ili turudi kulitumikia taifa.
Tumefanya utafiti huu wa
migomo, vurugu na
maandamano ya mara kwa mara,
ili tutoe taarifa ya upande wa pili
wa wanafunzi, kwani kumekuwa
na desturi au utamaduni wa
vyuo kutoa taarifa zisizokuwa na
ukweli kwa wananchi (umma),
kwa kuwasingizia wanafunzi
kwamba wanatumiwa na
viongozi wa siasa kufanya fujo,
vurugu na migomo matatizo
haya yanapojitokeza.
Taarifa hizi zisizokuwa na ukweli
zimekuwa zikitolewa na baadhi
ya watawala wa vyuo, ili
kukwepa kutekeleza madai yetu
ya msingi kwa kisingizio hiki
kisicho na ukweli ndani yake,
kama ilivyonekana katika gazeti
la Mtanzania toleo namba na
5842 la Jumapili Januari 15,
2012.
Kuna makala yenye kichwa cha
habari kilichoandikwa kwa
herufi kubwa na kusomeka:
Vurugu UDSM: Uongozi wa chuo
wadai waliofukuzwa ni
wanasiasa.
Habari kama hiyo ilichapishwa
katika gazeti la Uhuru ilisomeka,
“Vurugu za: Chama cha …
cashukiwa kuwa nyuma ya
mgomo’. Gazeti la Mzalendo la
Januari 15, 2012 lilikuwa na
makala yenye maudhui kama
hayo.
Kwa bahati mbaya, kwa upande
wa wanafunzi hatukupata nafasi
ya kukanusha madai hayo kwa
ushahidi wa wazi kwa wazazi,
walimu, viongozi wetu wa dini
na Watanzania waliolipa kodi
zinazotusomesha, wakaamini
madai yaliyotolewa na Serikali na
utawala wa chuo kuwa ni sahihi.
Wakatuhukumu na kuwafukuza
chuo wenzetu kwa kutuhusisha
kutumiwa na vyama vya siasa,
kitendo ambacho si kweli.
Walifanya hivyo ili kukwepa na
kupinga hoja na madai yetu ya
msingi kwa majibu mepesi eti
tumetumwa, ni ajabu kweli!
Namna hii siasa zinavyoingizwa
katika chuo, matokeo yake chuo
kinakuwa sehemu ya kisiasa,
jambo ambalo si sahihi. Chuo ni
taasisi inayojitegemea, hivyo
inapaswa kuendesha mambo
yake bila kuingiliwa na taasisi
nyingine.
Hali hii ikiachwa iendelee kama
Serikali haitatekeleza
mapendekezo yetu ambayo ni
njia sahihi ya kupunguza vurugu,
migomo na maandamano, vyuo
vikuu nchini kama siyo kumaliza
kabisa, tutaomba wazazi wetu,
walimu wetu na Watanzania
walipa kodi mtuelewe kwa
uamuzi mgumu tutakaochukua
kama itakavyoonekana inafaa.
Lakini vyuo vikuu vitapoteza sifa
yake ya ndani na nje ya nchi.
Vitabaki ni vyuo vya migogoro ya
migomo, vurugu na
maandamano miaka nenda rudi.
Kufukuza wanafunzi si
mwarobaini wa tatizo kwani
maandamano, vurugu, migomo
itaendelea kuwapo endapo
madai na mahitaji ya wanafunzi
hayatatekezwa.
Yapo madhara makubwa
ambayo yanatokana na migomo
vyuoni, yakiwamo ya kuharibiwa
kwa rasilimali za chuo, kuharibu
ratiba za masomo, Serikali
kuingia hasara na gharama za
ziada chuo kinapofungwa kwa
mgomo, kwani bajeti ya chuo
inakuwa ilishapitishwa, na
gharama za kupeleka polisi na
magari ya maji ya kuwasha na
mabomu ya machozi zinakuwa
mzigo.
Kibaya zaidi ni kwa wanafunzi
kufukuzwa na kusimamishwa
masomo, ambao
wamegharamiwa na kodi za
Watanzania wakitarajiwa
kuhitimu na kurejesha mikopo
na kulitumikia taifa letu.
Tunaomba wazazi, walimu,
viongozi wetu wa dini na
Watanzania walipa kodi, kwa
pamoja mtumie fursa hii
kuishauri Serikali kutekeleza
mapendekezo yetu, ili kuinusuru
sekta mama ya elimu nchini
isiyumbe na kuporomoka kwa
kasi ya ajabu.
Ni matumaini yetu kila kundi
litatumia nafasi yake kuishauri
Serikali kupokea mapendekezo
yetu.
Ili binadamu aweze kuzikabili
changamoto za maisha na
kujikomboa katika lindi la
umasikini, lazima awe na elimu.
Elimu ndiyo msingi wa
kujitambua, kuyatawala na
kuyatumia mazingira anamoishi
binadamu ili kuboresha maisha
yake na kujiletea maendeleo ya
haraka.
Ni wazi kuwa elimu ndiyo
ukombozi wa binadamu kuiona
kesho iliyo bora zaidi na
kuogelea katika bahari ya
utandawazi, ambayo inamtaka
kila mmoja aogelee kwa namna
awezavyo.
Kwa kutambua ukweli huo,
Serikali ya Tanzania imetoa fursa
kwa wadau wa elimu kuwekeza
katika sekta hiyo, ili kujenga taifa
la watu wenye maarifa, ujuzi na
uwezo wa kuzalisha.
Dira ya Taifa ya Maendeleo ya
