Kwa upande wa Waislamu, zoezi la uchaguzi ujao linaweza kuwa Ibada na hatua muhimu ya kuwakomboa na hatimaye kuwapatia fursa muhimu kama ilivyo kwa raia wenzao Wakiristo. Haya yatategemea maamuzi na umakini wao wakati wa kuchagua wagombea udiwani, ubunge na urais. Ni kwa sababu hii basi, Shura ya Maimamu Tanzania inaona ni wajibu wake kutoa muongozo huu kwa Maimamu kwa lengo la kuwaandaa Waislamu kote nchini kushiriki uchaguzi ujao kwa kuzingatia maslahi ya Waislamu na Uislamu wao.
(17) HITIMISHO
Kwa kulitambua hilo, Shura kupitia kamati zake za siasa ambazo ni, kamati kuu, kamati za Mikoa, Wilaya/Majimbo na kamati za Kata, zimejitwisha dhima ya kuhakikisha kuwa Waislamu wa Tanzania kama Waislamu wanaingia katika uchaguzi ujao Kuingia katika uchaguzi kama Waislamu hakuna maana ya kupigia kampeni chama chochote cha siasa, kwani katika vyama vyote vilivyopo hakuna chama kilicho sajiliwa kama chama cha Waislamu wala cha Kiislamu.
Hii ndiyo elimu ya uraia!
Katika taarifa ya habari ya kituo cha luninga cha ITV, saa 02:00 usiku wa kuamkia uchaguzi, Mkuu wa Jeshi la Polisi (wakati huo) Bw. Omari Mahita alihitimisha kampeni za vitisho kwa Waumini wa Dini ya Kiislamu na kuwanasibisha wapinzani hususani CUF na visu kuwa ni silaha walizojiandaa nazo kwa ajili ya kuhatarisha amani nchini. Hauta hii ya mahita ilikuwa ni moja kati
Kamati Kuu ya Siasa ya Shura ya Maimamu Tanzania, ilimuandikia Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuomba kuruhusiwa kuweka waangalizi katika majimbo yote ya uchaguzi nchini
chaguzi zote za nyuma Waislamu wamekuwa wakipiga kura kwa kuzingatia zaidi umoja wa kitaifa na kile walichoamini kwamba ni maslahi ya Taifa. Pamoja na kuwa wao ndiyo kundi kubwa la kidini kuliko yote, mtizamo na msimamo huu umesababisha nguvu yao kisiasa kuwa dhaifu mno na hivyo kuathirika mno kijamii. Tofauti na Waislamu, Wakristo wao wamekuwa wakizingatia sana maslahi yao ya kidini kila wakati wa uchaguzi. Kutokana na mazingatio haya karibu viongozi wote wanaochaguliwa, hata wale ambao ni Waislamu wamejikuta wakiendesha shughuli za kila siku za nchi kwa kuzingatia maelekezo na maslahi ya kanisa na Wakristo. Kwa ujumla, kuna vielelezo vingi mno vinavyoashiria kuwa japo nchi yetu ni ya kisekula kikatiba, lakini kiutendaji inatawaliwa na ‘Mfumo Kristo'
Nimejitahidi kuusoma waraka huu kwa haraka haraka kwa kuwa sikuvutia kutumua muda wangu mwingi. Waraka unaonyesha uwezo mdogo walionao waandaaji hasa katika masuala ya siasa, dini na ushawishi kwa ujumala.
Waraka huu umekaa kama mhadhara wa kawaida kama ile ambayo huwa inatolewa ktk baadhi ya misikiti hapa bongo. Waraka umetumia kurasa nyingi kumlaumu Nyerere, Kanisa katoliki na ukristo kuliko mlengwa ambae ni Serikali.
Waraka haukujikita kuchambua sera bali umeonyesha baadhi ya yale yanayoonekana ni kero hasa kutokana na kutofuata sheria zilizopo. 35% unaongelea Kanisa Katoliki, 35% Uislam na waislam, 20% wakristo na 10% tu ndo inaongelea Serikali, Sera na uchaguzi 2010.
Binafsi waraka huu umenionyesha 'uwezo' wa wahusika katika kuyajua na kuchambua mambo.
Unafiki mtupu! kama ulisoma kwa haraka haraka hizo % ulizi compute wakati gani?
Ili uwe waraka mzuri lazima utoke kwa wakatoliki sio? mlishalikoroga subirini mlinywe sasa.
Hawa jamaa hawajui wanachofanya kaka. Na hii inatokana na uwezo mdogo wa elimu "DUNIA", kama wanavyoiita, walionao. Fikiria yafuatayo........Mi na wasiwasi na uwezo wa hawa watu kufikiri!
Hivi hawa jamaa wanajua wanachofanya kweli?
Unafiki mtupu! kama ulisoma kwa haraka haraka hizo % ulizi compute wakati gani?
Ili uwe waraka mzuri lazima utoke kwa wakatoliki sio? mlishalikoroga subirini mlinywe sasa.
Tutajadili vipi waraka ambao baraza la waisilamu mbalo ndilo linalotambuliwa na serikali hauutambui
Asanteni, Tumeusoma. Halafu mbona Mheshimiwa Kingunge Ngombale Mwiru haja comment? Au anawaogopa Waislamu? Mbona yeye anakomment za Wakatoliki tu? Mimi namwomba mheshimiwa Kingunge Ngombale Mwiru (kwa heshima na taadhima zote tulizo nazo kwake) atoe kommenti pia. mheshimiwa uko wapi? Toa kommenti. Kazi kwako Mheshimiwa Kingunge!