mwaka 2025, Mkakati wa Kukuza
Uchumi na Kupunguza Umasikini
Tanzania (MKUKUTA) pamoja na
Sera ya Elimu na Mafunzo, vyote
vinaeleza umuhimu wa elimu ili
kuiwezesha nchi kusonga mbele.
Watanzania na wazazi kwa
ujumla wanatarajia kuona
watoto wao wanapata maarifa
na uwezo, ili wachangie juhudi
za Watanzania na wazazi wao
kutatua changamoto zilizopo
katika jamii.
Wanafunzi wenye maarifa na
ujuzi huwa na uwezo wa
kufanya mambo mengi mapya
kwa usahihi na kuwaongoza
wenzao. Katika maendeleo ya
ukweli katika jamii tunamoishi,
matendo ya wasomi, kazi zao,
majukumu yao na shughuli
wanazofanya zinapaswa
kudhihirisha matunda ya elimu
waliyonayo.
Zao muhimu la elimu kwa mtoto
ni kuwa na uwezo mkubwa wa
kufikiri kwa makini. Uwezo huu
ndiyo unaohitajika sana katika
jamii ya leo. Mtu mwenye uwezo
wa kufikiri ndiye mwenye nguvu
ya kuibua dhana mpya na
kutafuta njia mbadala za kutatua
matatizo.
Watu walioibua teknolojia
tulizonazo waliongozwa na upeo
wa kufikiri ndipo wakaibuka na
dhana mpya. Tendo la kufikiri
lipo ndani ya akili na utashi wa
mtu. Bila kufikiri matokeo ya
juhudi za mtu mara nyingi huwa
anguko au hasara.
Serikali pamoja na wadau wa
elimu nchini, wana mchango
mkubwa wa kuibua taifa la
wasomi na kutekeleza Dira ya
Taifa ya Maendeleo ya Mwaka
2025, MKUKUTA na Sera ya Elimu
na Mafunzo ambavyo vyote
vinaeleza umuhimu wa elimu ili
kuiwezesha nchi kusonga mbele.
Kukua kwa uchumi pamoja na
mambo mengine hutegemea
uwekezaji hasa wenye manufaa
kama elimu, ili kupata wataalamu
ambao ndiyo watakaoinua
uchumi wetu. Kimsingi, uchumi
hauwezi kukua bila wasomi. Nchi
lazima iandae rasilimali watu
wanaohitajika ili kuinua uchumi
wa nchi yetu na kusaidia familia
zao masikini.
Rais wa Kwanza wa Tanganyika
(Tanzania Bara) aliwahi kusema
maneno yafuatayo katika hotuba
zake kwa wananchi kwamba:
“Hakuna Serikali yoyote duniani
inayowawekea wananchi wake
hela mfukoni, bali “the only best
way to enrich a poor people is to
educate their children” yaani njia
pekee ya kuwasaidia wananchi
masikini ni Serikali
kuwasomeshea watoto wao.
Kwa hili alikusudia kwamba
ukimsomesha mtoto wa maskini,
atakapopata hiyo elimu ataitumia
kuinua familia yake kiuchumi na
taifa kwa jumla. Ndiyo maana
baada ya kupata Uhuru, Mwalimu
Julius Nyerere alitambua maadui
watatu- Maradhi, Umaskini na
Ujinga.
Lakini ili ukabiliane na maadui
hawa, lazima uanze na adui
‘ujinga’ kwa kutoa elimu bora
kwa wananchi ili waondoe
umasikini na maradhi. Lakini
tumeshuhudia Serikali kwa sasa
inavyosuasua katika sekta hii
muhimu ya elimu nchini.
Katika Katiba ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania ibara ya
9 kifungu kidogo cha (i), inasema
hivi: “Matumizi ya utajiri wa Taifa
yanatilia mkazo maendeleo ya
wananchi na hasa zaidi
yanaelekezwa kwenye jitihada ya
kuondosha umasikini, ujinga na
maradhi.”
Kama tulivyosema, baada ya
Uhuru wa Tanganyika mwaka
1961, na baadaye Muungano wa
Tanganyika na Zanzibar mwaka
1964, Mwalimu Nyerere
alitangaza vita kwa maadui
watatu - Ujinga, Maradhi na
Umasikini.
Mwalimu alihakikisha
anafanikiwa katika mapambano
hayo. Alianza kuweka mikakati
mbalimbali ikiwa ni pamoja na
kukazia elimu ili kufuta ujinga,
kupatikana madaktari wa
kupambana na adui maradhi na
wataalamu wa uchumi wa
kupambana na adui umasikini.
Fikra hii ya Mwalimu ilidumu hadi
kufikia maziko ya Azimio la
Arusha na kuanzishwa Azimio la
Zanzibar Februari 1991 lililoamua
kufuata mfumo wa kibepari
uliokusudia kumilikisha rasilimali
ya Tanzania kwa wachache.
Baada ya hapo, maadui hawa
waliwavamia Watanzania. Ujinga
ulianza kuongezeka (idadi ya
watu wasiojua kusoma na
kuandika iliongezeka), maradhi
yakaongezeka - vifo kwa mama
na mtoto; uchumi ukadorora,
umasikini ukaongezeka, shilingi
ya Tanzania ikashuka thamani
siku hadi siku huku mfumuko wa
bei ya bidhaa ukiwaumiza
wananchi wa kipato cha chini.
Hilo ndilo Azimio la Zanzibar.
 
Waache siasa wasome,

Na ndio maana tunapata watendaji wabovu na wezi kwenye idara zetu, mitoto imekuwa mivivu kila kukicha inataka kugoma
 
Waache siasa ili iweje. Au hujui maana ya siasa. Ukiacha siasa unakuwa mfu ndani ya jamii. Au bado unafikiri siasa ni uongo. Siasa ni Art and Science of social life. Is a way of life.
 
Waache siasa ili iweje. Au hujui maana ya siasa. Ukiacha siasa unakuwa mfu ndani ya jamii. Au bado unafikiri siasa ni uongo. Siasa ni Art and Science of social life. Is a way of life.

Jifunze tofauti ya viunganishi and na or, usije aibika! ukisema art and science ni tofauti na kusema art or science!

Kaangalie upya tafsiri ya siasa!
 
"No person shall be condemed unheard" Wasiposikilizwa wakigoma msiseme wametumwa! Huo ni mwanzo mzuri!
 
Kwanza watuambie kama wao sio miongoni mwa waliondama kwenda kwa Nape kuipongeza CCM na JK siku chache zilizopita au?
 
Migomo duniani kote wanafunzi wanafanya sema Rais asake njia ya kuipunguza tu
 
Waache siasa wasome,

Na ndio maana tunapata watendaji wabovu na wezi kwenye idara zetu, mitoto imekuwa mivivu kila kukicha inataka kugoma

Kichwa chako kina shida sana....you don't even spend a second to think before you write your s.t.u.p.i.d.i.t.y....JK alianzia wapi siasa? Nyerere alianzia wapi siasa? Nkwame alianzia wapi siasa? Mbona hawa waliondamana juzi kuupongeza uamuzi wa cc ya ccm kuwaondoa wabunge wa ccm wezi haukusema kuw waache siasa wasome???? I do not think if you really make your BRAIN participate in your decision making? Bado unaamini kuwa ccm itatawala milele na ndiyo mbinu za ccm kusema kuwa wanafunzi wa vyuo vikuu waache siasa vyuoni wasome huku wao wakitafuna nchi...kama wasomi watakaa kimya nani atasema? Ilikuwa enzi zile....kitabu tunapiga na siasa kama kawa....imekula kwenu...!!!

STK ONE,
 
Kwanza watuambie kama wao sio miongoni mwa waliondama kwenda kwa Nape kuipongeza CCM na JK siku chache zilizopita au?

hiyo ni double standard ya nchi yetu. Wanapenda kusikia kwamba wanachuo wote wanaipenda ccm basi! Wakisikia kuna wanaodai haki zao wanasema ni wafuasi na wamechochewa na cdm. Miaka ya nyuma sita aliwahi kuongoza mgomo udsm mpaka akachapwa viboko na jkn,sijui ni cdm gani ya wakati ule iliwachochea.
 
Migomo duniani kote wanafunzi wanafanya sema Rais asake njia ya kuipunguza tu

serikali nyingi duniani ambazo ni dhaifu zimeangushwa/ziliangushwa na migomo ya wanachuo mf venezuela. Tanzania sio nchi ya kwanza kuwa na maandamano hayo.
 
wamenena. tuwasikilize na kufanyia kazi dukuduku zao.

Waraka huu ni
mrefu na JAMHURI itauchapisha
wote kuanzia leo. Endelea…
Tunapenda kuchukua fulsa hii
kwanza kuomba msamaha na
kuwataka radhi wazazi wetu
mliotutuma kwenda kutafuta
elimu vyuo vikuu hapa nchini,
kutokana na vurugu, migomo na
maandamano ya mara kwa mara.
Mambo hayo mmekuwa
mmekuwa mkiyasikia au
mkiyaona kupitia vyombo vya
habari yakitokea katika vyuo
mbalimbali hapa nchini.
Pia tunaomba radhi kutoka
mioyoni mwetu kwa walimu
wetu (lecturers) kwa adha
inayowakuta inapotokea
migomo na maandamano.
Pia tunawaomba msamaha
viongozi wetu wa dini ambao
kwa namna moja ama nyingine,
wamekuwa wakitulea kiroho na
kimaadili. Lakini tutakuwa
hatujawatendea haki Watanzania
ambao kodi zao ndizo
zinazogharamia elimu yetu hapa
chini.
Bila shaka walitarajia kutuona
tukisoma kwa bidii na kufaulu
vuzuri, ili tutakaporudi katika
jamii zetu tutumie elimu
tuliyoipata kuwakomboa
Watanzania wenzetu, ambao
hadi sasa wanalia na kuangamia
na vita kubwa ya Ujinga,
Umaskini, Maradhi na Ufisadi,
lakini wameendelea kushuhudia
migomo na maandamano ya
mara kwa mara yasiyo na
kikomo.
Baada ya kutafakari kwa kina
kama wasomi, tukaona kama
hatutakaa chini na kufanya utafiti
(research) wa vyanzo na sababu
zinazotufanya tuwe na migomo,
tuandamane na kufanya vurugu
za mara kwa mara vyuoni.
Hatutaeleweka na tutaonekana
kweli sisi ni wahuni, au
tunatumiwa na watu ama
wanasiasa wakati hizi ni tuhuma
ambazo hazina ukweli hata
chembe ndani yake.
Lakini tunapenda kuwataarifu
viongozi wetu, wazazi na
Watanzania kwa jumla, kwamba
matatizo haya yanatokana na
vitendo vichafu vya baadhi ya
watumishi pamoja na sera
mbovu za kikandamizaji,
kibaguzi, manyanyaso na uonevu
uliovuka mipaka kwa wanafunzi
wa elimu ya juu (vyuo vikuu).
Na hatutaeleweka kwa walimu
wetu waliojitolea kwa uzalendo
wao wa hali ya juu, kutufundisha
japo masilahi yao ni madogo
ukilinganisha na kazi kubwa
wanayoifanya.
Pia kama tungekaa kimya,
viongozi wetu wa dini ambao ni
walezi wetu wa kiroho na
maadili wasingetuelewa. Vilevile
hatutaeleweka zaidi kwa
Watanzania ambao wanatozwa
kodi kwa ajira ya kugharamia
elimu yetu ya juu, ili tusome kwa
bidii ili turudi kulitumikia taifa.
Tumefanya utafiti huu wa
migomo, vurugu na
maandamano ya mara kwa mara,
ili tutoe taarifa ya upande wa pili
wa wanafunzi, kwani kumekuwa
na desturi au utamaduni wa
vyuo kutoa taarifa zisizokuwa na
ukweli kwa wananchi (umma),
kwa kuwasingizia wanafunzi
kwamba wanatumiwa na
viongozi wa siasa kufanya fujo,
vurugu na migomo matatizo
haya yanapojitokeza.
Taarifa hizi zisizokuwa na ukweli
zimekuwa zikitolewa na baadhi
ya watawala wa vyuo, ili
kukwepa kutekeleza madai yetu
ya msingi kwa kisingizio hiki
kisicho na ukweli ndani yake,
kama ilivyonekana katika gazeti
la Mtanzania toleo namba na
5842 la Jumapili Januari 15,
2012.
Kuna makala yenye kichwa cha
habari kilichoandikwa kwa
herufi kubwa na kusomeka:
Vurugu UDSM: Uongozi wa chuo
wadai waliofukuzwa ni
wanasiasa.
Habari kama hiyo ilichapishwa
katika gazeti la Uhuru ilisomeka,
“Vurugu za: Chama cha …
cashukiwa kuwa nyuma ya
mgomo’. Gazeti la Mzalendo la
Januari 15, 2012 lilikuwa na
makala yenye maudhui kama
hayo.
Kwa bahati mbaya, kwa upande
wa wanafunzi hatukupata nafasi
ya kukanusha madai hayo kwa
ushahidi wa wazi kwa wazazi,
walimu, viongozi wetu wa dini
na Watanzania waliolipa kodi
zinazotusomesha, wakaamini
madai yaliyotolewa na Serikali na
utawala wa chuo kuwa ni sahihi.
Wakatuhukumu na kuwafukuza
chuo wenzetu kwa kutuhusisha
kutumiwa na vyama vya siasa,
kitendo ambacho si kweli.
Walifanya hivyo ili kukwepa na
kupinga hoja na madai yetu ya
msingi kwa majibu mepesi eti
tumetumwa, ni ajabu kweli!
Namna hii siasa zinavyoingizwa
katika chuo, matokeo yake chuo
kinakuwa sehemu ya kisiasa,
jambo ambalo si sahihi. Chuo ni
taasisi inayojitegemea, hivyo
inapaswa kuendesha mambo
yake bila kuingiliwa na taasisi
nyingine.
Hali hii ikiachwa iendelee kama
Serikali haitatekeleza
mapendekezo yetu ambayo ni
njia sahihi ya kupunguza vurugu,
migomo na maandamano, vyuo
vikuu nchini kama siyo kumaliza
kabisa, tutaomba wazazi wetu,
walimu wetu na Watanzania
walipa kodi mtuelewe kwa
uamuzi mgumu tutakaochukua
kama itakavyoonekana inafaa.
Lakini vyuo vikuu vitapoteza sifa
yake ya ndani na nje ya nchi.
Vitabaki ni vyuo vya migogoro ya
migomo, vurugu na
maandamano miaka nenda rudi.
Kufukuza wanafunzi si
mwarobaini wa tatizo kwani
maandamano, vurugu, migomo
itaendelea kuwapo endapo
madai na mahitaji ya wanafunzi
hayatatekezwa.
Yapo madhara makubwa
ambayo yanatokana na migomo
vyuoni, yakiwamo ya kuharibiwa
kwa rasilimali za chuo, kuharibu
ratiba za masomo, Serikali
kuingia hasara na gharama za
ziada chuo kinapofungwa kwa
mgo
 
Ngoja nilale kwanza halafu nirudi kumalizia kuusoma huu waraka, ...
 
Usiseme walaka wa wanafunzi wa vyuo vikuu. Taja chuo husika sisi wengine mbona hatuujui huo?? Na utakuwa walaka wa wanafunzi wa UDOM.
 
Back
Top Bottom